Tumefikaje hapa?

Tumefikaje hapa?

GoPPiii.

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2014
Posts
1,792
Reaction score
3,079
Kila mtu asali sana na kuiombea hii nchi kwa namna anayojua yeye inafaa ilimradi lile jambo la bandari lisitokee.

Lakini tumefikaje huku? Tumefikaje kuwa na mjadala wa namna hii!?

Nina nadharia mbili tatu kwa nini tuna jadili jambo la hovyo lenye hasara kwa taifa, mpaka mitaa inatikisika hivi.

1/ Deni la taifa sasa halilipiki. Kinachotokea ni namna nyingine ya kulipa hela za watu.

2/ Ahadi ya kuchangia bajeti ya nchi kwa kiwango ambacho serikali imeona inapunguza mzigo kwake. Mfano; Mishahara ya wafanyakazi ambayo huchukua kiasi kikubwa cha mapato ya nchi itatoka kwa hawa watu hivyo serikali haitawaza mishahara tena ya wafanyakazi.

3/ Kuna watu wameshalipwa pesa ndefu sana, kuhakikisha hili jambo linafanyika. Pesa ambayo inahitaji roho ngumu kuikataa. Hii ni wadubai wametumia roho zetu za ufisadi kuhakikisha dili kama hili linafanyika.


Tumefikaje hapa?

Kama kuna mtu anajua faida ya hili jambo tafadhari nieleweshe maana mpaka sasa sielewi zaidi ya kuona hasara tu.
 
Kuna Wajinga wachache wanaosapoti ubinafsishwaji wa bandari, but hawajui kuwa Kuna effect kubwa Sana itawapata wafanyabiashara wanaotumia bandari ku export na ku import mizigo yao,

Bandari ikibinafsishwa hakutokuwa na misamaha ya Kodi Kama tulivozoea, Ndugu zetu wa karikaoo na wafanyabiashara wote waliozoea kukwepa Kodi lazima wakione chamoyo, pia Kuna uwezekano Kodi za kutoa mizigo badarini zikaongezeka Mara dufu

Sio hivyo tu pia Wafanyakazi wa bandarini wako hatarini Sana kupoteza ajira zao....
 
Kuna Wajinga wachache wanaosapoti ubinafsishwaji wa bandari, but hawajui kuwa Kuna effect kubwa Sana itawapata wafanyabiashara wanaotumia bandari ku export na ku import mizigo yao,

Bandari ikibinafsishwa hakutokuwa na misamaha ya Kodi Kama tulivozoea, Ndugu zetu wa karikaoo na wafanyabiashara wote waliozoea kukwepa Kodi lazima wakione chamoyo, pia Kuna uwezekano Kodi za kutoa mizigo badarini zikaongezeka Mara dufu

Sio hivyo tu pia Wafanyakazi wa bandarini wako hatarini Sana kupoteza ajira zao....
Sasa faida ya hili jambo ni nini!??
 
Tuna watawala waliojaa kiburi, tamaa na ulafi wa kiwango ambacho hakijawahi kuonekana, kiasi cha kuwafanya watumwa wa pesa na kuwatia ukichaa na upofu, kiasi cha kupoteza uwezo wa kufikiri maamuzi wanayoyafanya leo.
 
Serikalii pamoja na viongozi wachache watafaidika,

Ila wafanyabiashara hasa wanaotumia bandari kuimport na ku export bidhaa watakuwa affected sana
Na mwisho wa siku anayekoma zaidi kuliko wote ni mlaji wa mwisho wa hizo bidhaa zitakazoingizwa nchini kupitia bandari hiyo. Kodi zote atakazopigwa mfanyabiashara zitafidiwa kwenye bei ya bidhaa husika!
 
Kuna Wajinga wachache wanaosapoti ubinafsishwaji wa bandari, but hawajui kuwa Kuna effect kubwa Sana itawapata wafanyabiashara wanaotumia bandari ku export na ku import mizigo yao,

Bandari ikibinafsishwa hakutokuwa na misamaha ya Kodi Kama tulivozoea, Ndugu zetu wa karikaoo na wafanyabiashara wote waliozoea kukwepa Kodi lazima wakione chamoyo, pia Kuna uwezekano Kodi za kutoa mizigo badarini zikaongezeka Mara dufu

Sio hivyo tu pia Wafanyakazi wa bandarini wako hatarini Sana kupoteza ajira zao....
Hasa hasa hapo kwenye haya ya mwisho hapo...
 
Kuna Wajinga wachache wanaosapoti ubinafsishwaji wa bandari, but hawajui kuwa Kuna effect kubwa Sana itawapata wafanyabiashara wanaotumia bandari ku export na ku import mizigo yao,

Bandari ikibinafsishwa hakutokuwa na misamaha ya Kodi Kama tulivozoea, Ndugu zetu wa karikaoo na wafanyabiashara wote waliozoea kukwepa Kodi lazima wakione chamoyo, pia Kuna uwezekano Kodi za kutoa mizigo badarini zikaongezeka Mara dufu

Sio hivyo tu pia Wafanyakazi wa bandarini wako hatarini Sana kupoteza ajira zao....
Kama mnapinga sababu ya hizo point basi nibupuuzi wabinafsishe haraka sana.

Mnapinga kelele kumbe mmezoea vya bure na loopholes..!
 
Tuna watawala waliojaa kiburi, tamaa na ulafi wa kiwango ambacho hakijawahi kuonekana, kiasi cha kuwafanya watumwa wa pesa na kuwatia ukichaa na upofu, kiasi cha kupoteza uwezo wa kufikiri maamuzi wanayoyafanya leo.
Kila nikiwaza inakuwaje hivi sipati majibu yaan.
 
Na mwisho wa siku anayekoma zaidi kuliko wote ni mlaji wa mwisho wa hizo bidhaa zitakazoingizwa nchini kupitia bandari hiyo. Kodi zote atakazopigwa mfanyabiashara zitafidiwa kwenye bei ya bidhaa husika!
Ndio mkuu, ma jeans ya Vunjabei, tutauziwa elfu 90
 
Walete TRA waarabu.. ATCL waje waarabu...TRC waje waarabu maana tumeshindwa kujiongozaaa.
 
Mama atakuwa anawaamini sana wasaidizi wake.Watakachomfanya atashangaa.She should never trust waswahili hawa...hawana uzalendo, ubinadamu na roho mbaya..hawajali kabisa...
Si uaona hata mikeke ya nafasi nyeti..wanaweka majina ya watoto, ndugu..yaani ni kama kuna familia fulani zinazungukwa tu...na hii ni sababu anawaamini sana watu...
Mama akiendelea kukata mbuga na kupiga hafla..nyuma atakuta watu waishamaliza mboga tayari
 
Yaani serikali kutumia busara na uzalendo tutajikuta tunaleta watu wa nje na kubinafisha vitu vingi sana..
Hivi hamna watu wanaoweza kutengeneza kampuni kama hizo, hela ikabaki hapahapa...?
Kama serikali inaangalia future ya waswahili...na kama hamna kampuni zenye uwezo..
1.Itengeneze kampuni yenye ubia na serikali na watu binafsi (PPPP)
2 Serikali 51% Kampuni ya washahili 49%
3.Serikali iwawezeshe kiutaalamu, vifaa etc...wakatane kwenye malipo huko.
4.Iundwe kamati ya kuijengea uwezo.
5.Wachukue watu wenye uwezo nje wawaajiri kwa miaka kadhaa kwenye transistion..
Hapohapo TPA kuna vijana kibao wanauwezo..
6.N.k
 
Back
Top Bottom