Tulipokwama kama Taifa; tutajinasua?

Tanzania inahitaji kiongozi mwenye uchungu na Watanzania,viongozi kama Nyerere na Sokoine(R.I.P) ni vigumu kuwapata kwenye zama zetu hizi.

Inawezekana lakini sitaki kuamini hivyo. Tatizo ni mfumo si kiongozi naomba nifafanue kwa lugha nyepesi mfumo ni sawa na gari huwezi kufika unakokwenda kama gari ni bovu hata ukiwa na dereva mzuri kiasi gani (kiongozi) ili uweze kufika salama uendako una njia 2 tu za kufanya ama uuze hilo gari bovu ununue gari nyingine imara ama ulikarabati kwanza (major overhaul) sasa zama za Nyerere na sokoine gari au mfumo waliokua wanausimamia ulikua bora kiasi .Sasa mfumo huo (gari) limeoza halifai na wala hauwezi kulikarabati tena njia na suluhisho la pekee ni kunnua gari jipya (mfumo mbadala) ili tufike huko tunakotaka kubadili dereva pekee haitoshi.
 
- Haya yote ilikuwa tunayaendesha kwa hasara, yaani behind a hoax ideology, mashirika ya umma yalikua a big lie Tanzania tukawa nchi ya kwanza duniani kuwa na kampuni za bia na sigara zinazoendeshwa kwa hasara, leo hizi kampuni mbili ndio tegemeo letu nationally katika hela za matumizi ya serikali maana kodi kubwa inakusanywa na serikali toka hapa, lakini sio enzi zile tunazoambiwa tulikuwa paradise, as if hatukuwepo vile,

- Leo hakirushwi kitu tena, hakuna bia ya kuruka, mchele wa kuruka, sabuni imperial ya kuruka, raba za mtoni, wala ugali wa yanga hakuna tena na zile foelni za ungwa wa njano na sukari hakuna tena, labda tunamkumbuka kiongozi aliyekua serious na uongozi na maadili binafsi ya uongozi, lakini otherwise wengine tunakumbuka petroli ya kuruka na haiuzwi Jumapili, that was a very sad situation, cement ya kuruka, I mean ulikuwa ni mwendo wa kuruka kila kona ya maisha, I mean tulikwua wadogo kiumri, lakini tulijuionea mengi ya ajabu ambayo tukiwaambia vijuana wetu wa kisasa hawaamini kabisa kama ni kweli!

- Hatuwezi kujinasua kwa sababu hatujui hata tuliponasia ni wapi na tumenasa na nini, tutaendelea kuzunguka tu bila kusonga mbele kwa sababu mifano hakuna!

Respect.


FMEs!

Hii obsession yako na Mwalimu imekuwekea wingu zito usoni mpaka unashindwa kabisa kuona mambo mengi tu kwa usahihi wake kamili. Hebu jaribu kutoa timeline kwa haya mambo unayoyadai ili tuweze kupima kama yalisababishwa na mapungufu ndani au nje ya Azimio. AD ilitangazwa mwaka 1967, je ilichukua muda gani kwa matatizo hayo unayoyadai kutokea na yalisababishwa na nini.

Duniani kote watu wote hawawezi kukubaliana kwa kila jambo hata likiwa zuri namna gani na hasa linapokinzana na maslahi ya kundi fulani. Hivi sasa tunashuhudia Marekani ilivyogawanyika katika swala la afya kwa wote na kuna wanaoapa kabisa eti lisifanikiwe - naam, ndivyo watu walivyo. Ni hapo mafanikio yatakapoonekana ndiyo hao wenye roho ngumu watakapoweza kusalimu amri japo shingo upande.

Lakini hali hii ipo tofauti kidogo kwa nchi masikini na changa kama yetu. Shuhudia inavyokuwa vigumu kuwashughulikia hata mafisadi - watu ambao dhahiri tungeweza kuwaita wahujumu uchumi. Ni rahisi kwa watu wenye uwezo wa kifedha kuwarubuni wananchi ambao wengi wao ni masikini wa kutupwa kuwaunga mkono. Ndio maana demokrasia kwenye nchi kama zetu siku zote hazifanikiwi au hubaki zikisuasua.

