Tulioshuhudia vita ya wahujumu uchumi iliyosimamiwa na Sokoine tunauona uungwana wa Rais Magufuli kuwapa fursa ya toba

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,947
141,922
Kiukweli sisi wahenga tunakumbuka vizuri vita ya wahujumu uchumi miaka ile ya 1980s iliyosimamiwa na Waziri mkuu wa wakati ule rip Edward Moringe Sokoine.

Vita ile ilisomba wengi na kwa kuwa hapakuwepo fursa kama hii iliyotolewa na Rais Magufuli watuhumiwa wengi walikaa gerezani kwa muda mrefu na wengine kuonekana hawana hatia baada ya kuwa wamesota sana rumande.

Msamaha wa Rais Magufuli utasaidia kuwaondoa wakosaji wengi kwani watatubu na kurejesha fedha na wao kuachiwa.
Hii maana yake ni kuwa kesi za ufisadi zitapungua sana na wale wachache wanaoamini wameonewa hivyo hawajatubu kesi zao zitasikilizwa kwa haraka na watapata haki yao

Kwa mara ya kwanza Tanzania tunafaidi matunda ya kuongozwa na Rais ambaye ni mwanasayansi

Maendeleo hayana vyama!
 
Nonsense, tueleze ni utawala wa nani Lisu alimiminiwa risasi? nani anawapoteza watu baharini, nani anawateka watu? Nani anawafungulia kesi wapinzani and many many other atrocities! Uungwana uko wapi. Stop that rubbish!
Kwani Chacha alipataje ajali?

Kwanini Zitto alipoachana na Chadema aliwaambia hamuwezi kumchachawangwe?

Usikariri bwashee mara nyingi kikulacho.......!
 
Hiviii leo sheria za Nchi zimebadilika? kwamba Rais anatoa msamaha kwa watuhumiwa na sio wafungwa??. Kwamba majaji sasa na majengo yetu hayana kazi tena??, maaana kazi zao zinaamliwa na muhimili mwinngine??. Twafaaaaaaaa\a
 
C alisema alitoa kama ushauri au mapendekezo wakili ili wasamehewe kama dpp na mahakama watakubali????
Hiviii leo sheria za Nchi zimebadilika? kwamba Rais anatoa msamaha kwa watuhumiwa na sio wafungwa??. Kwamba majaji sasa na majengo yetu hayana kazi tena??, maaana kazi zao zinaamliwa na muhimili mwinngine??. Twafaaaaaaaa\a
 
Nonsense, tueleze ni utawala wa nani Lisu alimiminiwa risasi? nani anawapoteza watu baharini, nani anawateka watu? Nani anawafungulia kesi wapinzani and many many other atrocities! Uungwana uko wapi. Stop that rubbish!
Kuna utawala wa nani mwandishi wa habari alipigwa kwa bomu la machozi tumboni? Utawala gani kiongozi wa mgomo wa madr alitekwa? Tuondolee siasa hapa.
 
Kwani tulishawahi kuwa na utawala tofauti na Nyinyiemu? Kwa hiyo hayo yote ni matokeo ya utawala wa hicho chama
Kuna utawala wa nani mwandishi wa habari alipigwa kwa bomu la machozi tumboni? Utawala gani kiongozi wa mgomo wa madr alitekwa? Tuondolee siasa hapa.
 
Sokoine na kinachoitwa uhujumu uchumi.
Kwa Ufupi Wakati huo miaka ya1977-82 Watawala walisha shindwa kuingoza nchi ki siasa na kiuchumi.
Kila kitu kinaendeshawa na serikali kuanzia
Chakula
Sukari
Mafuta ya gari
Ununuzi wa magari
Mabenki
Bima
Viwanda vyote
Mashamba ya Mkonge , Pamba, Tumbaku, Korosho
Uzalishaji chakula nk nk nk

Uhujumu wa uchumi ulifanywa na Watawala kuanzia Nyerere , Sokoine na kundi lao. Nchi ilikauka haina chakula na huku tukawa tunapigana bita na Uganda kwa sababu za kidini.

Wananchi walikua hawana chochote wapo fukara . Kwanza wakaanza kubadilisha Sarafu na Raia wakanyanganywa akiba zao.

Baada ya hapo ndio ikaja kinachoitwa uhujumu uchumi wa Sokoine.

Zoezi jili lengo lake lilikua ni muendelezo wa unyanganyi wa awamu ya kwanza na pia kama njia ya kuhamishia kufeli kwao kuindesha nchi kwa Raia hasa wa Kiasia na Kiarabu.

Wakanyanganya watu wana sabuni za kutoka kenya na nlue band.

Badala ya ku deal na viongozi walio yafilisi mashirika na mashamba ya umma wakawa wanakamata dawa za colgate za Wahindi.

Sokoine na Nyerere wote walifanya dhulma tu baada ya kushindwa na Watanzania wengi wakapigwa na propaganda za Radio Tanzania na chakubanga . Adui mkubwa wa uchumi wakayi huo ni Nyerere , Sokoine na kundi lao .

Haya ya sasa ni muendelezo wa dhulma kutoka kwa wanao jiita wafuasi wa Nyerere.

Na tuliona Dhulma hulipwa hapa hapa duniani...
 
Kiukweli sisi wahenga tunakumbuka vizuri vita ya wahujumu uchumi miaka ile ya 1980s iliyosimamiwa na Waziri mkuu wa wakati ule rip Edward Moringe Sokoine.

Vita ile ilisomba wengi na kwa kuwa hapakuwepo fursa kama hii iliyotolewa na Rais Magufuli watuhumiwa wengi walikaa gerezani kwa muda mrefu na wengine kuonekana hawana hatia baada ya kuwa wamesota sana rumande.

Msamaha wa Rais Magufuli utasaidia kuwaondoa wakosaji wengi kwani watatubu na kurejesha fedha na wao kuachiwa.
Hii maana yake ni kuwa kesi za ufisadi zitapungua sana na wale wachache wanaoamini wameonewa hivyo hawajatubu kesi zao zitasikilizwa kwa haraka na watapata haki yao

Kwa mara ya kwanza Tanzania tunafaidi matunda ya kuongozwa na Rais ambaye ni mwanasayansi

Maendeleo hayana vyama!
Hivi kesi zimesikilizwa lini hadi muwahukumu watu?
 
Kiukweli sisi wahenga tunakumbuka vizuri vita ya wahujumu uchumi miaka ile ya 1980s iliyosimamiwa na Waziri mkuu wa wakati ule rip Edward Moringe Sokoine.

Vita ile ilisomba wengi na kwa kuwa hapakuwepo fursa kama hii iliyotolewa na Rais Magufuli watuhumiwa wengi walikaa gerezani kwa muda mrefu na wengine kuonekana hawana hatia baada ya kuwa wamesota sana rumande.

Msamaha wa Rais Magufuli utasaidia kuwaondoa wakosaji wengi kwani watatubu na kurejesha fedha na wao kuachiwa.
Hii maana yake ni kuwa kesi za ufisadi zitapungua sana na wale wachache wanaoamini wameonewa hivyo hawajatubu kesi zao zitasikilizwa kwa haraka na watapata haki yao

Kwa mara ya kwanza Tanzania tunafaidi matunda ya kuongozwa na Rais ambaye ni mwanasayansi

Maendeleo hayana vyama!

Sasa muhenga Role ya Mahakama hapa unaionaje?
 
Back
Top Bottom