Tumewaona, tumewasikia, mpo ambao hamkumaanisha!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,478
39,997
Tatizo la Viapo: Mojawapo ya mambo ambayo yamenitibua sana na yanaendelea kunitibua hili la watu kula viapo kwa ajili ya kupata kazi tu lakini si kwa ajili ya kuvisimamia! Wote tumewasikia wakila kiapo tena mbele ya hadhara na wanasema kabisa kwa majina yao na mbele ya Mungu wao tena wakiwa na macho meupe kabisa, sauti za upole na zenye kusikika (ili walioko nyumbani warekodi vizuri) kuwa wanaapa "kuilinda, kuihifadhi na kuitetea" Katiba za vyama vyao.

Samahani wanaapa kutetea misimamu ya vitabu vyao vya dini walivyoshikilia; au marafiki na ndugu zao! Hapana, wanaapa kuilinda, kuitetea na kuhifadhi Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Tumewasikia na tena siyo kwa jumla (maana wengine wangeweza kumung'unya maneno) bali mmoja mmoja tena wakiitwa mbele. Tumewasikia.

Tatizo wanajua uzito wa kiapo hicho? Na je wanamaanisha? Fikiria kwa mfano, watu wanaapa kuhusu hiyo hiyo Katiba halafu wanaanza hapo hapo kuipuuzia! Hawakuapa kuvikubali na kuvilinda vipengele vya Katiba wanavyovipenda; au vile ambavyo vimewafanya wawe wabunge na nafasi zao; wameapa kulinda Katiba yote!

Nina uhakika wa kutosha tu (kwani historia ni mwalimu mzuri) watu hawa hawa ambao tumewaona wakiapa kuilinda, kuitetea na kuihifadhi Katiba Hii hii watakuwa wa kwanza kujaribu kuivunja kama walivyofanya katika Bunge lililopita ambapo walijaribu kuifuta bila kuwa na mamlaka kufanya hivyo (kitu ambacho binafsi naamini ilikuwa ni uhalifu mkubwa - high crimes). Unaweza vipi kutaka kufuta Katiba ambayo uliapa kuihifadhi na bado ukabakia na uhalali wa kuwa huko Bungeni?

Ugomvi wetu mkubwa katika miaka hii mitano ijayo ya Bunge hili la 11 ni jinsi gani itabidi tuwakatalie na kuwakumbusha ndugu zetu hawa juu ya kiapo chao hiki; kwamba kina matokeo. Na kama wanaona hawakubaliani sana na hii Katiba - ni lazima wajiuzulu! Pamoja na ubovu wake wote leo tumewaona wameapa kuitetea, kuihifadhi na kuilinda.

Sasa wasipoitetea, kuihifadhi au kuilinda nani mwingine afanye hivyo? Sisi wengine tunaweza kusema vyovyote juu ya Katiba hii hatufungwi na viapo hivi; wao wenzetu hawawezi. Wamejifunga.

Isipokuwa kama walikuwa wanatupigisha porojo tu!

MMM
 
Katiba hiyo inatoa mwongozo gani pale inapobidi kuifanyia mabadiliko au kuunda upya? Sioni tatizo mtu kula kiapo ili apate fursa pana zaidi ya kikatiba kushinikiza upatikanaji wa katiba mpya.
 
Nimeshangaa Sana Kitu Alichoapia Kukulinda Na Kukitetea Leo Hii Hakilindi Wala Kukitetea Tena Bali Asema Ni Kibovu Kimepitwa Na Wakati,inastaajabisha Kwakweli Na Ni Udhihirisho Hawamaanishi Viapo Vyao Aisee.
 
Kutaka Mabadiliko ya katiba siyo kuivunja katiba, kuhujumu uchumi, ufisadi na kubaka demokrasia ndiyo uvunjifu wa Katiba.


Sasa tuone watakaoilinda au kuivunja ni wepi!?
 
Katiba hiyo inatoa mwongozo gani pale inapobidi kuifanyia mabadiliko au kuunda upya? Sioni tatizo mtu kula kiapo ili apate fursa pana zaidi ya kikatiba kushinikiza upatikanaji wa katiba mpya.

Mtazamo,

Tatizo linakuja pale ambapo umeapa kuillinda na kuihifadhi katiba ambayo wewe umepata madaraka au mamlaka ya kiutawala au kiutendaji chini yake.
Ni ngumu na kwa kweli ni kosa kuba la kikatiba lenye nguvu sawa na uhaini katika uzito wa jinai, kuidhaurau, au kuibeza hadharani katiba hiyo hiyo.

Kwa watu hawa walioapa chini ya katiba, wanaweza tu kuikosoa katika maeneo machache na kupendekeza maboresho na sio kuifuta yote au kusema katiba husika haina maana, imekosa mwelekeo, imepitwa na wakati n.k.

Na kwa sababu hii kuna mantiki kubwa pale ilipokuwa inatakiwa wabunge/wajumbe wa bunge maalum la katiba wasiwe wabunge wa kawaida kwani hao wanabanwa na viapo vyao. Lakini kwa uchu wa posho iliyodhaniwa kuwa ni laki 7 kwa siku wabunge wakaikinbilia kwa kishindo.

Ni wakati sasa wabunge wetu na viongozi wa nchi wakahwshimu viapo vyao. Wakaiheshimu katiba na kuilinda na kuihifadhi inavopaswa na ilibidi kufanyiwa marekebisho basi yafanyike katika mfumo ule tu, na kwa kiwango kile tu ambacho katiba imeruhusu.
Huo ni utawala wa sheria na "supremacy of the constitution".
 
Sheria za bunge zinawataka wabunge wataeule wasajiliwe then wale kiapo kama ishara ya kuapishwa kwao kuwa wabunge. Sasa, watateteaje upatikanaji wa katiba mpya bila kuapishwa? Je! Umeona tu la kuapa? Mbona hukuwashauri wasishiriki uchaguzi kabisa kwa kutumia katiba hii mbovu? Bali ulikuwa mstari wa mbele kumnadi jamaa yako Slaa hadi alipopigwa chini ndo ukaleta unafiki? Kwa hiyo ulitaka wasiape ili tena, tukarudie chaguzi za ubunge?

Zile post zako za uchaguzi bado zimekulewesha, ndio maana unaandika mada kama mtoto wa chekechea. Poor argument!
 
Kwa hiyo unataka kutuaminisha tuendelee kutumia katiba ya zamani ili iweje je hatuna ruhusa ya kuibadilisha au unaona no sahihi kuendelea na 1977
 
Mimi ninaichukulia katiba kama nyumba, kuilinda nyumba ni kutoibomoa nyumba kama nyumba ila kufanya marekebisho ya ndani si kuibomoa nyumba. Tukija upande wa wabunge ili uwe mbunge ni lazima ule kiapo sasa utakulaje kiapo cha kuilinda katiba ambayo haipo? lazima kuwepo na katiba ule kiapo ili uwe na nguvu ya kuilinda na hukatazwi kuiboresha ili kukidhi mahitaji ya wakati huo
 
Back
Top Bottom