Viwanda vingi baada tu ya kutaifishwa, pamoja na kukosa wataalamu waliobobea, vilifanya kazi vizuri tu na na kwa faida kubbwa tu. Kama kuna wakati tuliweza kufanya biashara kama kuuza nje bidhaa za viwango zilizotengenezwa Tanzania ni wakati huo. Lakini kuna walioapa toka mwanzoni kuhakikisha kuwa Azimio halifanikiwi kabisa. Hebu fikiria the Patels, the Somaiyas and the Rostamus wa wakati huo.

Uwezo wa kuvihujumu walikuwa nao na viwanda viliweza kuhujumiwa, period. Hata hivyo tuliweza kustahimili na kupambana na hizi hujuma za ndani mpaka pale matatizo yalipojitokeza nje ya uwezo wetu kama kupanda kwa bei ya mafuta duniani na vita vya Kagera. Of course kuna Watanzania ambao wanaona hivi vita havikuwa lazima na kuna wanaoenda mbali zaidi na kudai tulimwonea Idi Amin lakini kama alivyosema Mwalimu - sabau, nia na uwezo vyote tulikuwa navyo.

Je, kabla ya vita kama hali ingekuwa mbaya unavyotaka kutuaminisha, huo uwezo tungeupata wapi kwani ni kweli tulimpiga yeye, Walibya na Wapalestina waliokuja kumsaidia. Tulikuwa na uwezo wa kumtoa mvamizi wa ardhi yetu lakini leo hii hatuna hata uwezo wa kuwatoa mafisadi wanaotafuna rasilimali za taifa kama mchwa. Hivi sasa hatuna hata cha kujivunia halafu wanatokea watu kama wewe - unakuwa na jeuri ya kumkashifu Mwalimu, shame on you.
amin-with-army-new.jpg

Jemadari Mkuu akiwatembelea vijana wake wakati wanatembeza kipigo kumtoa nyoka pangoni.
 
Inawezekana lakini sitaki kuamini hivyo. Tatizo ni mfumo si kiongozi naomba nifafanue kwa lugha nyepesi mfumo ni sawa na gari huwezi kufika unakokwenda kama gari ni bovu hata ukiwa na dereva mzuri kiasi gani (kiongozi) ili uweze kufika salama uendako una njia 2 tu za kufanya ama uuze hilo gari bovu ununue gari nyingine imara ama ulikarabati kwanza (major overhaul) sasa zama za Nyerere na sokoine gari au mfumo waliokua wanausimamia ulikua bora kiasi .Sasa mfumo huo (gari) limeoza halifai na wala hauwezi kulikarabati tena njia na suluhisho la pekee ni kunnua gari jipya (mfumo mbadala) ili tufike huko tunakotaka kubadili dereva pekee haitoshi.

Mkuu Miner,kama unasema kuwa inawezekana tunahitaji viongozi wa caliber ya mwalimu na Sokoine,je una maanisha kuwa ni mfumo peke yake ndiyo uliowaangusha?

Na kama mfumo huu unawa favor mafisadi,sasa utategemea vipi waubadilishe?Kuna mtu mwenye kutaka kukata tawi la mti alilokalia?

Hapo utaona kuwa cha kwanza ni viongozi wapya then mfumo mpya...Kwasababu hao viongozi walio "uozesha" mfumo ni kivipi wataufanya mpya? Na sababu za wao kuufanya mpya zitakuwa zipi?

Tunahitaji both gari mpya na dereva mpya!

Gari jipya na dreva yule yule aliyeliozesha gari la zamani ni mabadiliko gani?Sheria si unaona zinabadilishwa/kuozeshwa?

Tafakari tena labda unaweza kuwa na jibu la tofauti!
 
Mkuu hapa umenifanya nifikirie sana; inawezekana uko sahihi kuliko unavyowezea kujua maana kama unayosema ni kweli basi yawezekana matatizo yetu baada ya uhuru hadi alipokuja Mwinyi hayakuwa makosa ya Mwalimu! Hakukuwa na watu wa kutekeleza zile njozi zetu za taifa. Ingekuwa vigumu sana kwa Nyerere kufanya kila kitu yeye mwenyewe; kiongozi ni lazima awe na watu anaowategemea.

Leo hii mojawapo ya mambo tunayogongana nayo katika uongozi wetu ni kama abebe lawama Kikwete au wasaidizi wake. Kwa kiasi kikubwa tunaambiwa ni wasaidizi wake ndio wanamuangusha, lakini upande mwingine tunasema "the buck stop with the president".

