Tumuunge mkono rais Magufuli

Tumuunge mkono rais Magufuli

mumagoma

Senior Member
Joined
Jan 15, 2014
Posts
186
Reaction score
95
MIPANGO ya Muda mrefu na MIPANGO ya Muda mfupi

Tunachokiona katika serikali hii ya awamu ya tano chini ya mh Rais John Magufuli ni Kuwa ilani inatekeleza mipango yake kwa kubalance ile ya muda mfupi kidogo na ya muda mrefu kwa sana...

Mipango ya muda mfupi huonesha Matokeo chanya muda mfupi, wananchi na wanasiasa wanapenda sana mipango hii kwani huwafanya wakubalike muda mfupi , lakini uhalisia watalamu wanasema mipango hii huwa inaziba tatizo na sio kutatua

Mipango ya muda mrefu ambayo ni njia muafaka ya kutatua shida na matatizo ktk jamii hufanyika na kutekelezwa kwa muda mrefu na ikisha timia huleta faida kubwa katika jamii

.... Ndege mbili zilizo nunuliwa ni mipango ya muda mrefu, faida ya hili ni ya muda mrefu Katika nchi yetu

... Bomba la mafuta linalotarajiwa kujengwa toka Tanga kwenda uganda ni mipango ya muda mrefu, itatoa ajira muda mrefu kwa watanzania

... Kuhakiki watumishi hewa ni kujenga msingi wa kutorudia kosa la kuwa na watumishi hewa, faida ya hili itakuwa serikali itakiwekea mfumo mzuri wa kuwabaini watumishi wake kiurahisi na itakuwa faida ya muda mrefu

... Reli inayotarajiwa kujengwa, Reli ya kati ya standard gauge itahudumia kusafirisha mizigo Tanzania na nchi zote za ukanda wa africa kati kutokea bandari ya Dar es salama, faida ya hili ikaonekana muda mrefu

... Kutoa vigezo stahiki vya kuwakopesha wanafunzi elimu ya juu lengo lake ni kuhakikisha wale wanaokopeshwa wanarejesha mkopo ndani ya muda baada ya kuhitimu, hili litafafanya board ya mikopo ijiendeshe muda mrefu bila kukwama, faida ya hili ni muda mrefu

Mh Rais amekuwa akitekeleza ilani ya chama kwa kuangalia mbali, faida ya hayo anayosimamia hatutaiona siku hio hiyo hiyo , faida yake tutaiona baadae, Ningependa na mimi niurudie ule usemi wa mh Rais kuwa "ingekuwa vyema Malaika wajitokeze wazime mitandao ya kijamii yote na ili baada ya miaka miwili au mitatu aje awashe tena ili wale wanaodanganywa na mitandao mbalimbali waone utofauti "

Ndani ya mwaka mmoja mengi na ya msingi yamefanyika na Serikali yetu tiifu kwa sisi wanyonge imekuwa ikitekeleza mipango chanya ya muda mfupi na muda mrefu, na huku ikitupilia mbali mipango hasi ya muda mfupi

MFANO wa MIPANGO hasi YA MUDA MFUPI

Mfano wa mipango hasi ya muda mfupi ambayo serikali hii sijaona ikiitumia na sijaona ikiweka kama kipaumbele ni...

... Kugawa fedha bure kwa wananchi wake hata wenye nguvu ya kufanya kazi, binafsi hili siliungi kwa kuwa hutatua shida ya siku moja na baada ya hapo shida huibuka tena na wananchi wanaendelea kutabika

...... Kuruhusu wanafunzi hata wasio na vigezo kusoma vyuo vikuu ili kupata wasomi wengi ndani ya muda mfupi, binafsi hili pia naungana na Serikali kulipinga maana ndio huwa baadae tunapata wasomi wasio na ubora

... Kuruhusu muda wote watu wafanye siasa ili kuwafurahisha wao badala ya kufanya kazi, ukiwaruhusu watu wafanye siasa muda wote utawafurahisha muda huo kwa kuwapa haki ya kukusanyika lakini furaha hiyo itaondoka mapema baada ya njaa kuingia badae maana watu hawakuzalisha, naungana pia na Serikali kupinga siasa za muda wote

... Kuwaruhusu wananchi wajenge mabondeni kwenye mafuriko ilihali unajua wakati wa mvua kutakuwepo na mafuriko, utawafurahisha muda mfupi lakini baadae watapata shida

... Kuruhusu watu wajenge kwenye road reserve ili kuwafurahisha muda huo mfupi ilihali unajua barabara baadae itatanuliwa ni mipango ya muda mfupi

Mipango hasi ya muda mfupi inatatua shida kwa muda mfupi lakini baadae shida inaibuka tena

My take....

tuiache serikali ifanye kazi iliyo tumwa na wananchi tuache kupotosha ukweli​
 
Maelezo mengi lakn lamana hata moja, et mapanga shaa,Ni mpango wa mda mrefu
 
MIPANGO ya Muda mrefu na MIPANGO ya Muda mfupi

Tunachokiona katika serikali hii ya awamu ya tano chini ya mh Rais John Magufuli ni Kuwa ilani inatekeleza mipango yake kwa kubalance ile ya muda mfupi kidogo na ya muda mrefu kwa sana...

