Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,498
Taarifa ya INEC imetolewa leo Machi 23, 2025 na Mwenyekiti wa tume hiyo, Jaji Jacobs Mwambegele ikiwa ni siku moja tangu Mwananchi iripoti wingi wa watu vituoni na malalamiko ya baadhi kushindwa kuboresha taarifa zao.
Uboreshaji wa taarifa huo awali mkoani Dar es Salaam ulianza Machi 17 na ulitakiwa kumalizika leo Jumapili Machi 23, 2025.
"Kama mnavyofahamu Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi inaendelea na hatua ya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapigakura kwa Mkoa wa Dar es Salaam, hatua ambayo kwa mujibu wa ratiba ilianza Machi 17, 2025 na ilitarajiwa kukamilika Machi 23, 2025."
"Kutokana na mwitiko mkubwa Tume ilichukua hatua za kuongeza mashine za bvr kits pamoja na watumishi katika maeneo yote yaliyoonekana kuwa na watu wengi na hatua hii imewezesha shughuli hiyo kuendelea kwa utulivu katika maeneo yote. Hatua hiyo imewezesha kuongeza kasi ya kuwahudumia wananchi na kupunguza kwa kiasi kikubwa misongamano kwenye baadhi ya maeneo," imeeleza taarifa hiyo.
Taarifa hiyo imeongeza kuwa: "Licha ya hatua zilizochukuliwa na Tume, bado katika maeneo kadhaa kuna mwitikio mkubwa wa wananchi. Hivyo basi, napenda kuwatangazia wananchi wote wa mkoa wa Dar es Salaam kuwa Tume imeongeza siku mbili za uboreshaji wa daftari kwa Machi 24 na 25, 2025."