Je Rais yeyote anaweza kufanikiwa bila ya kuwa na watu anaoweza kuwaamini kutekeleza sera na maagizo yake?

Je, wale wanaodhaminiwa nafasi mbalimbali wanatakiwa wasimamiwe na Rais kwa kila kitu ili wakifanikishe?

Kwa kweli inawezekana tatizo letu la uongozi ni kubwa zaidi kuliko ni Rais gani yuko madarakani.

Hii obsession yako na Mwalimu imekuwekea wingu zito usoni mpaka unashindwa kabisa kuona mambo mengi tu kwa usahihi wake kamili. Hebu jaribu kutoa timeline kwa haya mambo unayoyadai ili tuweze kupima kama yalisababishwa na mapungufu ndani au nje ya Azimio. AD ilitangazwa mwaka 1967, je ilichukua muda gani kwa matatizo hayo unayoyadai kutokea na yalisababishwa na nini.

Duniani kote watu wote hawawezi kukubaliana kwa kila jambo hata likiwa zuri namna gani na hasa linapokinzana na maslahi ya kundi fulani. Hivi sasa tunashuhudia Marekani ilivyogawanyika katika swala la afya kwa wote na kuna wanaoapa kabisa eti lisifanikiwe - naam, ndivyo watu walivyo. Ni hapo mafanikio yatakapoonekana ndiyo hao wenye roho ngumu watakapoweza kusalimu amri japo shingo upande.

Lakini hali hii ipo tofauti kidogo kwa nchi masikini na changa kama yetu. Shuhudia inavyokuwa vigumu kuwashughulikia hata mafisadi - watu ambao dhahiri tungeweza kuwaita wahujumu uchumi. Ni rahisi kwa watu wenye uwezo wa kifedha kuwarubuni wananchi ambao wengi wao ni masikini wa kutupwa kuwaunga mkono. Ndio maana demokrasia kwenye nchi kama zetu siku zote hazifanikiwi au hubaki zikisuasua.

Viwanda vingi baada tu ya kutaifishwa, pamoja na kukosa wataalamu waliobobea, vilifanya kazi vizuri tu na na kwa faida kubbwa tu. Kama kuna wakati tuliweza kufanya biashara kama kuuza nje bidhaa za viwango zilizotengenezwa Tanzania ni wakati huo. Lakini kuna walioapa toka mwanzoni kuhakikisha kuwa Azimio halifanikiwi kabisa. Hebu fikiria the Patels, the Somaiyas and the Rostamus wa wakati huo.

Uwezo wa kuvihujumu walikuwa nao na viwanda viliweza kuhujumiwa, period. Hata hivyo tuliweza kustahimili na kupambana na hizi hujuma za ndani mpaka pale matatizo yalipojitokeza nje ya uwezo wetu kama kupanda kwa bei ya mafuta duniani na vita vya Kagera. Of course kuna Watanzania ambao wanaona hivi vita havikuwa lazima na kuna wanaoenda mbali zaidi na kudai tulimwonea Idi Amin lakini kama alivyosema Mwalimu - sabau, nia na uwezo vyote tulikuwa navyo.

Je, kabla ya vita kama hali ingekuwa mbaya unavyotaka kutuaminisha, huo uwezo tungeupata wapi kwani ni kweli tulimpiga yeye, Walibya na Wapalestina waliokuja kumsaidia. Tulikuwa na uwezo wa kumtoa mvamizi wa ardhi yetu lakini leo hii hatuna hata uwezo wa kuwatoa mafisadi wanaotafuna rasilimali za taifa kama mchwa. Hivi sasa hatuna hata cha kujivunia halafu wanatokea watu kama wewe - unakuwa na jeuri ya kumkashifu Mwalimu, shame on you.
amin-with-army-new.jpg

Jemadari Mkuu akiwatembelea vijana wake wakati wanatembeza kipigo kumtoa nyoka pangoni.

Kwanza nianze kwa kusema Wakuu asanteni sana kwa useful posts hizo hapo juu...........

Mkuu jmushi1

Tumekwama as a nation kwa sababu ya..........choyo, chuki, unafiki, ujambazi wa sasa wa CCM, na ubinafsi................Taifa tumekosa muelekeo.........tumebaki ku-imitate tu...........
 
