Tumechanganywa kwenye msamaha wa IMF

Tumechanganywa kwenye msamaha wa IMF

Joined
Jun 10, 2020
Posts
11
Reaction score
15
Hivi majuzi International Monetary Funds (IMF) imetangaza msamaha kwa Tanzania kulipa marejesho yake kwa muda wa mezi sita. Kiasi ni shilling bilioni 30 ikiwa ni jitihada za kutumia mapato hayo kwa ajili ya kupambana na corona ambayo serikali inadai imemalizika.

Lakini badala ya kusema kwamba ulipaji wa deni hili umesogezwa mbele, spin doctors wanajaribu kutuaminisha kwamba tumesamehewa hiyo fedha. Nimeona mpaka magezeti ya kimkakati yakiripoti hivyo.

Ikumbukwe kwamba serikali iliomba mkopo kwa ajili ya Covid-19 lakini wakanyimwa kutokana na kutokukamilika kwa maombi. Mwezi uliofuata ndio wakaja na monetary policy instrument ya kuungaunga.

Cha kushangaza, serikali yenyewe inaanza kutopisha kwamba huu ni msamaha na hakuna nchi nyingine iliyosamehewa huu ni uongo uliotukuka.

MATAGA HAMNA HELA. KUJIMWAMBAFAI KWINGI BUT YOU ARE BROKE
 
Ungeeleza kwanini wamesogeza mbele na je tunastahili kusogezewa mbele?
 
Hivi Hawa preise team wanavyokomaa kusifia ikitokea wameombwa jicho watachomoa kweli?.
 
Back
Top Bottom