Mipango ya muda mfupi huonesha Matokeo chanya muda mfupi, wananchi na wanasiasa wanapenda sana mipango hii kwani huwafanya wakubalike muda mfupi , lakini uhalisia watalamu wanasema mipango hii huwa inaziba tatizo na sio kutatua

Mipango ya muda mrefu ambayo ni njia muafaka ya kutatua shida na matatizo ktk jamii hufanyika na kutekelezwa kwa muda mrefu na ikisha timia huleta faida kubwa katika jamii

.... Ndege mbili zilizo nunuliwa ni mipango ya muda mrefu, faida ya hili ni ya muda mrefu Katika nchi yetu

... Bomba la mafuta linalotarajiwa kujengwa toka Tanga kwenda uganda ni mipango ya muda mrefu, itatoa ajira muda mrefu kwa watanzania

... Kuhakiki watumishi hewa ni kujenga msingi wa kutorudia kosa la kuwa na watumishi hewa, faida ya hili itakuwa serikali itakiwekea mfumo mzuri wa kuwabaini watumishi wake kiurahisi na itakuwa faida ya muda mrefu

... Reli inayotarajiwa kujengwa, Reli ya kati ya standard gauge itahudumia kusafirisha mizigo Tanzania na nchi zote za ukanda wa africa kati kutokea bandari ya Dar es salama, faida ya hili ikaonekana muda mrefu

... Kutoa vigezo stahiki vya kuwakopesha wanafunzi elimu ya juu lengo lake ni kuhakikisha wale wanaokopeshwa wanarejesha mkopo ndani ya muda baada ya kuhitimu, hili litafafanya board ya mikopo ijiendeshe muda mrefu bila kukwama, faida ya hili ni muda mrefu

Mh Rais amekuwa akitekeleza ilani ya chama kwa kuangalia mbali, faida ya hayo anayosimamia hatutaiona siku hio hiyo hiyo , faida yake tutaiona baadae, Ningependa na mimi niurudie ule usemi wa mh Rais kuwa "ingekuwa vyema Malaika wajitokeze wazime mitandao ya kijamii yote na ili baada ya miaka miwili au mitatu aje awashe tena ili wale wanaodanganywa na mitandao mbalimbali waone utofauti "

Ndani ya mwaka mmoja mengi na ya msingi yamefanyika na Serikali yetu tiifu kwa sisi wanyonge imekuwa ikitekeleza mipango chanya ya muda mfupi na muda mrefu, na huku ikitupilia mbali mipango hasi ya muda mfupi

MFANO wa MIPANGO hasi YA MUDA MFUPI

Mfano wa mipango hasi ya muda mfupi ambayo serikali hii sijaona ikiitumia na sijaona ikiweka kama kipaumbele ni...

... Kugawa fedha bure kwa wananchi wake hata wenye nguvu ya kufanya kazi, binafsi hili siliungi kwa kuwa hutatua shida ya siku moja na baada ya hapo shida huibuka tena na wananchi wanaendelea kutabika

...... Kuruhusu wanafunzi hata wasio na vigezo kusoma vyuo vikuu ili kupata wasomi wengi ndani ya muda mfupi, binafsi hili pia naungana na Serikali kulipinga maana ndio huwa baadae tunapata wasomi wasio na ubora

... Kuruhusu muda wote watu wafanye siasa ili kuwafurahisha wao badala ya kufanya kazi, ukiwaruhusu watu wafanye siasa muda wote utawafurahisha muda huo kwa kuwapa haki ya kukusanyika lakini furaha hiyo itaondoka mapema baada ya njaa kuingia badae maana watu hawakuzalisha, naungana pia na Serikali kupinga siasa za muda wote

... Kuwaruhusu wananchi wajenge mabondeni kwenye mafuriko ilihali unajua wakati wa mvua kutakuwepo na mafuriko, utawafurahisha muda mfupi lakini baadae watapata shida

... Kuruhusu watu wajenge kwenye road reserve ili kuwafurahisha muda huo mfupi ilihali unajua barabara baadae itatanuliwa ni mipango ya muda mfupi

Mipango hasi ya muda mfupi inatatua shida kwa muda mfupi lakini baadae shida inaibuka tena

My take....

tuiache serikali ifanye kazi iliyo tumwa na wananchi tuache kupotosha ukweli​
Ninakubaliana na hoja yako.

Mimi ninafurahishwa sana na watu wanaomkosoa bila unafiki au katika mtazamo wa kujenga kwa maslahi ya taifa.

Ninachomuomba Rais Magufuli na ninaamini ameanza kukifanyia kazi ni kuacha kuwajibu jibu hawa wanasiasa ambao wanatafuta uhalali wa hoja zao baada ya kuwajibu.

Awajibu tu pale ambapo hoja yao/zao zinagusa maslahi mapana ya kitaifa.
 
Vizuri mimi na familia yangu yote na majirani zangu tunamuunga mkono na kumuombea
 
tumuunge mikono tena? kwani ya kwake imekatika btw alisema sirikali yake tajiri wacha afanye ajisikiavyo
 
Tumuunge mkono mara ngapi?
Tumefanya hivyo hata kabla hajaingia madarakani lakini mwisho wa siku kutuangusha kabisa.
Push Up tulipiga, Kibwagizo cha hapa Kazi tu tulikiimba sana, kura tulichakachua na mitandaoni tulimpamba kama malaika, tukakesha kumwombea na mwisho wa siku tumeishia kuisoma namba tu.

Asitafute mchawi hapa. Amechemka mwenyewe tena mapema sana.
 
Hata yeye mwenyewe kwa sasa anasema huu mziki wa kuongoza watanzania ni mnene sana hadi kufikia hata kutamani kujiuzuru.

Kama akichukua uamuzi huo, sote tutamuunga mkono sana.
 
Ninakubaliana na hoja yako.

Ninachomuomba Rais Magufuli na ninaamini ameanza kukifanyia kazi ni kuacha kuwajibu jibu hawa wanasiasa ambao wanatafuta uhalali wa hoja zao baada ya kuwajibu.

Awajibu tu pale ambapo hoja yao/zao zinagusa maslahi mapana ya kitaifa.

Nazani ungesema awe anajipanga kuongea maana kila akiongea lazima sintofahamu
 
MIPANGO ya Muda mrefu na MIPANGO ya Muda mfupi

Tunachokiona katika serikali hii ya awamu ya tano chini ya mh Rais John Magufuli ni Kuwa ilani inatekeleza mipango yake kwa kubalance ile ya muda mfupi kidogo na ya muda mrefu kwa sana...

Mipango ya muda mfupi huonesha Matokeo chanya muda mfupi, wananchi na wanasiasa wanapenda sana mipango hii kwani huwafanya wakubalike muda mfupi , lakini uhalisia watalamu wanasema mipango hii huwa inaziba tatizo na sio kutatua

Mipango ya muda mrefu ambayo ni njia muafaka ya kutatua shida na matatizo ktk jamii hufanyika na kutekelezwa kwa muda mrefu na ikisha timia huleta faida kubwa katika jamii

.... Ndege mbili zilizo nunuliwa ni mipango ya muda mrefu, faida ya hili ni ya muda mrefu Katika nchi yetu

... Bomba la mafuta linalotarajiwa kujengwa toka Tanga kwenda uganda ni mipango ya muda mrefu, itatoa ajira muda mrefu kwa watanzania

... Kuhakiki watumishi hewa ni kujenga msingi wa kutorudia kosa la kuwa na watumishi hewa, faida ya hili itakuwa serikali itakiwekea mfumo mzuri wa kuwabaini watumishi wake kiurahisi na itakuwa faida ya muda mrefu

... Reli inayotarajiwa kujengwa, Reli ya kati ya standard gauge itahudumia kusafirisha mizigo Tanzania na nchi zote za ukanda wa africa kati kutokea bandari ya Dar es salama, faida ya hili ikaonekana muda mrefu

... Kutoa vigezo stahiki vya kuwakopesha wanafunzi elimu ya juu lengo lake ni kuhakikisha wale wanaokopeshwa wanarejesha mkopo ndani ya muda baada ya kuhitimu, hili litafafanya board ya mikopo ijiendeshe muda mrefu bila kukwama, faida ya hili ni muda mrefu

Mh Rais amekuwa akitekeleza ilani ya chama kwa kuangalia mbali, faida ya hayo anayosimamia hatutaiona siku hio hiyo hiyo , faida yake tutaiona baadae, Ningependa na mimi niurudie ule usemi wa mh Rais kuwa "ingekuwa vyema Malaika wajitokeze wazime mitandao ya kijamii yote na ili baada ya miaka miwili au mitatu aje awashe tena ili wale wanaodanganywa na mitandao mbalimbali waone utofauti "

Ndani ya mwaka mmoja mengi na ya msingi yamefanyika na Serikali yetu tiifu kwa sisi wanyonge imekuwa ikitekeleza mipango chanya ya muda mfupi na muda mrefu, na huku ikitupilia mbali mipango hasi ya muda mfupi

MFANO wa MIPANGO hasi YA MUDA MFUPI

Mfano wa mipango hasi ya muda mfupi ambayo serikali hii sijaona ikiitumia na sijaona ikiweka kama kipaumbele ni...

... Kugawa fedha bure kwa wananchi wake hata wenye nguvu ya kufanya kazi, binafsi hili siliungi kwa kuwa hutatua shida ya siku moja na baada ya hapo shida huibuka tena na wananchi wanaendelea kutabika

...... Kuruhusu wanafunzi hata wasio na vigezo kusoma vyuo vikuu ili kupata wasomi wengi ndani ya muda mfupi, binafsi hili pia naungana na Serikali kulipinga maana ndio huwa baadae tunapata wasomi wasio na ubora

... Kuruhusu muda wote watu wafanye siasa ili kuwafurahisha wao badala ya kufanya kazi, ukiwaruhusu watu wafanye siasa muda wote utawafurahisha muda huo kwa kuwapa haki ya kukusanyika lakini furaha hiyo itaondoka mapema baada ya njaa kuingia badae maana watu hawakuzalisha, naungana pia na Serikali kupinga siasa za muda wote

... Kuwaruhusu wananchi wajenge mabondeni kwenye mafuriko ilihali unajua wakati wa mvua kutakuwepo na mafuriko, utawafurahisha muda mfupi lakini baadae watapata shida

... Kuruhusu watu wajenge kwenye road reserve ili kuwafurahisha muda huo mfupi ilihali unajua barabara baadae itatanuliwa ni mipango ya muda mfupi

Mipango hasi ya muda mfupi inatatua shida kwa muda mfupi lakini baadae shida inaibuka tena

My take....

tuiache serikali ifanye kazi iliyo tumwa na wananchi tuache kupotosha ukweli​
Mkuu komaa utapewa ukuu wa wilaya
 
Nazani ungesema awe anajipanga kuongea maana kila akiongea lazima sintofahamu
Sintofahamu ni dhana tu kifikra.

Kuna wengine mpaka leo wanadhani kuna sintofahamu kwenye vitabu vya Mwenyezi Mungu. Kwa hiyo unataka kuniambia Mwenyezi Mungu hakujipanga wakati anatuletea maandiko yake?
 
Naunga mkono hoja, tumsupport kwa asilimia 100% ila pia tumkosoe anapoboronga.

Pasco
 
Ninakubaliana na hoja yako.

Mimi ninafurahishwa sana na watu wanaomkosoa bila unafiki au katika mtazamo wa kujenga kwa maslahi ya taifa.

Ninachomuomba Rais Magufuli na ninaamini ameanza kukifanyia kazi ni kuacha kuwajibu jibu hawa wanasiasa ambao wanatafuta uhalali wa hoja zao baada ya kuwajibu.

Awajibu tu pale ambapo hoja yao/zao zinagusa maslahi mapana ya kitaifa.
Nadhani wanaoomba Rais aungwe mkono, kwa upande mwingine hawamuungi mkono

Kumuunga mkono Rais si kukubaliana na kila analofanya. Na wala kukataa anayofanya hakuzuii kuungwa mkono

Wanaotaka Rais aungwe mkono, ni wale wasiomtakia mema kwa kutomwambia ukweli

Anayevuruga kuungwa mkono si wapinzani, ni self destructions within the government a.k.a autolysis

Wananchi wanaona yanayofanyika na wanajua tofauti ya jana na leo au juzi na leo.

Wanovuruga message ni wenyewe, ni hawa wanaozua mambo yanayo derail message iliyokusudiwa. Tunajua ofisi ya serikali za mitaa ipo chini ya ofisi ya Rais.

Wizara hiyo iliwekwa chini ya Rais ili iwe rahisi kudhibiti mwenendo mzima wa pesa na maendeleo katika grassroots level. Hilo ndilo lengo la awali

Uchaguzi wa Meya wa Dar ulisusua na kuitia wizara chini ya ofisi ya Rais aibu!

Tunajua ilikuwa ni aibu kwasababu mgogoro ule uliisha kisiasa. Ilifanywa makusudi tu

Leo kuna mgogoro mwingine wa Kinondoni ambao ukiutizama hauna maana.

Huu nao unaitia aibu kwasababu mambo yanayofanyika yanasikitisha na hayana maana

Hawa wanaofanya uchafu wanaachiwa, pengine kuna baraka

Badala ya kujadili mambo ya muda mfupi na mrefu, message yote inakuwa na wingu la uchaguzi wa kinondoni

Hapa mnaomba aungwe mkono kwa dua , maombi au kitu gani?

Kwanini msimwambie mambo kama uchaguzi wa Meya ni self destructions
 
Maombi yangu, kumuunga mkono na kumtia moyo mh Rais aendeleze haya ayatendayo maana kwa hakika yana nia njema kwa taifa hili.

Na washawasha!
 
Back
Top Bottom