- Haya yote ilikuwa tunayaendesha kwa hasara, yaani behind a hoax ideology, mashirika ya umma yalikua a big lie Tanzania tukawa nchi ya kwanza duniani kuwa na kampuni za bia na sigara zinazoendeshwa kwa hasara, leo hizi kampuni mbili ndio tegemeo letu nationally katika hela za matumizi ya serikali maana kodi kubwa inakusanywa na serikali toka hapa, lakini sio enzi zile tunazoambiwa tulikuwa paradise, as if hatukuwepo vile,

- Leo hakirushwi kitu tena, hakuna bia ya kuruka, mchele wa kuruka, sabuni imperial ya kuruka, raba za mtoni, wala ugali wa yanga hakuna tena na zile foelni za ungwa wa njano na sukari hakuna tena, labda tunamkumbuka kiongozi aliyekua serious na uongozi na maadili binafsi ya uongozi, lakini otherwise wengine tunakumbuka petroli ya kuruka na haiuzwi Jumapili, that was a very sad situation, cement ya kuruka, I mean ulikuwa ni mwendo wa kuruka kila kona ya maisha, I mean tulikwua wadogo kiumri, lakini tulijuionea mengi ya ajabu ambayo tukiwaambia vijuana wetu wa kisasa hawaamini kabisa kama ni kweli!

- Hatuwezi kujinasua kwa sababu hatujui hata tuliponasia ni wapi na tumenasa na nini, tutaendelea kuzunguka tu bila kusonga mbele kwa sababu mifano hakuna!

Respect.

FMEs!


FMES,

Hakuna nchi hata moja dunia hii ambayo haina shirika la umma au haikuwa na Dola iliyoshikilia uchumi na uzalishaji mzima.

Hata Uingereza, Marekani, Ujerumani, Ufaransa na nchi za magharibi zilizokuwa na maendeleo ya Viwanda, hadi miaka ya karibuni bado zimeendela kuwa na mashirika ya umma katika nyanja mbali mbali.

Hivyo kulaumu Tanzania au uongozi wa Tanzania kushikilia uzalishaji na kuonyesha kana kwamba sisi tulikuwa nchi pekee tuliyowahi kufanya kitu kama hicho ni upotoshaji na kujidanganya kama si kujivua kile tulichoweza kufanya.

Likija kwenye suala la uhaba wa vitu, je umeshawahi kusoma historia ya Great Depression na kilichotokea Marekani?

Watu walipanga foleni ya chakula, nguo, ajira na hata mafuta ya gari. Tena hapo ndipo kulikuwa na kile kipindi cha prohibitation kuanzia kwenye Pombe moaka Sigara!

Leo hii Marekani ni kosa la jinai kuvusha pombe au sigara kutoka mkoa mmoja na kwenda mwingine, na kuna kikosi maalumu cha ATF kunachosimamia hilo.

Tuna mengi ya kujivuna kuliko vichache tulivyoshindwa kuvipata. Tulipopata Uhuru tumepiga hatua moja kubwa kama Taifa katika mambo mengi sana hasa Umoja na hata kuwa na lugha moja ya maelewano.

Tanzania ni moja ya nchi chache sana za Dunia ya Tatu ambayo imesogeza maendeleo ya namna fulazi katika kila kona ya nchi.

Je tunaridhika na tulichonacho, jibu ni hapana kwa kuwa tunabaini kuna mengi ambayo tungeweza kuyafanya na kutufanya tuwe bora.

Je tuendelee kulia na kulaumu ya kale au kutafuta mbinu mpya ya kurekebisha na kusahihisha tulipopotea? jibu ni ndiyo.

Leo hii tuna miaka 20 tangu tuwe na mfumo wa soko Huria na kuruhusu Sekta binafsi ishikilie misingi ya uzalishaji.

Lakin Umaskini wa yule mwananchi pale Kisiju haujabadilika tangu mwaka 1985 mpaka leo hii. nenda pale Chanika watu bado wanakaa kwenye nyumba za udongo, hawana maji, hawana umeme, hawana ajira, watoto wao wanakwenda shule zisizo na madawati, lakini maduka yamejaa kila aina ya sabuni, manukato na nguo! Kuna bia za mpaka kutoka Uchina na kila kitu unachokitaka ambacho kiko ulaya ulaya kipo, lakini Mtanzania hana fedha kununua hata kile kinachotengenezwa Tanzania.

Kila kitu kimebakia fahari ya macho!
 
