Tume ya Uchaguzi; Kama hamko na CCM katika hoja hizi, Mnapaswa kutoka na kukemea!

BEHOLD

JF-Expert Member
Nov 17, 2013
5,057
10,715
Ni aibu kubwa chama kikongwe kama CCM kutumia hoja muflisi kama inavyoshughudiwa katika kipindi cha kampeni za uchaguzi.

Imekuwa ni kawaida kwa Chama hiki kuibuka na hoja zenye lengo la kuzua hofu au kuchochea mgawanyiko kwa watanzania kwa nia ya kuhakikisha chama hiki kinaendelea kutawala Taifa hili kinavyotaka.

Kwa mfano:-

Mwaka 2000 CCM ilizusha hoja ya vita vya wenye kwa wenyewe kuzuka kama upinzani utapewa kuongoza nchi.

Mwaka 2010, Kwa kujua dhahiri kuwa upinzani utachukua nchi, wakaja na hoja ya udini hasa ukatoliki ili kuchafua taswira ya mgombea wa wakati huo Dr, Slaa na Chama chake CHADEMA, dhidi ya wasiokuwa wakristo na pia dhidi ya wasiokuwa wakatoliki.

Mwaka huu 2015, ambapo hatari ya CCM kupumzishwa imekuwa kubwa zaidi, Waimeibuka na hoja nyingine TATU,

KWANZA, Wameibua tena udini na hasa ULUTHERI kwakua tu mgombea wa upinzani ni Mkristo (MLUTHERI);

PILI, Wamekuja na hoja ya Ukanda, kwa maana ya atokako mgombea wa upinzani, hoja ya ukaskazini.

TATU, nimeshughudia hapa Tanga leo, ambapo tokea asubuhi wanazunguka kuwaomba watu wahudhurie mkutano wa magufuli hapo kesho, wakiwatangazia wananchi kuwa CHADEMA ni FREE MASONS.

Kwa vyovyote vile pamoja na kwamba uelewa na mwamko wa wananchi wengi umekua sana hasa katika uchaguzi huu, bado sio vyema kauli hili hizi zikaachwa bila kukemewa kwani hata cheche moja huweza kuzua moto mkubwa sana ukamaliza pori.

Ni vema Tume ya Uchaguzi, kama mwamuzi wa mtanange huu, ikakemea siasa za kibaguzi kama hizi za CCM.

Hii ni bila kusahau kauli tata za CCM hii kuwa watashinda "HATA KWA BAO LA MKONO" na pia hawako tayari kumpisha mtu ikulu kwa "USHINDI VYA VIKARATASI".
 
Mimi nashangaaa tume ya uchaguzi sjuwi ipo ipo tu, nn maana yake sasa, ccm hapa wanazidisha mda tunaona hata hawakemewi, why this? Tume ya uchaguzi nadhani ninyi ndo stering na hatima ya nchi hii katk uchaguz huu jamani hebu jitahidini kukemea na kuchukua hatua, tumeona lema kule kawekwa ndani, wengne hawawekwi kwa nn? Eee jamani mnazidiwa mpaka na humani right japo wao tunawona wanajitahid kwel kweli.
 
Hayo yote ni mateke ya mwisho ya ukataji wa roho wa CCM,nakuhakikishia kuwa hakuna wa kuikemea CCM zaidi ya wapiga kura katika sanduku la kura 25 Oktoba,2015 na kuitupilia benchi.Andaa kitambulisho chako,Ushindi mkubwa unakuja.
 
Hata mngeweka picha humu ya kuyaonesha hayo mnayo lilia. NEC watasema mmeunga unga tu. Hakika hili ni jibwa lisilo na meno. Tena likisikia kishindo linaingia mvunguni ati halikuona wala kusikia.
Kama wameshindwa kukemea kuongeza muda jana kule Morogoro ambapo kiila mpenda haki alilia, watathubutu wapi kukemea ya Tanga? Wanangojea mtu mmoja tu atoke na kujaribu kuiga uone. Lema alijaribu kuiga akakaa kwa dakika 6. Hakuona kitanda chake siku hiyo. Picha za Lowasa zinachanwa na kuchomwa moto, tena hapo Darisalama kwao, lakini hakuna hata wa kukaripia hata kwa kelele tuu.
Tunamshukuru Mungu kuwa UKAWA weshagundua hayo kuwa ni miongoni mwa mitego yao kama vile kina Dr. Mihogo na wapinzani feki wanaoupinga upinzani Tz.
UKAWA wao ni macho mbele kuelekea Magogoni tu. Na hakika, Watz wameamua, mpaka kitaeleweka tuuuu. Kwa msaada wa Mungu, Tutatenda makuu. NEC watuminye sawa, ila Ikulu 2015 Oktoba 25 lazima, kwa hivyo hivyo vikaratasi vyetu. CCM mtatupisha kwa amani
 
Ni aibu kubwa chama kikongwe kama CCM kutumia hoja muflisi kama inavyoshughudiwa katika kipindi cha kampeni za uchaguzi.

