Tanzania inahitaji kiongozi mwenye uchungu na Watanzania,viongozi kama Nyerere na Sokoine(R.I.P) ni vigumu kuwapata kwenye zama zetu hizi.
Inawezekana lakini sitaki kuamini hivyo. Tatizo ni mfumo si kiongozi naomba nifafanue kwa lugha nyepesi mfumo ni sawa na gari huwezi kufika unakokwenda kama gari ni bovu hata ukiwa na dereva mzuri kiasi gani (kiongozi) ili uweze kufika salama uendako una njia 2 tu za kufanya ama uuze hilo gari bovu ununue gari nyingine imara ama ulikarabati kwanza (major overhaul) sasa zama za Nyerere na sokoine gari au mfumo waliokua wanausimamia ulikua bora kiasi .Sasa mfumo huo (gari) limeoza halifai na wala hauwezi kulikarabati tena njia na suluhisho la pekee ni kunnua gari jipya (mfumo mbadala) ili tufike huko tunakotaka kubadili dereva pekee haitoshi.