Tumwache Hayati Magufuli apumzike

Nyakabindione

Member
Jan 5, 2015
7
1
TUMWACHE JPM APUMZIKE

Taifa lilipatwa na msiba mzito tarehe 17 Machi 2021 kwa kupotelewa na kiongozi wake shupavu, Rais wa Awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli. Kwa hakika, huu ni msiba mzito kwa taifa. Ni msiba mzito kwa sababu haijawahi kutokea katika historia ya nchi yetu rais aliyeko madarakani kufariki dunia. Ni ukweli usiopingika kwamba taifa lilitikisika pale msiba ulipotangazwa na aliyekuwa Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hasaan.

Baada ya kutangazwa msiba huo mzito, kuliibuka makundi mawili miongoni mwa Watanzania. Hilo halifichiki. Kuna kundi lililonesha 'kushangilia' msiba huu. Na kuna lile lililonesha 'kuomboleza' msiba huu. Maandishi yangu hayatajikita kuangalia sababu za haya makundi kushangilia na/au kuomboleza kwa wakati mmoja. Maandishi yangu yatajikita kuyaomba au kuyaasa makundi haya KUMWACHA JPM APUMZIKE.

Kwa nini naandika kuyaomba makundi haya KUMWACHA JPM APUMZIKE? Ninawiwa kuandika hivyo kwani kadri siku zinavyokwenda, majibizano ya makundi haya nayo yanaongezeka. Ripoti ya CAG nayo kwa namna moja imekuja kuongeza majibizano haya. Wapo waliofikia kumtuhumu mpaka CAG kwamba ripoti yake ni ya uongo na kwamba imeandaliwa mahsusi kumchafua JPM. Hii siyo halali kabisa. Hatumtendei haki marehemu.

Iko wazi, kama binadamu JPM alitenda mambo mbalimbali. Yapo mazuri, yapo mabaya pia. Mazuri yaliwafurahisha wote au wengi. Mioyo yao ilinawiri na kupata bashasha. Mabaya yaliwakasirisha walioguswa. Yapo mabaya pia yaliyowaumiza watu na watu wao. Mioyo yao ikaumia, nafsi zao zikakasirika na kusinyaa. Ni sehemu ya ubinadamu wake.

Wakati nasoma Kidato cha Pili, mwalimu wangu wa Fizikia alinifundisha Newton's Laws of Motion tatu. Kuna ya kwanza, ya pili na ya tatu. Kanuni ya tatu inasema, "To every action, there's an equal and opposite reaction". Sina uhakika kama nimeinukuu kwa usahihi. Lakini lengo langu hapa ni kutumia maudhui yake tu katika mjadala wangu. Kwa tafsiri isiyo rasmi, "Kwa kila tendo, kuna mwitikio ulio sawa au ulio kinyume na tendo husika". Mtu ukimpa mkate naye atakupa juisi. Lakini ukimpa konzi, naye atakupa kofi!

Kwa wale tunaomthamini marehemu JPM tuwe wa kwanza kumtakia mapumziko mema. Mazuri yake yanajulikana na yanaonekana. Hayahitaji kuhubiriwa. Tunapozidi kuyaandika mtandaoni au hata kuyasimulia kwenye vyombo vya habari, tunatonesha vidonda vya wale walioumia, waliokasirika na kusinyaa mioyo. Tuyaache mazuri yake yajitangaze yenyewe ili kuwaziba midomo pia wanaoandika au kusimulia mabaya yake. Kwa kufanya hivi, tutakuwa tumemtendea haki marehemu. Haki yake ya kupumzika.

R. I. P JPM.
 
Mkuu JIWE alikuwa katili sana ,alikuwa hana huruma akiwa behind the scenes ,achana na maigizo ya kuwapa hela barabarani watu huku TV zikimuonyesha.

