ndege JOHN
JF-Expert Member
- Aug 5, 2015
- 20,509
- 47,766
Alipita mkapa nilikuwa sijanenepa,akaja kikwete na yeye katika enzi yake sikuwahi kunenepa,lakini toka Magufuli ashike nchi naona nazidi tu kunenepa na ngozi inazidi kunawiri.ila sio ule unene wa kutisha ambao watu wanaulalamikia Ni unene wa afya na usisahau shavu limetoka kwa mbali.kimsingi Sina stress zozote Kodi ya chumba nalipa kwa wakati na sidaiwi na mtu.nakula ninachokitaka na napata muda wa kutosha wa mazoezi na wa ibada.Kama Ni mawazo niliyonayo Basi Ni kuhusu TU kifo ndo kitu nachokifikiria yaani nitakufaje lini na wapi na roho yangu itarudi vipi kwa muumba.hayo ndo mawazo niliyonayo sana yanayoniumiza kwani ningetamani Sana kuishi milele Ila ndo hivo kila kukicha siku ya kufa inakaribia lakini siwazi Sana kuhusu maisha hakuna hofu yoyote nashangaa mnaomlalamikia Magufuli wakati ipo wazi kabisa yajayo yanafurahisha na Mambo yote yanazidi kutengemana.