Imekuwa ni kawaida kwa Chama hiki kuibuka na hoja zenye lengo la kuzua hofu au kuchochea mgawanyiko kwa watanzania kwa nia ya kuhakikisha chama hiki kinaendelea kutawala Taifa hili kinavyotaka.

Kwa mfano:-

Mwaka 2000 CCM ilizusha hoja ya vita vya wenye kwa wenyewe kuzuka kama upinzani utapewa kuongoza nchi.

Mwaka 2010, Kwa kujua dhahiri kuwa upinzani utachukua nchi, wakaja na hoja ya udini hasa ukatoliki ili kuchafua taswira ya mgombea wa wakati huo Dr, Slaa na Chama chake CHADEMA, dhidi ya wasiokuwa wakristo na pia dhidi ya wasiokuwa wakatoliki.

Mwaka huu 2015, ambapo hatari ya CCM kupumzishwa imekuwa kubwa zaidi, Waimeibuka na hoja nyingine TATU,

KWANZA, Wameibua tena udini na hasa ULUTHERI kwakua tu mgombea wa upinzani ni Mkristo (MLUTHERI);

PILI, Wamekuja na hoja ya Ukanda, kwa maana ya atokako mgombea wa upinzani, hoja ya ukaskazini.

TATU, nimeshughudia hapa Tanga leo, ambapo tokea asubuhi wanazunguka kuwaomba watu wahudhurie mkutano wa magufuli hapo kesho, wakiwatangazia wananchi kuwa CHADEMA ni FREE MASONS.

Kwa vyovyote vile pamoja na kwamba uelewa na mwamko wa wananchi wengi umekua sana hasa katika uchaguzi huu, bado sio vyema kauli hili hizi zikaachwa bila kukemewa kwani hata cheche moja huweza kuzua moto mkubwa sana ukamaliza pori.

Ni vema Tume ya Uchaguzi, kama mwamuzi wa mtanange huu, ikakemea siasa za kibaguzi kama hizi za CCM.

Hii ni bila kusahau kauli tata za CCM hii kuwa watashinda "HATA KWA BAO LA MKONO" na pia hawako tayari kumpisha mtu ikulu kwa "USHINDI VYA VIKARATASI".

Hata hvyo kwa kua unakipenda chama unaweza usione hayo!
 
Pia MAGUFULI amekuwa akisema kuwa tukiichagua CHADEMA ya Libya yatatokea Tanzania. Mimi binafsi siogopi, ila kuna watanzania ambao hawawezi kuchambua mbivu na mbichi hawa wanaweza kutiwa hofu na MAGUFULI hivyo kupelekea kutompigia kura mgombea wamtakaye!
 
Umeongea maneno ya busara sana! ingawa pia kuna changamoto ktk fikra zako....
Hata kauli za Slaa na clips za Lowassa kusambaa hivi kunaweza kuathiri sana muelekeo wa siasa.
Tume haipaswi kukaa kimya juu ya shutuma za kidini hasa wakati huu.
Haitoshi tu kuwasikiliza kina slaa na gwajima na lowassa na kuchambua pumba, inatakiwa mamlaka husika kuingilia kati.
Lakini hata wewe haitoshi tu kuilaumu ccm wakati umeona clip ya Lowassa.
Lowassa alipaswa kujua madhara ya kauli zake. yeye ni mwanasiasa kwa zaidi ya miaka 30 anajua alichokifanya na madhara yake, inampasa awajibike kwa uzembe wake na sio kuhurumiwa kwa hilo.
Gwajima pia anapaswa kuhojiwa juu ya ushiriki wake kisiasa, kuchagua kwake kuwa na side ya kampeni kunatoa advantage kwa ukawa lkn sio kitu cha kukikalia kimya, ni sawa na kumuona mufti au pengo wakiwa ktk side moja ya kampeni, inaleta utata ktk siasa.
kauli za slaa, hazipaswi kuishia serena, tume pia inatakiwa kumuhoji yeye na Gwajima kwa kuwa kwa namna moja ama nyingine wameathiri muitikio wa wapiga kura, wameleta utata kwa umma.
pia suala la wanasiasa wakubwa kama kina makamba kuliweka hewani jambo hili na si kuliripoti kwa vyombo husika nalo si sahihi, wanaplatform ya kuliwasilisha ktk maeneo husika. ccm wanapaswa kucomplain juu ya siasa chafu za wapinzani na sio kuziweka hadharani na kuleta mtafaruku kwa watu.

wewe na ukawa wenzio badala ya kulialia yawapasa pia kuwakemea viongozi wenu waache ujinga wa kutumia mbinu ambazo zinaweza kuwaangusha, siasa za udini na ukabila ni mbaya sana. sidhani kama Lipumba au Lowassa wametengenezewa hizi clips.
Ni aibu kubwa chama kikongwe kama CCM kutumia hoja muflisi kama inavyoshughudiwa katika kipindi cha kampeni za uchaguzi.

Imekuwa ni kawaida kwa Chama hiki kuibuka na hoja zenye lengo la kuzua hofu au kuchochea mgawanyiko kwa watanzania kwa nia ya kuhakikisha chama hiki kinaendelea kutawala Taifa hili kinavyotaka.

Kwa mfano:-

Mwaka 2000 CCM ilizusha hoja ya vita vya wenye kwa wenyewe kuzuka kama upinzani utapewa kuongoza nchi.

Mwaka 2010, Kwa kujua dhahiri kuwa upinzani utachukua nchi, wakaja na hoja ya udini hasa ukatoliki ili kuchafua taswira ya mgombea wa wakati huo Dr, Slaa na Chama chake CHADEMA, dhidi ya wasiokuwa wakristo na pia dhidi ya wasiokuwa wakatoliki.

Mwaka huu 2015, ambapo hatari ya CCM kupumzishwa imekuwa kubwa zaidi, Waimeibuka na hoja nyingine TATU,

KWANZA, Wameibua tena udini na hasa ULUTHERI kwakua tu mgombea wa upinzani ni Mkristo (MLUTHERI);

PILI, Wamekuja na hoja ya Ukanda, kwa maana ya atokako mgombea wa upinzani, hoja ya ukaskazini.

TATU, nimeshughudia hapa Tanga leo, ambapo tokea asubuhi wanazunguka kuwaomba watu wahudhurie mkutano wa magufuli hapo kesho, wakiwatangazia wananchi kuwa CHADEMA ni FREE MASONS.

Kwa vyovyote vile pamoja na kwamba uelewa na mwamko wa wananchi wengi umekua sana hasa katika uchaguzi huu, bado sio vyema kauli hili hizi zikaachwa bila kukemewa kwani hata cheche moja huweza kuzua moto mkubwa sana ukamaliza pori.

Ni vema Tume ya Uchaguzi, kama mwamuzi wa mtanange huu, ikakemea siasa za kibaguzi kama hizi za CCM.

Hii ni bila kusahau kauli tata za CCM hii kuwa watashinda "HATA KWA BAO LA MKONO" na pia hawako tayari kumpisha mtu ikulu kwa "USHINDI VYA VIKARATASI".
 
Magufuli alizidisha muda wa kampeni kwa dakika 21, polisi hawakuchukua hatua

Lema kazidisha dakika 6 tu, wamemkamata

Halafu mnasema kuna uchaguzi huru na haki
 
Pia MAGUFULI amekuwa akisema kuwa tukiichagua CHADEMA ya Libya yatatokea Tanzania. Mimi binafsi siogopi, ila kuna watanzania ambao hawawezi kuchambua mbivu na mbichi hawa wanaweza kutiwa hofu na MAGUFULI hivyo kupelekea kutompigia kura mgombea wamtakaye!

Hilo la Libya ndo limefanya nimdharau Mapadlock to the max,yaani mabadiliko yaliyoletwa na mtutu under the supervision of NATO anataka ayafananishe na mabadiliko yaletwayo kwa uchaguzi huru na wa haki!

Hawa jamaa wakibanwa lazima watafute hoja dhaifu za vitisho,kitu pekee kitakacho leta machafuko katika nchi hii ni CCM kung'ang'ania madaraka hata pale itakapo kuwa dhahiri kuwa imedondoshwa.
 
Ccm wanahangaika sana kwenye social network wakifikiri itawaboost
 
Back
Top Bottom