-Kufukuza vyeti feki karibu elfu 11 bila kuangalia familia ngapi zitateseka ,mbali na kuwafukuza pia akawanyima stahili/stahiki zao,kama ulivyosema hakuna binadamu asiyefanya makosa ,na pia JIWE alitakiwa atumie busara,hata wao kuna mambo mengi wanafanya tena yenye makosa makubwa lakini hakuna wakumgusa,kavunja katiba sana ambayo aliapa kuilinda(Kitendo cha kuvunja katiba basi na yeye kilimdisqualify nafasi ya urais)

-Kuzuia fao la kujitoa , kaumiza wafanyabiashara wakafunga biashara zao ,wafanyakazi wakapata redundancy then akazuia mafao,huyo alikuwa anajali wanyonge kweli? JK ndani ya wiki 3 ukiacha kazi ulikuwa unavuta MTONYO wako wote.

-Hakuna nyongeza ya miashara kwa kipindi chake chote cha miaka 6...yeye kila kitu analipiwa na mabilioni alikuwa anapewa kwenye bajeti ya ikulu ila wafanyakazi mshahra wao wa laki 3 toka enzi za JAKAYA mpaka leo hajapandishiwa.

-Wafanyabiashara kufilisiwa ,kufungwa ,kutekwa ,kuuwawa.

-Kuua/kuteka/kutesa wapinzani.

-Biashara ya utumwa aka Ng'ombe wasio na mkia aka makalai aka Gweregwere ilishamiri sana enzi za JIWE na alikuwa anatumia fedha nyingi kununua wapinzani.
 
Kipindi cha utawala wake hakutuacha tupumzike hata kidogo kwa muda wa miaka 5 mfululizo, alikua ni mwendo wa kutufokea na kututukana, na alidiriki kutupangia mpaka muda wa mapumziko (Muda wa Kufanya Starehe). Kivipi sisi tumuache apumzike??? Hapumziki mtu aisee!!!

Sasa mungu kamchukua ili kupisha uchunguzi wa ufisadi alioufanya wakati wa utawala wake, ndio muda wetu wa kuyatoa ya moyoni ili malaika (Wayajue zaidi aliofanya) waongeze kichapo huko alipo.
 
DRCCAG.jpg



TUNASHANGAA TAARIFA ZA CAG, KWA SABABU TULINYIMWA TAARIFA SAHIHI.

Taarifa za mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG) zimeivua nguo serikali ya awamu ya tano iliyokuwa chini ya Dikteta John Magufuli.
Angalau sasa watanzania wanajifunza jambo moja; faida za uhuru wa habari.

Dikteta Magufuli alidhibiti vyombo vya habari kwa kutunga sheria ngumu zilizowanyima wakosoaji wa serikali uhuru wa kuchapisha habari. Ilibidi vyombo vya habari vitoe taarifa nzurinzuri za kumpendeza Dikteta Magufuli.

Shirika la habari la Taifa (TBC) likaongoza ngonjera za kumsifu Dikteta Magufuli.

Mashirika binafsi ya habari yakaitikia kwa beti za kusifu na kumpamba Dikteta Magufuli.

Chombo cha habari kilichochapisha taarifa zisizopendeza kilishughulikiwa.

Tafsiri ya uzalendo ikawa kumsifu Dikteta Magufuli, kuandika habari za kupendeza hata kama ni za uongo na kuficha madudu ya serikali. Huo ndio uzalendo wa nyakati za Dikteta Magufuli.

Waliotaka kuutafuta ukweli, walikiona cha mtema kuni. Walitekwa na kupotezwa. Ukweli ungepatikana, nani angemsifu Dikteta Magufuli kwa nyimbo na mapambio? Propaganda za kusifu zilibamba kwelikweli. Watu wakaaminishwa kwamba eti Magufuli amefanya mambo makubwa ndani ya muda mfupi. Wajinga ambao ni wengi wakaamini kwamba hakuna Rais aliyewahi kufanya makubwa zaidi ya Dikteta Magufuli.


