Tumfanyaje huyu dogo?

daah haki ya Mungu kuna watu wengine unaweza ukawala nyama hivihivi yan sikufichi mkuu!! Yani wadau wanavyo fight na hili life bila ramani, alaf yeye anatafuniwa hvyo then hamezi anatema na kumwagia mchanga!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! sikufichi MNYAMAKAZI unaweza ukamtafuna mtu hivix2 yani.
 
Muundie mishe akae sero kama miezi kadhaa atatoka na akili kumkichwa

umeniwahi mkuu, hiyo ni solution mojawapo. Tatizo alilonalo ni kwamba hajui upande wa pili wa maisha uko vipi na kama mnampenda kosa mtakalofanya ni kumuacha afunzwe na ulimwengu, ulimwengu hauchagui jinsi gani nzur ya kumfunza mtu asipoishia kufa kwa wizi atabaki kilema au ataishia kua teja. Jaribuni kutafuta njia za kumuonesh upande wa pili wa maisha ulivyo nina imani atajifunz na kurekebika na ikishindikana basi acheni mapenzi ya Mungu juu yake yatimie.
 
mwacheni huyo anawachezea akili tu dunia itamfunza tena hakuna kupewa msaada wowote aiii
 

Huyo ameshavuka kipengere cha kupelekwa kwa mwana saikolojia, sehem inayomfaa kwa sasa ni jela tu. Akitoka hapo hajabadilika basi tena.
 



mtu anakimbia mpa mnampeleka jw
shenzi akaungane na mdogo wangu wakafe kwa shaba. Nina hasira na watu hao jamani!
 




siku ya kumpiga kiberiti mnijulishe nimlete dogo wangu waungane kwani ni zaidi ya uchovu ila nahisi ni malezi mabovu
 
Ana uhakika wa kula bure na kunya bure kulala bure

Kwanza kila mmoja ampige biti kwenda kwake

Aende akatafute maisha

Mshagawana mirathi? Kila mmoja achujur sehemu yake

Halafu mumuache dunia imnyooshe
 
Tumewahi kukubaliana namna hii mkuu but kuna sister na anti yetu mmoja kila akitua selo wanamtoa.

Sasa hawa muwaite pamoja na dogo

Muwakabithi na waambieni hamhusiki kwa lolote kiufupi wamchukue

Akishawaibia akili itawakaa sawa
 
Mpelekeni kwa hao wanaomtoa akaishi nao na huko kwenu mumpige marufuku kuonekana
 

kwa experience niliyoona kwa watoto wa aina hiyo jela huwa haiwasaidii sana, nimeshaona vijana kama watatu hivi wa aina hiyo mmoja alikuja kubadilika mwenyewe tu manake njia zote za kumbadilisha zilishindikana ila kwa neema ya Mungu akaja kubadilika na sasahivi ni mtumishi wa Mungu mzuri tu, ila hao wawili jamani huwa nasikia huruma sana kwa wazazi wao mmoja hajulikani alipo kwasasa sijui alishakufa au vipi manake wazazi wali give up wala hawahesabu kama wana mtoto huyo mwingine jela anaingia na kutoka yani mtaani hamalizi hata mwaka anarudishwa tena lakini wapi na ameshakuwa mtu mzima sasa
 
[Sasa hawa muwaite pamoja na dogo

Muwakabithi na waambieni hamhusiki kwa lolote kiufupi wamchukue

Akishawaibia akiki itawakaa sawa]


(Mpelekeni kwa hao wanaomtoa akaishi nao na huko kwenu mumpige marufuku kuonekana)

Nakubalina na hawa watu
 
Solution yenye uhakika ya kumsaidi haipo ila atakuja kubadilika mwenyewe kadri umri unavyokwenda au asije kubadilika kabisa
 

Mpelekeni segerea. Akikaa miaka 5, atashika adabu yake.

 
Pelekeni Segerea mwaka mmoja atarudi na adabu hii si kwa kumkomoa bali kumfunza dunia.
 
akili yk haifany kaz kuhuxu lfe mwache kwanz akomae kitaa kwanza kama 2 yrz mcmpe matumiz yoyote atafute mwenyew akiiba lubango ipo bana kwa nn msumbue kichwa wakat kuna wa2 wanaxotea hzo chance hawazipat huku ye anazichezea
 
Mpeleke polisi akapate mafunzo kwa miezi mitatu, halafu mtoe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…