Mzalendo2015
JF-Expert Member
- Aug 14, 2012
- 7,195
- 9,812
Kwa hali tulipofikia na tunakoelekea kuhusu mambo ya Uchaguzi chini ya hii NEC isiyo Huru amani ya nchi inaenda kutoweka!!!
Haihitaji mtu uwe na elimu ya sayansi ya kurusha Roketi ili kujua kinachofanywa na Tume ya Uchaguzi Tanzania NEC ili kuhakikisha wanakibeba Chama Tawala cha CCM. Kwamba sasa NEC wamedhamiria kuibeba CCM bila hata aibu baada ya tamko la Mwenyekiti wa CCM(T) na Rais wa JMT Bwana John Joseph Pombe Magufuli ya kwamba CCM itatawala milele.
Tunapoelekea kwenye Chaguzi ndogo za Ubunge Jimbo la Buyungu na Udiwani katika Kata 72 inaonekana kuwa NEC wana mpango kabambe wa kuhakikisha Upinzani hawapati Jimbo la Ubunge wa Kata hata moja. Vituko vinavyojitokeza kwenye maeneo yenye wagombea wa Udiwani kwa Upinzani inasikitisha kama siyo kutishia Amani ya nchi. Kwamba sasa kuna wagombea wa Udiwani toka Upinzani wameambiwa siyo Raia wa Tanzania.....Kuna maeneo Wagombea wanasakwa na Polisi kwa kesi za Mauaji. na kuna maeneo Wagombea wanalazimishwa kujiuzulu au kujaza Fomu kimakosa kwa maksudi ili wawe DISQUALIFIED na Wasimamizi wa Uchaguzi ambao ni Wakurugenzi wa Halmashauri na Miji.
Chondechonde kwa Rais JPM aingilie kati na aepushe huu uhuni unaofanywa na wateule wake toka NEC...!!Ikibidi hata ajitokeze hadharani afute kauli yake ya CCM ITATAWALA MILELE MAANA KAULI HIYO INAONEAKANA KULETA UCHOCHEZI na ikizingatiwa tunaelekea kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka kesho 2019 na Uchaguzi Mkuu 2010 hali inaweza kuwa mbaya sana!!!!
Naomba kuwasilisha.
Haihitaji mtu uwe na elimu ya sayansi ya kurusha Roketi ili kujua kinachofanywa na Tume ya Uchaguzi Tanzania NEC ili kuhakikisha wanakibeba Chama Tawala cha CCM. Kwamba sasa NEC wamedhamiria kuibeba CCM bila hata aibu baada ya tamko la Mwenyekiti wa CCM(T) na Rais wa JMT Bwana John Joseph Pombe Magufuli ya kwamba CCM itatawala milele.
Tunapoelekea kwenye Chaguzi ndogo za Ubunge Jimbo la Buyungu na Udiwani katika Kata 72 inaonekana kuwa NEC wana mpango kabambe wa kuhakikisha Upinzani hawapati Jimbo la Ubunge wa Kata hata moja. Vituko vinavyojitokeza kwenye maeneo yenye wagombea wa Udiwani kwa Upinzani inasikitisha kama siyo kutishia Amani ya nchi. Kwamba sasa kuna wagombea wa Udiwani toka Upinzani wameambiwa siyo Raia wa Tanzania.....Kuna maeneo Wagombea wanasakwa na Polisi kwa kesi za Mauaji. na kuna maeneo Wagombea wanalazimishwa kujiuzulu au kujaza Fomu kimakosa kwa maksudi ili wawe DISQUALIFIED na Wasimamizi wa Uchaguzi ambao ni Wakurugenzi wa Halmashauri na Miji.
Chondechonde kwa Rais JPM aingilie kati na aepushe huu uhuni unaofanywa na wateule wake toka NEC...!!Ikibidi hata ajitokeze hadharani afute kauli yake ya CCM ITATAWALA MILELE MAANA KAULI HIYO INAONEAKANA KULETA UCHOCHEZI na ikizingatiwa tunaelekea kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka kesho 2019 na Uchaguzi Mkuu 2010 hali inaweza kuwa mbaya sana!!!!
Naomba kuwasilisha.