Yote hayo ni kwa sababu wanahabari walitakiwa kuandika hayo. Aliyethubutu kuandika kinyume aliandamwa na vitisho, makaripio na hata kufanyiwa mambo yasiofaa kwa utu.
Lakini sasa Dikteta Magufuli hayupo.

Tumejua; kumbe alibinya uhuru wa habari ili wananchi wapate habari za kumpamba tu na sio zile zinazomchafua hata kama zina ukweli. Kama kungelikuwa na uhuru wa habari, yapo mambo ambayo kama yangesemwa hadharani, yangepigiwa kelele na serikali ingechukua hatua (hata kwa aibu tu) kuyarekebisha. Taarifa za CAG zimeonesha ufisadi wa kihistoria ndani ya ardhi ya Tanzania baada ya Dikteta Magufuli kuondoka. Laiti kama angekuwa hai, pengine tusingepata taarifa hizi za ufisadi.


Hata hivyo, tukubaliane kwamba tatizo kubwa la nchi yetu halikuwa Dikteta Magufuli peke yake, bali ni Watanzania wenyewe. Kwa sehemu kubwa wahusika wa ufisadi ni WATANZANIA. Ni bahati mbaya tu tulikuwa na kiongozi dikteta aliyebana uhuru wa habari na hivyo kuwa sehemu ya Tatizo la nchi yetu. Tulikuwa na kiongozi aliyeamini katika uongo mzuri kuliko ukweli unaouma - tingatinga liloharibu mazao kwa kisingizio cha kusafisha shamba.

Tunahitaji uhuru wa habari ili mambo mengi yawekwe hadharani. Tuyajue, tupige kelele, tusutane, tubishane, tusemane, tuzomeane, turekebishane kabla ya kukaguliwa na kuumbuliwa na CAG.
 
Mwendazake. Why do people continue giving him free airtime? Alipokuwa hai alikuwa ni jogoo pekee linalowika. Na inavyoonekana sasa, bado anaendelea kuwika. Tunashindwa kukubali ametangulia mbele ya haki.
JPM ana bahati kubwa sana. Tupende tukatae
 
Watu wake woote hawajui kusoma na kuandika vizuri. Nikazie kwenye vizuri hapo.

Cheki na huyu sasa anavyoandika😀

Sio apumzike sema ahukumiwe kwa kadiri ya matendo yake.

Pusi😈😈😈😈😈
 
Praise to Lord, kifo cha marehemu dikiteta magufuli happened for a good purpose.
 
Mwendazake. Why do people continue giving him free airtime? Alipokuwa hai alikuwa ni jogoo pekee linalowika. Na inavyoonekana sasa, bado anaendelea kuwika. Tunashindwa kukubali ametangulia mbele ya haki.
JPM ana bahati kubwa sana. Tupende tukatae
Nakazia
 
Magufuli ametusumbua miaka mitano sisi tumevumilia,leo tunamsumbua yeye kwa mwezi tu mnalalamika?
Huyu hayati alikua katili sana tuacheni tumsakame!
 
Kwa wema wenu mtaishi milele?
Mkuu tofautisha JIWE na Sisi ambao wanyonge tunaodunduliza kwa dola moja kwa siku,sisi tunaongoza familia tu huku mtaani.

JIWE alikuwa anaongoza watu milioni 60 ,maamuzi yake yana athari kubwa kwa watu wote hao ,tofautisha maamuzi yetu ngazi ya familia yana effect familia yetu/yako tu.

Maamuzi aliyokuwa anayafanya JIWE yalikuwa yanaumiza waTZ wote,Uchumi umepiga mweleka tunaumia sote,kwahiyo Mungu akaona ngoja ampumzishe ili watu wake wasiendelee kuumia ,ndio maana baada ya kufa umeona kila mtu anafunguka ,umeona kina kigwangala,Prof Assad ,Spika etc ina maana wakati yupo walikuwa hawakubaliani nae sema ndio hivyo hawakuthbutu kutamka wazi maana kifuatacho ITV wanakijua.
 
Back
Top Bottom