Nakumbuka kanga za Mwatex, Urafiki na Mutex, nakumbuka betri za National, nakumbuka nyama za kusindika za Tanganyika packers, nakumbuka dawa za mbu za Expel, nakumbuka baiskeli zetu, nakumbuka kiwanda cha kuunganisha redio, nakumbuka sabuni zetu za kufulia na kuogea, pombe zetu za kienyeji, nakumbuka --- n.k. n.k.(nostalgia kali !)

Naam vyote hivi tulikuwa navyo hii ilikuwa ni vision ya Mwalimu Baba yetu wa Taifa katika kuhakikisha uchumi wa Tanzania unakuwa mikononi mwa Watanzania. Nakumbuka Tanelec kule Mwanza, nakumbuka tuliwahi kuwa nambari 1 duniani katika kusafirisha korosho na mkonge nje ya nchi. Viwanda vyote ndiyo vilikuwa na matatizo ambayo yangeweza kabisa kurekebishwa ili viendelee kuwepo na kusaidia kutoa ajira chungu nzima kwa Watanzania na kuongeza mapato ya Serikali. Tukapata viongozi ambao wakiona Mzungu basi hawaulizi chochote kile kinachosemwa na Mzungu huo.

Wakatuletea SAP (Structure Adjustment Program)ili kureform uchumi wetu (Program ambazo hazikuwa na manufaa yoyote katika developing countries pamoja na kupigiwa debe sana na IMF na WB) na masharti kibao kwamba viwanda vyote hivyo viuzwe wenyewe wakaiita sera ya ubinafsishaji. Leo hii ukiwauliza kama nchi Watanzania tumepiga hatua gani za kimaendeleo kutokana na sera za ubinafsishaji!? Wanabaki kung'aa macho. Ukiwauliza Mwalimu aliwakatalia IFM na WB kushusha thamani ya shilingi yetu, nyie mkakubali kushusha thamani ya shilingi yetu je kushushwa huko kwa shilingi kumetuletea mafanikio gani kama nchi!? wanakuwa hawana jibu. Tatizo kubwa la nchi yetu ni Viongozi ambao wanajifanya kujua sana kila kitu na kutotaka kuwashirikisha Wananchi katika maamuzi mbali mbali.

Hawa wakiingia madarakani cha kwanza wanachokifikiria ni kujitarisha kwa speed kali sana wao, ndugu, jamaa na marafiki wao wa karibu. Wakimaliza awamu yao ya miaka 10 na tukiangalia nyuma nini walichokifanya walipokuwa madarakani hatuoni lolote lile zaidi ya madudu tu. Kwa chama chenye kupenda Wananchi wake na kuweka maslahi ya nchi mbele Kikwete asingestahili kabisa hata jina lake kutajwa kama ni mgombea wa 2010 maana kuna ushahidi wa kutosha kabisa kwamba kazi imemshinda vibaya sana, lakini huko ndani ya chama kuna Viongozi wa siku nyingi hawaoni hata soni kutamka hadharani kwamba ndani ya chama chetu kuna utamaduni wa kuachiana mtu amalize awamu zake mbili bila kumuingilia!! Kwa maana nyingine hata akiboronga kama Kikwete anaambiwa fukia mashimo tusonge mbele bila kuangalia maslahi ya nchi.

Mpaka hapo tutakapopata Viongozi katika vyama hivi watakaoweka maslahi ya nchi yetu mbele badala yao wenyewe na vyama vyao Tanzania itaendelea kusuasua kimaendeleo kwa miaka mingi ijayo nasema yote haya kwa kusikitika sana lakini ndiyo ukweli wa mambo kuhusu nchi yetu pamoja na rasilimali chungu nzima tulizonazo lakini bado hatuoni maendeleo ya kweli kwa miaka 50 tangu tuwe huru.
 
quote me: "Tulipoacha kulijenga taifa ndipo tulipoanza kulibomoa".. matokeo yake leo tunafurahia mitumba hadi ya kandambili wakati tunabeza uwepo wa kiwanda cha viatu cha BORA; leo tunafurahia mazuria toka Uarabuni wakati tulikuwa tujengeneza ya kwetu wenyewe; mablanketi yetu kutoka kiwanda cha mablanketi yanatumiwa sijui na nani (sijui kama kile kiwanda kipo anyway).. Tumefikia mahali hadi tunawaweezaji wanaotujengea vyoo kama mamlaka ya maji taka ya mbeya ilivyodokeza hivi juzi tu..
Ndo maana nilimpigia kura, wapi viwanda mkuu? Au huoni umuhimu labda wa kuongelea hili?
 
