Tuliowahi kupata pesa na kufilisika/kufulia, tujikumbushe hapa

View attachment 2592498
Mimi ni programmer kuna project nilipata kampuni x la mtandao wa simu na baada ya kuikamilisha hii ndo amount nimelipwa ( 12,000,000 ) baada ya dalali kukata yake na kodi za serikali kukatwa , sijawahi miliki this amaont.

Nimeicha kama wiki hivi sasa nikifikiria nini cha kufanya ili kui zalisha hii hela naomba nipate ushauri na mimi nisije imaliza kwa kujilaumu

NB: Sijaoa bado nimepanga na chuo nimamaliza 2021 nyumbani hawanitegemei sana maana kila mtu ana jishughulisha kiasi.
Unaendeleaje na hicho kiasi...?
Dadeki bonge la mtaji.
 
View attachment 2592498
Mimi ni programmer kuna project nilipata kampuni x la mtandao wa simu na baada ya kuikamilisha hii ndo amount nimelipwa ( 12,000,000 ) baada ya dalali kukata yake na kodi za serikali kukatwa , sijawahi miliki this amaont.

Nimeicha kama wiki hivi sasa nikifikiria nini cha kufanya ili kui zalisha hii hela naomba nipate ushauri na mimi nisije imaliza kwa kujilaumu

NB: Sijaoa bado nimepanga na chuo nimamaliza 2021 nyumbani hawanitegemei sana maana kila mtu ana jishughulisha kiasi.
Unaendeleaje na hicho kiasi...?
Dadeki bonge la mtaji.
 
Nimewahi kufanya kazi fulani nje ya Tz kwa miaka mitatu mpaka nakuja kukacha kazi nilikuwa nimesave $137,000 kitu pekee nilichofanikisha ni kujenga nyumba na kununua gari tu maana biashara niliyoanzisha ni kama ilinirudisha nyuma tu sahizi kwenye akaunti hata 10M sidhani kama itafika......anyway kitu cha muhimu nikichogundua kijana kama una nafasi ya kuwekeza fanya hivyo ingali bado hujaoa japo wapo wanaotoboa pia wakiwa kwenye ndoa
 
Nimewahi kufanya kazi fulani nje ya Tz kwa miaka mitatu mpaka nakuja kukacha kazi nilikuwa nimesave $137,000 kitu pekee nilichofanikisha ni kujenga nyumba na kununua gari tu maana biashara niliyoanzisha ni kama ilinirudisha nyuma tu sahizi kwenye akaunti hata 10M sidhani kama itafika......anyway kitu cha muhimu nikichogundua kijana kama una nafasi ya kuwekeza fanya hivyo ingali bado hujaoa japo wapo wanaotoboa pia wakiwa kwenye ndoa
Ulikunja parefu sana ,vipi nyumba ya maana lakini?
 
Nimewahi kufanya kazi fulani nje ya Tz kwa miaka mitatu mpaka nakuja kukacha kazi nilikuwa nimesave $137,000 kitu pekee nilichofanikisha ni kujenga nyumba na kununua gari tu maana biashara niliyoanzisha ni kama ilinirudisha nyuma tu sahizi kwenye akaunti hata 10M sidhani kama itafika......anyway kitu cha muhimu nikichogundua kijana kama una nafasi ya kuwekeza fanya hivyo ingali bado hujaoa japo wapo wanaotoboa pia wakiwa kwenye ndoa
Mil 300 plus mkuu aiseee..!!
 
Mkuu nilishusha mansion ya kwenda maeneo ya kibada nikavuta na kausafiri kangu tako la nyani starehe zikanizidia mpunga umekata najipanga kuanza upya mzee but sio mbaya ilikuwa ni ujana na ninacho cha kujivunia kwamba muda wangu haukupotea bure....pesa inatafutwa tu mzee
Kama sio alex wewe sio bure....ulivyotoka Japan ulikuwa vizuri zaidi ya sana
 
Kwa mara ya kwanza kudraw hela ya Forex 2 Million, kwa akili zangu those days iyo hela sio rahisi kuisha.

Niliwahi lipia mhudumu mmoja alikuwa off duty nauli ya Tax usiku saa 7 aje anichanganyie cocktails eti siwezi kulala bila iyo kitu.

Ilikuwa ukinikuta nimetulia bar hata kama sikujui na umenizidi umri utasikia, "mbona unanikosea adabu, weita mpige huyu na bia anazotaka" hapo niko na John walker red label.

Mamaaaee ile hela hata Boksa sikununua.
Daah hela mwanaharamu aisee😂😂
 
Nina mjomba wangu mmoja hivi alikuwa anaimba imba kwenye hizi bendi za muziki kipindi hicho. Unawataja ma papaa, watu wazito alaf wanakutunza pesa ndefu. Sasa sijui alipigaje hela, ila alikuja kumiliki pesa ndefu. Mjini akawa yeye ndio Don, kila kona ana demu. Muda wote kachomekea, starehe mwanzo mwisho. Baada ya miezi kadhaa akafulia mbaya, hadi soo.

Akapotelea migodini. Huko alikaa kama miaka miwili au mitatu. Akapiga mshindo wa maana. Kurudi town ana hela chafu. Akiingia bar anatoa watu wote, anaikodi bar alaf anabaki na wapambe wake tu. Kuna siku mlevi mmoja wakati anatolewa nje kwavile bar imekodiwa na anko, yule mlevi alitukana. Anko akaomba aitiwe huyo aliyetukana. Kabla hata hajamwangalia usoni, akamuagiza mhudumu ampe yule mlevi kreti za bia sawa na urefu wake. Siku nyingine anaweza akatoa order kuwa wahudumu wote wa bar wabaki na pichu tu na sidiria. Haikupita miaka miwili akafulia mbaya.

Alivyofulia akapotea bila kujua kaenda wapi. Akaja kuibuka baada ya miaka kadhaa. Siku anakuja home kanawiri kichizi, akampa bi mkubwa (mama angu mimi) busness kadi yake ambayo inaonesha yeye ni engeneer na anamiliki kampuni ya ujenzi wa barabara (anko aliishia la saba)

Sasa hivi ameshaoa na ana life zuri tu. Ukimpigia simu story zake ni either yupo njiani anaenda makao makuu Dodoma au yupo njiani anatoka kule. Ukimpigia simu asipopokea, badae akikuchek utaskia alikuwa kwenye kikao na Mama ndio maana hakupokea (hapo anamaanisha mama Salma Kikwete)

Mara ya mwisho kumpigia simu aliniambia "Ngoja naingia Usalama, ntakuchek badae, siunajua ofisi za watu hizi"

Mungu akupe maisha marefu anko.
Hii stori ya uncle unafurahisha sana aisee🤣🤣
 
Nikiwa nimemaliza chuo sina hili wala lile, niko kitaa nikijipanga, nikachangiwa na ndugu zangu mtaji wa milion 4 point something huko, niende nikafanye biashara ya mchele toka Moro vijijini kuleta mijini na kusambaza kwa bei ya jumla.

Biashara mwanzo ilienda vizuri, mwisho wateja wangu wa siku zote wakawa wakopaji wangu wakubwa, malipo yakawa ya kuzungushana, nikawa mkali kidogo ila kwa bahati mbaya pesa ikawa ndogo kwenye mzunguko wangu, sinunui tena zile kilo nilizoanza nazo kwa wakati, mambo yakawa tofauti kidogo, nikaenda weee.

Mwisho wa siku nikachanganyiwa mchele kipuuzi kabisa na mtu ambae nilikua namuamini, nikajikuta nipo na mchele wa vitumbua na jamaa yule kakimbia, hapo ndio ukawa mwisho wangu, nilifilisika kama kuku, ndugu zangu hawakunielewa tena, nilipata stress kama tani 7 hivi.

Wakati tena nikapataga milion 3 kwa enzi zile haikua haba aisee, nikawa naishi vizuri tu, hizo elf 10 kwangu zilikua buku, sina cha kujibania kwa kweli, kuja kustuka nimenunua friji na tv tu vya geto tena ka friji kale kadogoo kabisaa, hela yotee imeisha katika njia zisizoeleweka, nilichanganyikiwa tena, sina nidhamu ya fedha.

Mwisho nikarudi zangu kusoma tena chuo ndio nikaja kutoboa kwa njia zingine kabisa kwa kutumia kazi niliyosomea.

Je, wewe unakumbuka vipi? Nini kilikupata?

Nimeufuatilia mjadala kwa ukaribu sana. Na kwa hakika haya ndiyo niliyojifunza.

1. Ukipata pesa bila kuwa na plan, ni ngumu sana kuitumia vyema.

2. Kuna uhusiano wa moja kwa moja Kati ya Pombe, Wanawake, Kampani mbovu na Starehe zingine katika kuua mafanikio ya kifedha. Kwa upande wa Wanawake kuna kitu kinaitwa "SEXUAL TRANSMITTED DEMONS" ambazo huweza kuharibu mipango ya mafanikio kwa asilimia kubwa.

3. Elimu ya kifedha ni muhimu sana Kwa kila mtu bila kujali level ya elimu,jinsia ama Umri.

3. Budget inapoheshimiwa na kufuatwa huweza kuzuia mianya ya upotevu wa pesa zisizo kwenye matumizi.

4. Unapoipata pesa jitahidi uiamrishe na siyo kukuamrisha.


5. Tunajifunza kutokana na makosa, usipoanguka huwezi kujifunza.

6. Kuna uwezekekano mkubwa wa mtu aliyefirisika kurudi katika hali yake ya zamani au hata zaidi ya Hapo, kwani nidhamu, kujiamini, maarifa, uthubutu na ukomavu huwa ni mkubwa sana.

7. Ni vyema kumshirikisha MUNGU katika mipango yetu ya kifedha ili atupe uwezo wa kuitumia vyema kwa manufaa bora zaidi.

Na mwisho niwatakie mafanikio mema wale wote walioamua kuanza upya, kwani uwezo wa kuinuka tena Upo. Lakini kwa ambao hawajawahi kufirisika wasiwaone waliofirisika kuwa ni wazembe ama hawana nidhamu. La hasha. Haya maisha ni fumbo. Hivyo badala ya kuwadharau kaa chini UJIFUNZE ili usije ukarudia makosa.

Asanteni.
 
Nimesoma page zote 88 za huu uzi,na sababu ya kunifanya nisome uzi huu ni kwa sababu na mimi ni katika wana wapotevu.

Kufulia ama kufilisika ni jambo hatari sana na kama ni mwepesi unaweza kujiua.

katika upotevu wangu na huu uzi nimejifunza mambo makuu yafuatayo.

1.ukiwa huna hela njaa huja mara kwa mara.,ukiwa una hela ya kutosha kula unajilazimisha unajikuta pesa ndio inakufanya uwe full all the time.

2. Ili ujue kama msoto uliopitia umekufunza kitu basi kipimo kiwe baada ya kuzipata tena pesa ndio utaona kama umejifunza au laa.
Kila mtu life likimpiga atajidai amejifunza ila true measure ni pale utakapopata tena fursa ndio utaona.

3.Tatizo sio kuwa na uthubutu wa kula na mipango kabla ya pesa bali tatizo ni kufuata mipango uliyoipanga,wengi tukifulia tunapanga vizuri ila tukizipata hatufuati mipango,sio tatizo ni kufuata ama kutekeleza ulichopanga.

Kila mtu anajua mambo ya msingi ya kufanya pesa inapopatikana na anajua mambo gani asifanye ili pesa ilipotee,TATIZO JE UTHUBUTU WA KUFUATA NA KUFANYA ZURI NA KUACHA BAYA UPO ?

4.ukifulia kuna possibility kubwa sana kya kuinuuka zaidi ya ulivyokuwa kabla endapo tu UTAJUA WAPI ULIFELI MWANZO NA UKAREKEBISHA SABABU HIZO ZA KUFELI MWANZO.

5.kitu kikuba unaweza kujivunia ukishafilisika ni AFYA YA AKILI kwani kama haupo njema unawez kujiua na kama upo vizuri unaweza ukalidogosha tatizo lako na kuliona kama funzo na kumove on.

6.Mara nyingi sana kujifunza kwa kuexperience mwenyewe ndiko kunaufundisha mwili vizuri kuliko kujifunza kwa kusimuliwa,hakuna mtu hajawahi kusikia kwamba starehe zinamaliza pesa,ila cha ajabu tukipata pes atunarudi huko hata kama tunajua yaani alimradi tujifunze kwa experience wenyewe.
 
Nimesoma page zote 88 za huu uzi,na sababu ya kunifanya nisome uzi huu ni kwa sababu na mimi ni katika wana wapotevu.

Kufulia ama kufilisika ni jambo hatari sana na kama ni mwepesi unaweza kujiua.

katika upotevu wangu na huu uzi nimejifunza mambo makuu yafuatayo.

1.ukiwa huna hela njaa huja mara kwa mara.,ukiwa una hela ya kutosha kula unajilazimisha unajikuta pesa ndio inakufanya uwe full all the time.

2. Ili ujue kama msoto uliopitia umekufunza kitu basi kipimo kiwe baada ya kuzipata tena pesa ndio utaona kama umejifunza au laa.
Kila mtu life likimpiga atajidai amejifunza ila true measure ni pale utakapopata tena fursa ndio utaona.

3.Tatizo sio kuwa na uthubutu wa kula na mipango kabla ya pesa bali tatizo ni kufuata mipango uliyoipanga,wengi tukifulia tunapanga vizuri ila tukizipata hatufuati mipango,sio tatizo ni kufuata ama kutekeleza ulichopanga.

Kila mtu anajua mambo ya msingi ya kufanya pesa inapopatikana na anajua mambo gani asifanye ili pesa ilipotee,TATIZO JE UTHUBUTU WA KUFUATA NA KUFANYA ZURI NA KUACHA BAYA UPO ?

4.ukifulia kuna possibility kubwa sana kya kuinuuka zaidi ya ulivyokuwa kabla endapo tu UTAJUA WAPI ULIFELI MWANZO NA UKAREKEBISHA SABABU HIZO ZA KUFELI MWANZO.

5.kitu kikuba unaweza kujivunia ukishafilisika ni AFYA YA AKILI kwani kama haupo njema unawez kujiua na kama upo vizuri unaweza ukalidogosha tatizo lako na kuliona kama funzo na kumove on.

6.Mara nyingi sana kujifunza kwa kuexperience mwenyewe ndiko kunaufundisha mwili vizuri kuliko kujifunza kwa kusimuliwa,hakuna mtu hajawahi kusikia kwamba starehe zinamaliza pesa,ila cha ajabu tukipata pes atunarudi huko hata kama tunajua yaani alimradi tujifunze kwa experience wenyewe.
Mwana mpotevu mwingine nipo hapa
 
Back
Top Bottom