Tumsaidie mtu huyu, amechanganyikiwa

Tumsaidie mtu huyu, amechanganyikiwa

vamda

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2012
Posts
919
Reaction score
598
Salamu wana JF. Kuna mtu mmoja ameniomba ushauri lakini nimeona ni vema kushirikisha wanajukwaa ili tuweze kumpatia jibu lililo sahihi.

Suala lenyewe lipo hivi: Nina jirani yangu ambaye tunaelewana sana, hivi karibuni aliniambia hamwelewi mchumba wake wa kike anayetarajia kufunga naye ndoa hivi karibuni maana (mwanamke) hapendi jamaa ashike simu yake.

Kila siku wanamke anatumia muda mwingi sana kuongea na watu mbalimbali ambao jamaa hawatambui, simu hiyo ipo bize mchana kutwa na hata usiku.

Siku moja mwanake alipokuwa anaoga simu yake iliita zaidi ya mara 3, jamaa akaamua kuipokea, simu ile ilipigwwa na mwanamme ambaye alitaka kuongea na mwenye simu (mwanamke), jamaa akamwambia mwenye simu ametoka kidogo, yule jamaa aliyepiga simu akakata simu.

Mwanamke aliporudi ndani akaelezwa kuhusu simu iliyopigwa. Mwanamke alikasirika sana kwamba kwa nini jamaa (mchumba wake) ameipokea ile simu, ugomvi ilikuwa mkubwa.

Tukio lingine lilitokea siku moja wachumba hao walipokuwa wapo faragha meseji iliingia kwenye simu ya mwanamke, jamaa akataka kumjua aliyetuma meseji lakini mwanamke akamzuia na pia akafuta hiyo meseji, pakatokea tafrani ya nguo kuchanika kwa wapenzi hao.

Kutokana na visa hivyo jamaa anaomba ushauri je huyo mchumba wake ana mapenzi ya kweli kwake? Kwa nini hapendi simu yake ichunguzwe na huyo mchumba wake?

Jamaa anaomba ushauri afanyeje?
 
Wanawake wa namna hiyo mara nyingi huwa ni Machangu!!! Huyo bwana achukue tahadhari mapema.
 
Hajatulia tulia huyo dem mapeepe(in Juma Nature's voice)
amshtue amwambie kama hawi muwazi na mambo yake waachane af umsikie!!anaweza hata asishtuke cos it seems ana mabranch zaidi ya nmb!!!LOL
kama hayupo comfortable,asiharakishe ndoa. May be they werent meant to be!
 
Namlaumu sana huyo jamaa. kabla hujatangaza nia ya kuoa hakikisha umemchunguza msichana wako vya kutosha. Kinachooneka huyo msichana sio muaminifu.

SOLUTION- Kwa maelezo machache uliyotoa namshauri kuachana na huyo msichana
 
ndugu mimi nina miaka minne na mke wangu, anaweza akaniachia hata simu yake siku nzima na mimi nampa uhuru wa kushika simu yangu. Mwambie jamaa yako huyoi msichana hamfai.
 
Jamaa anatatizo la maamuzi.kama nanini wa pale magogon
 
Jamaa anatatizo la maamuzi.kama nanini wa pale magogon

Sasa unataka mtu amwache mchumba kwa sababu ya simu tu. mwambie atangaze ndoa na marufuku kugusa simu ya mrembo yoyote kwani nao wana privacy zao. yeye anaoa simu au mke. si anunue hata tigo na yeye
 
Kama hana amani ya moyo si lazima kulazimisha ndoa...
 
Jamaa yako hata kama kusoma hajui,je macho hana,picha haoni?mwambie aachane na huyo binti,hakuna njia nyngne.
 
Jamaa yako yuko sahihi kuwa na mashaka, Kifupi ukiona manyoya ujue ndo vile, ila suala la maamuzi ni lake.
 
Kwenye ndoa huingii na madukuduku,na anazoziona sasa ni ishara ya kwamba mda wa ndoa bado na huyo mrembo.
 
hayo yote anayoyaona ndio tunayaita MANYOYA. so hapo ni kujiongeza ukishaona manyoya
 
Ebu jamani wana JF please wekeni vitu vya msingi kwenye jukwaa sio huu upumbavu km huu wa huyu jamaa yetu na hawara yake! Yaani hata kunya nako ufundishwe wakati choo unakiona..?!!!
Please do not post nonsense topics.
 
alafu uyo jamaa inaonekana amewekwa kwenye kiganja!
 
ndugu mimi nina miaka minne na mke wangu, anaweza akaniachia hata simu yake siku nzima na mimi nampa uhuru wa kushika simu yangu. Mwambie jamaa yako huyoi msichana hamfai.


Je na zile laini mbili za mitandao mingine ambazo huwa zipo kwenye kale kapochi kadogo nazo huwa anakupa, huwa anaziweka ndaani ya pochi anafunga na zipu
 
Ebu jamani wana JF please wekeni vitu vya msingi kwenye jukwaa sio huu upumbavu km huu wa huyu jamaa yetu na hawara yake! Yaani hata kunya nako ufundishwe wakati choo unakiona..?!!!
Please do not post nonsense topics.

Maisha ya mtu mazuri yanatokana na maelewano mazuri ndani ya nyumba, mtu wako wa karibu wa kukuliwaza unapopatwa na tatizo ni mke au mme ndani ya nyumba, mimi nadhani wewe ndio --------, ungeona hili lililoletwa ni la kipumbavu ungeliacha na kusubiri yale unayoona ya maana ujibu. ipo siku utakuja sema tusijadili ya kwetu haapa Tanzania badala yake tujadili ya Marekani eti kwa kuwa wewe unamwita Obama ni rais wa dunia
 
Back
Top Bottom