Tunahitaji baraza la vijana la taifa?

harakat

JF-Expert Member
Jul 4, 2011
2,888
1,347
Kutokana na kuwepo kwa vijana wengi kwenye siasa katika wakati huu kuna uhitaji mkubwa wa vijana
kuanzisha baraza huru la kitaifa la vijana ambalo haitafungamana na chama chochote cha siasa na wale halitakuwa
linabase moja kwa moja kwenye siasa za kukosoana kichama hii ni ili

1. kuwepo kwa umoja wa kitaifa baina ya vijana wote.
2.kuwepo na utanzania kwanza kabla ya kuzungumzia chama.
3.Vijana kujenga umoja wao pasi na itikadi za vyama vyao .
4.Kuondoa mgawanyiko unaoweza kujitokeza sasa kwa vijana wa taifa hili.
5.Kuwepo na kulindwa kwa maslahi ya taifa hili katika nyanja zote kupitia vijana.
6.kujenga sauti ya pamoja kutoka kwa vijana pasipo chama wala Dini zao.
Ili kufanikisha haya wana JF, mnaombwa kutoa maonoi yenu ya kina .


nawasilisha................................
 
Kaka umenena ila umesahau kwa sasa baraza la vijana lipo,mataatizo ya vijana yameanzishwa na kuasisiwa na ccm.
Taabu za vijana ndio mtaji wa ccm kwa hiyo ukianzisha hilo baraza maana yake unataka vijana wwote wanaoona kuwa ccm ni adui wao kuungana pamoja na kama ni hivyo huwezi kuwakataza kutokuwa na itikadi ya chama chochote.
Kwanza kwa taarifa yako vijana zaidsi ya robo tatu(haswa wasomi)ni wakereketwa wa mageuzi na wengi wao wanaielewa zaidi chadema kutokana na misimamo yao,kwa hiyo kwa sasa na vuguvugu lililopo huwezi kuitnganisha chadema na baraza la taifa la vijana.
Kwa kuanzia naomba uwasiliane na john heche.
 
Hatudanganyiki, kila chama na umoja wa vijana wake na asiyekua wake aelekee jiwa. Ni miaka mingapi sasa tangu tuanze kuomba chombo kama hicho tangu enzi za Mudhihir Mudhihir bila mafanikio kwa kuhujumiwa na CCM?

Leo hii wameona mafanikio ya CHADEMA na chombo chetu cha BAVICHA ndio muanze sijui kitu gani huko; tokeni hapa mchezo wenu huo wa karata tatu. Hatudanganyiki tena, mambo ni mbele kwa mbele mpaka kieleweke.

CHADEMA makao makuu, hebu wapeni nafasi BAVICHA iandae programu ya 'Operesheni Vijiji Zindukeni' ili mziki mkubwa zaidi ya ile Ilioonyeshwa na BAVICHA kule Igunga ishike kasi zaidi. Wapeni vitega uchumi vya kuanzia ili waimarike zaidi na zaidi.

BAVICHA na vijana wa vyuo vikuu wazaliwa wa Igunga, nawapeni hongera sana sana sana kwa kuchapa kazi kwa mtindo ambao haujawahi kufahamika nchini. Hakika nyinyi ni chachu wa mabadiliko ya kweli nchini.

Nasema tena hongereni sana!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom