Salamu wana JF. Kuna mtu mmoja ameniomba ushauri lakini nimeona ni vema kushirikisha wanajukwaa ili tuweze kumpatia jibu lililo sahihi. Suala lenyewe lipo hivi: Nina jirani yangu ambaye tunaelewana sana, hivi karibuni aliniambia hamwelewi mchumba wake wa kike anayetarajia kufunga naye ndoa hivi karibuni maana (mwanamke) hapendi jamaa ashike simu yake. Kila siku wanamke anatumia muda mwingi sana kuongea na watu mbalimbali ambao jamaa hawatambui, simu hiyo ipo bize mchana kutwa na hata usiku. Siku moja mwanake alipokuwa anaoga simu yake iliita zaidi ya mara 3, jamaa akaamua kuipokea, simu ile ilipigwwa na mwanamme ambaye alitaka kuongea na mwenye simu (mwanamke), jamaa akamwambia mwenye simu ametoka kidogo, yule jamaa aliyepiga simu akakata simu. Mwanamke aliporudi ndani akaelezwa kuhusu simu iliyopigwa. Mwanamke alikasirika sana kwamba kwa nini jamaa (mchumba wake) ameipokea ile simu, ugomvi ilikuwa mkubwa. Tukio lingine lilitokea siku moja wachumba hao walipokuwa wapo faragha meseji iliingia kwenye simu ya mwanamke, jamaa akataka kumjua aliyetuma meseji lakini mwanamke akamzuia na pia akafuta hiyo meseji, pakatokea tafrani ya nguo kuchanika kwa wapenzi hao. Kutokana na visa hivyo jamaa anaomba ushauri je huyo mchumba wake ana mapenzi ya kweli kwake? Kwa nini hapendi simu yake ichunguzwe na huyo mchumba wake? Jamaa anaomba ushauri afanyeje?
"ndugu mimi nina miaka minne na mke wangu, anaweza akaniachia hata simu yake siku nzima na mimi nampa uhuru wa kushika simu yangu."
ndugu mimi nina miaka minne na mke wangu, anaweza akaniachia hata simu yake siku nzima na mimi nampa uhuru wa kushika simu yangu. Mwambie jamaa yako huyoi msichana hamfai.
Ebu jamani wana JF please wekeni vitu vya msingi kwenye jukwaa sio huu upumbavu km huu wa huyu jamaa yetu na hawara yake! Yaani hata kunya nako ufundishwe wakati choo unakiona..?!!!
Please do not post nonsense topics.
Je na zile laini mbili za mitandao mingine ambazo huwa zipo kwenye kale kapochi kadogo nazo huwa anakupa, huwa anaziweka ndaani ya pochi anafunga na zipu
Salamu wana JF. Kuna mtu mmoja ameniomba ushauri lakini nimeona ni vema kushirikisha wanajukwaa ili tuweze kumpatia jibu lililo sahihi.
Suala lenyewe lipo hivi: Nina jirani yangu ambaye tunaelewana sana, hivi karibuni aliniambia hamwelewi mchumba wake wa kike anayetarajia kufunga naye ndoa hivi karibuni maana (mwanamke) hapendi jamaa ashike simu yake.
Kila siku wanamke anatumia muda mwingi sana kuongea na watu mbalimbali ambao jamaa hawatambui, simu hiyo ipo bize mchana kutwa na hata usiku.
Siku moja mwanake alipokuwa anaoga simu yake iliita zaidi ya mara 3, jamaa akaamua kuipokea, simu ile ilipigwwa na mwanamme ambaye alitaka kuongea na mwenye simu (mwanamke), jamaa akamwambia mwenye simu ametoka kidogo, yule jamaa aliyepiga simu akakata simu.
Mwanamke aliporudi ndani akaelezwa kuhusu simu iliyopigwa. Mwanamke alikasirika sana kwamba kwa nini jamaa (mchumba wake) ameipokea ile simu, ugomvi ilikuwa mkubwa.
Tukio lingine lilitokea siku moja wachumba hao walipokuwa wapo faragha meseji iliingia kwenye simu ya mwanamke, jamaa akataka kumjua aliyetuma meseji lakini mwanamke akamzuia na pia akafuta hiyo meseji, pakatokea tafrani ya nguo kuchanika kwa wapenzi hao.
Kutokana na visa hivyo jamaa anaomba ushauri je huyo mchumba wake ana mapenzi ya kweli kwake? Kwa nini hapendi simu yake ichunguzwe na huyo mchumba wake?
Jamaa anaomba ushauri afanyeje?