Tuna Makumbusho ya miaka 5 lakini hatuna Makumbusho ya miaka 10

Bila bila

JF-Expert Member
Dec 20, 2016
21,494
37,786
1. Mwaka 1985-1995 Tanzania iliongozwa na Rais Alli Hassan Mwinyi. Alilirithi nchi iliyotoka kupigana Vita miaka 5 nyuma na kuacha uchumi uliodhoofika kiasi cha Rais wa nchi Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kuwataka Wananchi kufunga mikanda. Katika kipindi chake ndipo tulipoona Sera ya Soko huria (Yeye akiita Ruksa), Kurejeshwa Kwa mfumo wa kidemokrasia wa vyama vingi, Uhuru wa kukosoa, kufunguliwa Kwa wanasiasa waliokuwa kizuizini nk. Lakini mpaka Leo hakuna MAKUMBUSHO ya Mwinyi.

2. Mwaka 1995-2005 Tanzania ilikuwa chini ya Benjamin William Mkapa. Huyu ni Rais wa Kwanza Tanzania kuongoza nchi yenye upinzani rasmi wa Kisiasa baada ya ushindi wake katika sanduku la Kura dhidi ya Mgombea machachari Augustine Lyatonga Mrema (RIP). Huyu ndiye muasisi wa misingi ya uchumi unaotegemea pato la ndani Kwa kuanzisha mamlaka imara ya Mapato (TRA), Msamaha mkubwa wa madeni Kwa nchi, Ubinafsishaji wa mashirika ya Umma yaliyokufa au kudorora, akifungua uchumi wa kusini mwa Tanzania ulioathiriwa na Sera ya ukombozi wa Afrika, ujenzi wa miundombinu Kwa kauli yake ya "kusafiri Kwa Tax toka Mtwara hadi Bukoba, nk. Still hata huyu sijawahi kusikia MAKUMBUSHO ya Mkapa.

3. Mwaka 2005-2015 nchi iliongozwa na Jakaya Mrisho Kikwete akishirikiana Kwa karibu na Swaiba wake Waziri Mkuu Edward Ngoyai Lowassa. Huyu katika kipindi chake alijitahidi kuimarisha elimu Kwa kuhakikisha Kila Kata inakuwa na shule ya sekondari, Elimu Kwa walioikosa (MEMKWA), kuongeza miundombinu ya barabara, Uimarishaji wa demokrasia, Mchakato wa Katiba mpya japo haikufika mwisho nk. Mpaka Leo hakuna MAKUMBUSHO ya Kikwete.

4. Mwaka 2015-2020+ akaja jembe, tingatinga John Pombe Magufuli. Kwa miaka yake 5 na miezi 3 madarakani alijitanabaisha kama adui wa ufisadi, wizi, uzembe na udanganyifu. Muumini wa ujenzi wa miundombinu kama Msingi wa uchumi nk. Mwaka mmoja baada ya kifo chake tayari ana Makumbusho yake. Hivi ni serikali hii hii iliyoona aliyeongoza miaka 10 Hana cha kukumbukwa Bali aliyeongoza miaka 5? Au kuna mfadhili kajitolea kujenga na atatuwekea vitu vya kutukumbusha ukuu wa Mwendazale ndani ya miaka 5? Kama ni serikali basi kuna mahali hapako Sawa au Kwa makusudi mmeamua kuwadharau wengi na kumtukuza mmoja. Vinginevyo mtueleze vigezo mlivyotumia kufanya upendeleo huu.
 
Mjomba wewe utakuwa Msomali,siyo Mtanzania.Huyo mwamba kafanya mambo mengi yaliyowashinda watangulizi wake;serikali kuhamia Dodoma, Ujenzi wa Bwawa la Umeme Rufiji,Ujenzi wa reli ya SGR, kuondoa watumishi hewa na wenye vyeti feki kwenye system, kudhibiti madawa ya kulevya (Tanzania ilikuwa hub ya madawa ya kulevya), Ujenzi wa vituo vya Afya na hospitali za kanda nk.
Bado unataka niendelee?
 
Mjomba wewe utakuwa Msomali,siyo Mtanzania.Huyo mwamba kafanya mambo mengi yaliyowashinda watangulizi wake;serikali kuhamia Dodoma, Ujenzi wa Bwawa la Umeme Rufiji,Ujenzi wa reli ya SGR, kuondoa watumishi hewa na wenye vyeti feki kwenye system, kudhibiti madawa ya kulevya (Tanzania ilikuwa hub ya madawa ya kulevya), Ujenzi wa vituo vya Afya na hospitali za kanda nk.
Bado unataka niendelee?
Nimeorodhesha Kila mmoja aliyofanya. Hao wengine unawaona mapoyoyo hawakufanya lolote Ila Huyo Magufuli?
 
Mjomba wewe utakuwa Msomali,siyo Mtanzania.Huyo mwamba kafanya mambo mengi yaliyowashinda watangulizi wake;serikali kuhamia Dodoma, Ujenzi wa Bwawa la Umeme Rufiji,Ujenzi wa reli ya SGR, kuondoa watumishi hewa na wenye vyeti feki kwenye system, kudhibiti madawa ya kulevya (Tanzania ilikuwa hub ya madawa ya kulevya), Ujenzi wa vituo vya Afya na hospitali za kanda nk.
Bado unataka niendelee?
Acha undezi basi kwa hiyo hao wengine waliopita niwajinga. Magu alikuwa kiongozi mzuri ili alifanya propaganda nyingi ambazo zilimpa umaarufu kuliko hata taifa lenyewe. Uongozi ni kupokezana kijiti ukipewa unaanzia mwenzako alipoishia.
 
Magufuli kafanya mengi lakini kwa msingi ukiyojengewa na watangukizi wake, mtu kama mkapa ndio kajenga hii nchi kimfumo na kitaasisi, kwanni hana makumbusho?
 
Subiri muda si mrefu atajengewa sanamu la kumbukumbu pia...
 
Mjomba wewe utakuwa Msomali,siyo Mtanzania.Huyo mwamba kafanya mambo mengi yaliyowashinda watangulizi wake;serikali kuhamia Dodoma, Ujenzi wa Bwawa la Umeme Rufiji,Ujenzi wa reli ya SGR, kuondoa watumishi hewa na wenye vyeti feki kwenye system, kudhibiti madawa ya kulevya (Tanzania ilikuwa hub ya madawa ya kulevya), Ujenzi wa vituo vya Afya na hospitali za kanda nk.
Bado unataka niendelee?
Muwekee na kauli ya Mh Rais Mstaafu Mwinyi akimkubali Hayati JPM kwa aliyoyafanya akiwa Rais wa TZ
 
Kwa ufupi: yote yalifanyika chini ya miaka mitano. Tueleze ni Rais yupi alifanya mambo mengi hivi in the same time-frame.
ENf6knOX0AEwzJy.jpeg
 
Samia ni rais dhaifu sana, kila kukics anasumbuliwa sana na kivuli cha mwendazake, ndio maana kila siku safari za Chato haziishii wakati kuna mikoa mingine hajawahi kutia mguu kabisa

Tunahitaji Rais anayejiamini kuendesha hii nchi bila kujishtukia kila mara na atuondolee legacy mbaya ya mwendazake
 
mwamba kifo chake kuna nchi ambazo sikutegemea zilishusha bendera nusu mlingoti hadi ghana wametoa tuzo ya miundombinu.
 
Back
Top Bottom