Mikael Aweda
JF-Expert Member
- Dec 17, 2010
- 2,973
- 3,901
WanaJF,
Jumamosi, Mungu akinijalia nitahudhuria mkutano wa kwanza wa Tume ya Katiba watakapokuwa Kisarawe,pwani. Jambo hilo tunalifanya makusudi ili tupanguze yale tuliyo nayo kabla hatujapata fursa nyingine Dsm.
Kwa kuwa zoezi hili linaenda kwa kasi sana, na kwa kuwa hatuna uhakika kama tunaweza kusema kila kitu wakija hapa Dsm, na kwa kuwa hawaendi kila mahali (nina maanisha kila kata au mtaa wako) na
kwa kuwa baadhi yetu wanajf ni waajiriwa na tuko busy na hamtapata nafasi hii adimu sana na,
kwa kuwa tayari kuna malalamiko ya wakuu wa wilaya kuwaandaa watu na kuwafundisha kitu cha kusema, na kwa kuwa baadhi ya wana Jf wako nje ya nchi na wanaitakia mema nchi yetu (mf mwanakijiji etc)
Hivyo basi, kwa heshima na unyenyekevu tunaomba tukakuwakilishie hoja yako unayoona ni muhimu sana kupitia jukwaa letu murua na ambayo unahisi ni muhimu ikajumuishwa katika katiba mpya.
Tumejipanga kuhakikisha kuwa kila hoja muhimu inayoboresha muskabali wa watanzania wote bila kujali mipaka vyama, dini, kabila inawasilishwa kwenye tume husika bila upendeleo.
1) IKUMBUKWE; Vyama vinazaliwa na kufa lakini Taifa letu lipo hadi mwisho wa Dunia, hivyo ni matarajio yangu kuwa ushabiki wa kidini na kisiasa hautakuwepo ktk mjadala huu.
2) Fafanua vizuri hoja yako ili ieleweke vizuri, kiasi kwamba mwana JF ye yote ambaye atapata fursa ya kuhudhuria mikutano hii ya Katiba aweze kuelezea vizuri kwa niaba yako (siyo lazima sisi).
Sisi (kama watanzania kwanza kabla ya kuwa wanachadema) tunajitahidi kuratibu vizuri kila mahali lakini siyo garantii kuwa tutawasilisha kila jambo.
Kwa hiyo, napendekezo uzi huu hapa JF uwe kisima cha kuchukua mawazo mapya kwa kila mwana jf kutoa hoja hapa ama kuchota mawazo mapya na kuyawasilisha ktk tume husika kwa kuwa tunatofautiana uwezo wa kuibua mambo yenye maslahi kwa nchi yetu, Pili,inawezekana hoja yako mimi sikubaliani nayo, hivyo yule mwenye mawazo kama yako atayawasilisha kwa niaba yako.
NB; Paw,Silencer, PainKiller, Roulette, Fang, Buchanan, Cookie ni matarajio yangu kuwa uzi huu mtaupa muda kidogo ili tupate mawazo mengi kwa maslahi ya nchi yetu.
Regards
Aweda, Mikael
Jumamosi, Mungu akinijalia nitahudhuria mkutano wa kwanza wa Tume ya Katiba watakapokuwa Kisarawe,pwani. Jambo hilo tunalifanya makusudi ili tupanguze yale tuliyo nayo kabla hatujapata fursa nyingine Dsm.
Kwa kuwa zoezi hili linaenda kwa kasi sana, na kwa kuwa hatuna uhakika kama tunaweza kusema kila kitu wakija hapa Dsm, na kwa kuwa hawaendi kila mahali (nina maanisha kila kata au mtaa wako) na
kwa kuwa baadhi yetu wanajf ni waajiriwa na tuko busy na hamtapata nafasi hii adimu sana na,
kwa kuwa tayari kuna malalamiko ya wakuu wa wilaya kuwaandaa watu na kuwafundisha kitu cha kusema, na kwa kuwa baadhi ya wana Jf wako nje ya nchi na wanaitakia mema nchi yetu (mf mwanakijiji etc)
Hivyo basi, kwa heshima na unyenyekevu tunaomba tukakuwakilishie hoja yako unayoona ni muhimu sana kupitia jukwaa letu murua na ambayo unahisi ni muhimu ikajumuishwa katika katiba mpya.
Tumejipanga kuhakikisha kuwa kila hoja muhimu inayoboresha muskabali wa watanzania wote bila kujali mipaka vyama, dini, kabila inawasilishwa kwenye tume husika bila upendeleo.
1) IKUMBUKWE; Vyama vinazaliwa na kufa lakini Taifa letu lipo hadi mwisho wa Dunia, hivyo ni matarajio yangu kuwa ushabiki wa kidini na kisiasa hautakuwepo ktk mjadala huu.
2) Fafanua vizuri hoja yako ili ieleweke vizuri, kiasi kwamba mwana JF ye yote ambaye atapata fursa ya kuhudhuria mikutano hii ya Katiba aweze kuelezea vizuri kwa niaba yako (siyo lazima sisi).
Sisi (kama watanzania kwanza kabla ya kuwa wanachadema) tunajitahidi kuratibu vizuri kila mahali lakini siyo garantii kuwa tutawasilisha kila jambo.
Kwa hiyo, napendekezo uzi huu hapa JF uwe kisima cha kuchukua mawazo mapya kwa kila mwana jf kutoa hoja hapa ama kuchota mawazo mapya na kuyawasilisha ktk tume husika kwa kuwa tunatofautiana uwezo wa kuibua mambo yenye maslahi kwa nchi yetu, Pili,inawezekana hoja yako mimi sikubaliani nayo, hivyo yule mwenye mawazo kama yako atayawasilisha kwa niaba yako.
NB; Paw,Silencer, PainKiller, Roulette, Fang, Buchanan, Cookie ni matarajio yangu kuwa uzi huu mtaupa muda kidogo ili tupate mawazo mengi kwa maslahi ya nchi yetu.
Regards
Aweda, Mikael