Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC), uandikishaji wa wapigakura unaoendelea una dosari, unatia mashaka na unapaswa kurekebishwa

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,158
25,406
Binafsi, jana tarehe 12/10/2019, nimejiandikisha kwenye Orodha ya Wapigakura wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika mwezi ujao nchi mzima. Niliamua kujiandikisha kabla hata ya uhamasishaji nilioushuhudia ukifanywa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, viongozi wa CCM na wale wa CHADEMA Kibaha Mjini.

Nilifika kwenye Kituo cha Uandikishaji kwenye Ofisi za Serikali ya Mtaa ya Visiga A, Kata ya Visiga, Kibaha Pwani kwa ajili ya kujiandikisha. Nimejiandikisha kwakuwa naamininkatika demokrasia na hali zangu kama raia wa Tanzania ikiwemo hali ya kuchagua na kuchaguliwa kwenye chaguzi zinazoratibiwa na NEC.

Kituoni nilipofika kulikuwa na wahusika wawili. Mmoja alijitambulisha kwetu kama ndiye Mwandikishaji na mwingine ni Wakala, bila kuweka wazi ni Wakala wa chama au taasisi gani hasa. Tulikuwa watu watatu kwa jumla tuliohitaji kujiandikisha, wawili wakiwa wamenitangulia kwenye mstari.

Kwa nilichokishuhudia kwenye uandikishaji, uandikishaji huo una kasoro za wazi, unatia mashaka na nawaasa TAMISEMI kufanya marekebisho kwenye zoezi hilo. Waandikishwaji wanataja majina yao matatu kwa ajili ya kuandikishwa na umri wao kabla ya kutia saini zao pasipo ushahidi wowote wa mambo hayo.

Hawatakiwi kuonyesha kitambulisho chochote kuhusu majina au umri wao. Hili linawezekanaje? Udanganyifu wa majina na umri ni mkubwa mno.

Inashindikanaje kwa waliojiandikisha kurudi tena na majina na umri mwingine? Kwa uwezekano huo, naliona zoezi hilo lilivyo na kasoro na kutia mashaka.

TAMISEMI MNA jambo la kufanya katika hili ili kuhakikisha kuwa uchaguzi ujao unakuwa huru na haki. Kwa uandikishaji ulivyo, kuna kila dalili za uandikishaji batili. Nineongea nanyi TAMISEMI kwa nia njema kabisa.
 
Binafsi, jana tarehe 12/10/2019, nimejiandikisha kwenye Orodha ya Wapigakura wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika mwezi ujao nchi mzima. Niliamua kujiandikisha kabla hata ya uhamasishaji nilioushuhudia ukifanywa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, viongozi wa CCM na wale wa CHADEMA Kibaha Mjini.

Nilifika kwenye Kituo cha Uandikishaji kwenye Ofisi za Serikali ya Mtaa ya Visiga A, Kata ya Visiga, Kibaha Pwani kwa ajili ya kujiandikisha. Nimejiandikisha kwakuwa naamininkatika demokrasia na hali zangu kama raia wa Tanzania ikiwemo hali ya kuchagua na kuchaguliwa kwenye chaguzi zinazoratibiwa na NEC.

Kituoni nilipofika kulikuwa na wahusika wawili. Mmoja alijitambulisha kwetu kama ndiye Mwandikishaji na mwingine ni Wakala, bila kuweka wazi ni Wakala wa chama au taasisi gani hasa. Tulikuwa watu watatu kwa jumla tuliohitaji kujiandikisha, wawili wakiwa wamenitangulia kwenye mstari.

Kwa nilichokishuhudia kwenye uandikishaji, uandikishaji huo una kasoro za wazi, unatia mashaka na nawaasa NEC kufanya marekebisho kwenye zoezi hilo. Waandikishwaji wanataja majina yako matatu kwa ajili ya kuandikishwa na umri wao kabla ya kutia saini zao pasipo ushahidi wowote wa mambo hayo.

Hawatakiwi kuonyesha kitambulisho chochote kuhusu majina au umri wao. Hili linawezekanaje? Udanganyifu wa majina na umri ni mkubwa mno.

Inashindikanaje kwa waliojiandikisha kurudi tena na majina na umri mwingine? Kwa uwezekano huo, naliona zoezi hilo lilivyo na kasoro na kutia mashaka.

NEC MNA jambo la kufanya katika hili ili kuhakikisha kuwa uchaguzi ujao unakuwa huru na haki. Kwa uandikishaji ulivyo, kuna kila dalili za uandikishaji batili. Nineongea nanyi NEC kwa nia njema kabisa.
Mwanasheria msomi wa ngazi ya Ph.D in waiting, unatuangusha!. Uchaguzi wa serikali za mitaa, hausimamiwi na NEC.

Sifa ya kupiga kura ni presence yako mahali unapojiandikishia na ndipo utakapopigia kura kumaanisha unaishi hapo.

Hakuhitajiki kitambulisho chochote kuthibitisha jina, umri wala proof ya makazi kwasababu presence yako pale kituo cha kujiandikisha ni uthibitisho tosha.

Shime watu tujitokeze, huhitaji kitambulisho chochote.
Na siku ya kupiga kura tujitokeze kwa wingi njoo tupige kura.
P
 
Watatue kwanza changamoto yakutokuwepo waandikishwaji wengi,hata hivyo kwasasa watu wakitaka kurudiarudia hata mara 75 kwa siku wanaweza,nobody takes this issue serious except some hypocrites who in one way or another,are system beneficiaries.
 
Mwanasheria msomi wa ngazi ya Ph.D in waiting, unatuangusha!. Uchaguzi wa serikali za mitaa, hausimamiwi na NEC.

Sifa ya kupiga kura ni presence yako mahali unapojiandikishia na ndipo utakapopigia kura kumaanisha unaishi hapo.

Hakuhitajiki kitambulisho chochote kuthibitisha jina, umri wala proof ya makazi kwasababu presence yako pale kituo cha kujiandikisha ni uthibitisho tosha.

Shime watu tujitokeze, huhitaji kitambulisho chochote.
Na siku ya kupiga kura tujitokeze kwa wingi njoo tupige kura.
P
Paskali huyo ndio mwanasheria msomi,hajui kwamba uchaguzi huu wa 24 Nov 2019 haupo chini ya NEC.
 
Kaka Pascal Mayalla na wadau wengine, naomba radhi kiungwana kwa kuongea na NEC badala ya TAMISEMI. Ahusikaye na afahamu!

Hicho kitendo tu cha kwenda kujiandikisha kwenye huo uhuni kinaonyesha ww sio mtu makini. Hayo mapungufu uliyoyaona watu wenye akili timamu tumeshayasema sana humu na ndio maana tunahamasisha watu kutokwenda. Nashangaa uko humu mitandaoni lakini huwezi kuelewa nini tunasema, ama unadhani habari za humu ni za uzushi? Labda kama lengo lako lilikuwa kwenda kujiridhisha na tuhuma zetu na sio kujiandikisha.

Na kwa taarifa yako hayo uliyoyaona hayafanyiki kwa bahati mbaya, bali ni jambo la kupangwa ili ccm watangazwe washindi. Halafu utashangaa viongozi waliopatikana kwa uchafu wa aina hiyo wakihubiri kupambana na rushwa na uvunjwaji wa sheria! Katika mazingira hayo wazungu wakituita manyani tunapata wapi nguvu za kukataa? Kwa maneno marahisi huo uchaguzi ndio kipimo halisi cha ujinga na ushenzi wa kiafrika.
 
18 Reactions
Reply
Back
Top Bottom