- Tunawaheshimu Sokoine na Mwalimu only kwa sababu hawakuwa mafisadi, lakini kwa hali tuliyonayo ya kuvuna walichopanda hakuna cha kuonyesha, hili taifa hatujawahi kuwa na viongozi wenye uwezo wa kuongoza, tizama kina George Washington, waliyoyapanda mpaka leo yapo, sisi imekwua exuses tu kila siku tufike mahali tukubali ukweli tu kwamba we never had it!

- Viongozi wenye uwezo hujenga institutions na policies imara ambazo hata wakifa au kuondoka hapahitajiki watu mbadala wa kupokea vijiti vyao, Rais mbovu kama Carter huondolewa kwa kura after one term, lakini sisi alimaliza term zote mbili, sasa tutaendelea kulaumiana tu ni wewe ni yule sio mimi, yaliyopita si ndwele sasa tutafute yajayo!

Respect.


FMEs!
Haya ni maneno yako wewe Lemutuz? Kweli kuishi kweingi ni kuona mengi! cc minyoo
 
Mkuu Mushi, mtu huvuna alichopanda. Mwanzoni kabisa katika safari yetu kama taifa tulianza vizuri kwa kuamua kurutubisha utu wa Mtanzania kwa kuyapa kipaumbele mambo matatu ya msingi - afya, elimu na umoja. Hii misingi pamoja na kutupa heshima haikuwa rahisi kuiendeleza kwani ilihitaji uvumilivu, ustahimilivu na nidhamu ya hali ya juu. LAKINI njiani wakatokea walafi wakatafuta njia walizofikiria ni nyepesi za kufikia malengo yetu na za mkato ambazo hazikuhitaji kuzitolea jasho. Wakadai walihitaji colgate, wakadai walichoka kulishwa unga wa yanga, wakadai heri wakati wa mkoloni kuliko AD na hadi leo baada ya miaka 25 bado wanamlaumu Mwalimu. Mali, tamaa na utengano zikaota mizizi na matunda yake tunayashuhudia hadi leo kwa kukosekana misingi ya uadilifu, uaminifu na ustaarabu na badala yake kujengeka vitendo vya rushwa, ufisadi na uroho wa madaraka. Mkuu Mushi hapa tulipo all hell has broken loose and it will take nothing less than a revolution to fix it - a desperate and unfortunate action to take but sadly necessary.
This certainly still relevant!
 
Tumekwama kama Taifa kutokana na mambo makuu 4.
1. Siasa
2..Mipango
3.Usimamizi
4. Utekelezaji
Mwl. Nyerere alipata kusema ili tuendelee tunahitaji watu, ardhi na siasa safi.Watu wapo na ardhi pia tatizo ni siasa mbaya kama leo TIC wanatagaza kugawa ardhi yetu kwa wakoloni walewale kulikua na sababu gani ya kudai uhuru na kujitawala Watanzania ni lazima tukatae tena kwa kijitoa hadharani na silaha zetu za jadi kama walivyofanya wananchi waliodai ardhi yao waliyopewa Nafco.
Tutaendelea vipi kama hatuna mipango. Mpango wa kwanza wa maendeleo wa miaka 5 ulikua 1965 hadi 1970 nawa pili 1970-75 baada ya hapo nchi imepelekwa wanavyotaka watawala hebu angalia awamu hii tu miaka ya uongozi wa Lowasa ilikua Elimu na kipindi kilichobakia katika awamu hii chini ya uongozi wa Pinda ni kilimo hakuna tena ujenzi wa madarasa kwa kasi ile sasa halmashauri zinashindana kununua power tillers.
Tutaendelea vipi kama hatuwezi kutekeleza yale tulioamua na kuyasimamia ipasavyo ni wajibu wetu sote kuchukua hatua sasa.Nabii Mussa aliwatoa wana wa israeli misri akatangatanga nao jangwani na hakuwafikisha katika nchi ya ahadi ya maziwa na asali na CCM wametutoa katika ukoloni leo miaka 48 tunatangatanga na umskini , shida na taabu kamwe hawatatufikisha kwenye neema tele ni lazima tuchukue hatua..NDIO TUNAWEZA ; PAMOJA TUNAWEZA.
Kuhusu kila mtawala kuja na kufanya anachotaka! Umegongea penyewe kabisa! Ndo yale yale tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom