Tuliolelewa na watu ambao sio wazazi wetu ila wakatundea Mema Tukutane Hapa

Mkulima na Mfugaji

JF-Expert Member
Jul 26, 2013
1,013
1,635
Habar wana jamvi ,leo naomba tutoe ushuhuda kwa wale ambao tumelewa na watu ambao sio wazazi wetu mfano Baba mdogo, Mama mdogo, Shangazi, mjomba, mama wa kambo nk ila wakatundea mema

Mimi baada ya mama yangu wa kambo kunitendea yasiyo mema ila siwezi kuýataja hapa, baada ya mama yangu mzazi kufariki nikiwa mdogo, Mke wa baba yangu mdogo alimshawishi mumewe yaani baba yangu mdogo wanichukue niishi nao, baba yangu mdogo akanichukua kutoka kwa baba yangu mzazi nikawa naishi nao, Yule mama Mungu ambariki sana, alinilea kwa upendo mpaka watu wageni na mimi walijua yule ndio mama yangu Mzazi na yule baba mdogo ndio baba yangu mzazi, ingawa Mapungufu ya kibinadamu yalikuwepo kwani huwezi kupata haki sawa na watoto aliowazaa yeye, ila mimi mapungufu yale niliyaona ni mambo yakawaida, hata kwa watoto wako mwenyewe lazima tofauti ya upendo iwepo,
Mpaka nakumbuka kuna kipindi nilipata changamoto za kimaisha, nilikua napokea simu kutòka kwa yule mama, "Baba nimekutumia kiasi kidogo wanunulie sukari wajukuu zangu, "ukija ukipeleleza unagundua kwamba aliuza sehemu ya mavuno ndio akakutumia hiyo hela, baada ya muda utasikia simu yake "Baba nenda stendi na usubiri basi fulani kuna mzigo nimekutumia "ukienda pokea unakuta vyakula vya kutosha.
Kwa sasa yule mama namchukulia ndio mama yangu mzazi kwani mama yangu alifariki nikiwa mdogo, shida yake najitahidi nianze kuitatua mimi kabla ya watoto wake.
Naomba Mungu anipe Riziki zaidi na atupe maisha marefu ili aenjoy upendo wangu
 
Una moyo mwema. Una moyo wa shukrani. Unakumbuka mema uliyotendewa. Wewe ni binadamu!

Mungu Atakufanikisha mkuu ili uweze kuurudisha huo wema japo kwa kiasi kidogo. Na Mungu Amweke hai huyo mama ili auone mkono wa Bwana na wema wake kupitia kwako

Wema hauozi ati!
 
Una moyo mwema. Una moyo wa shukrani. Unakumbuka mema uliyotendewa. Wewe ni binadamu!

Mungu Atakufanikisha mkuu ili uweze kuurudisha huo wema japo kwa kiasi kidogo. Na Mungu Amweke hai huyo mama ili auone mkono wa Bwana na wema wake kupitia kwako

Wema hauozi ati!
Yule mama ndio kila kitu kwangu kwa sasa
 
Habar wana jamvi ,leo naomba tutoe ushuhuda kwa wale ambao tumelewa na watu ambao sio wazazi wetu mfano Baba mdogo, Mama mdogo, Shangazi, mjomba, mama wa kambo nk ila wakatundea mema

Mimi baada ya mama yangu wa kambo kunitendea yasiyo mema ila siwezi kuýataja hapa, baada ya mama yangu mzazi kufariki nikiwa mdogo, Mke wa baba yangu mdogo alimshawishi mumewe yaani baba yangu mdogo wanichukue niishi nao, baba yangu mdogo akanichukua kutoka kwa baba yangu mzazi nikawa naishi nao, Yule mama Mungu ambariki sana, alinilea kwa upendo mpaka watu wageni na mimi walijua yule ndio mama yangu Mzazi na yule baba mdogo ndio baba yangu mzazi, ingawa Mapungufu ya kibinadamu yalikuwepo kwani huwezi kupata haki sawa na watoto aliowazaa yeye, ila mimi mapungufu yale niliyaona ni mambo yakawaida, hata kwa watoto wako mwenyewe lazima tofauti ya upendo iwepo,
Mpaka nakumbuka kuna kipindi nilipata changamoto za kimaisha, nilikua napokea simu kutòka kwa yule mama, "Baba nimekutumia kiasi kidogo wanunulie sukari wajukuu zangu, "ukija ukipeleleza unagundua kwamba aliuza sehemu ya mavuno ndio akakutumia hiyo hela, baada ya muda utasikia simu yake "Baba nenda stendi na usubiri basi fulani kuna mzigo nimekutumia "ukienda pokea unakuta vyakula vya kutosha.
Kwa sasa yule mama namchukulia ndio mama yangu mzazi kwani mama yangu alifariki nikiwa mdogo, shida yake najitahidi nianze kuitatua mimi kabla ya watoto wake.
Naomba Mungu anipe Riziki zaidi na atupe maisha marefu ili aenjoy upendo wangu
Kuna Mke mwenza wa Mama mdogo niliishi kwake mwaka mmoja hakika alinibariki sana, ninamkumbuka na nitaendelea kumkumbuka sana maana alikuwa HAKI bin HAKI, yani akigawa majukumu ni kwa Watoto wake na kwangu bila upendeleo.

Tena ikitokea mtoto wake hajatekeleza sawa na mimi wote ni adhabu sawa, halikadhalika akigawa chochote kama zawadi au pongezi hata kama haupo lazima utapata sawa sawa na walivyopata wengine.

Na ikitokea akahisi au kushuhudia dalili zozote za ubaguzi wa mtoto wake yeyote juu yangu mimi, alikuwa hakopeshi kumkanya papo kwa hapo tena mbele ya Watoto wake akiwasisitizia dunia ni duara.

Ikimpendeza Mungu namwomba amjalie maisha marefu yule Mama na afanikiwe zaidi ya kufanikiwa, Amina.

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Kuna Mke mwenza wa Mama mdogo niliishi kwake mwaka mmoja hakika alinibariki sana, ninamkumbuka na nitaendelea kumkumbuka sana maana alikuwa HAKI bin HAKI, yani akigawa majukumu ni kwa Watoto wake na kwangu bila upendeleo.

Tena ikitokea mtoto wake hajatekeleza sawa na mimi wote ni adhabu sawa, halikadhalika akigawa chochote kama zawadi au pongezi hata kama haupo lazima utapata sawa sawa na walivyopata wengine.

Na ikitokea akahisi au kushuhudia dalili zozote za ubaguzi wa mtoto wake yeyote juu yangu mimi, alikuwa hakopeshi kumkanya papo kwa hapo tena mbele ya Watoto wake akiwasisitizia dunia ni duara.

Ikimpendeza Mungu namwomba amjalie maisha marefu yule Mama na afanikiwe zaidi ya kufanikiwa, Amina.

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
Ni wachache sana wenye moyo huo
 
Mimi ntamkumbuka milele mama yangu mdogo. Hakuwahi kupata mtoto wa kiume lakn mimi nilikua kama huyo mwanae wa kiume. Alinipenda kwelikweli. Mara zote nkienda kwake alikua lazma apike chai ya maziwa ili tunywe mimi na yeye tu tukiwa tunapiga stori. Alikua anaiita "sotu".
She was my confidant, na mtu nilieamini upendo wake haukua na rabsha
Mungu amlaze mahala pema huko aliko. Ntampenda milele
 
Ebhana muandishi umegusa jambo la muhimu sana unajua kupata mlezi au mtu alie jitoa kwako hasa kipindi ukiwa unahitaji watu kama wazazi dah ni jambo la faraja.

Mimi sikubahatika kulelewa na watu wa pembeni au ndugu kwakua baba na mama wapo ila katika kipindi fulani maishani mwangu kuna mjomba wangu alitokea kupita vyema sana kwenye maisha yangu kwanza yeye ndio alikua mtu mzima wa makamo ila hakuwa na mtoto na kazaliwa yeye na mama tu hivyo aliona mimi ni kama mwanae.
Kiufupi hakutaka nipate tabu namshukuru sana Alinionyesha njia nyingi sana toka nikiwa mtoto mpka miaka ya hivi karibuni.

Niliumia sana nilipopewa taarifa kwamba kafariki kwa covid 2020. Ila nakiri kwamba duniani watu wema bado wapo na hawakai wanapita kama upepo

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Mimi pia nimepitia hali kama yako na nawashukuru sana walionilea na kufikia hapa nilipo na huwa mara kwa mara nawalipa fadhila kwani bila wao nisingekuwa hapa wana mchango mkubwa sana na kwangu Mungu awabariki sana
 
Kuna Mke mwenza wa Mama mdogo niliishi kwake mwaka mmoja hakika alinibariki sana, ninamkumbuka na nitaendelea kumkumbuka sana maana alikuwa HAKI bin HAKI, yani akigawa majukumu ni kwa Watoto wake na kwangu bila upendeleo.

Tena ikitokea mtoto wake hajatekeleza sawa na mimi wote ni adhabu sawa, halikadhalika akigawa chochote kama zawadi au pongezi hata kama haupo lazima utapata sawa sawa na walivyopata wengine.

Na ikitokea akahisi au kushuhudia dalili zozote za ubaguzi wa mtoto wake yeyote juu yangu mimi, alikuwa hakopeshi kumkanya papo kwa hapo tena mbele ya Watoto wake akiwasisitizia dunia ni duara.

Ikimpendeza Mungu namwomba amjalie maisha marefu yule Mama na afanikiwe zaidi ya kufanikiwa, Amina.

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
Mbona tumeambiwa watu wazuri hawafi?
 
Mimi pia nimepitia hali kama yako na nawashukuru sana walionilea na kufikia hapa nilipo na huwa mara kwa mara nawalipa fadhila kwani bila wao nisingekuwa hapa wana mchango mkubwa sana na kwangu Mungu awabariki sana
Kwa kweli tuwape heshima yao
 
Watu wema kwangu nimewapoteza wote

Mmoja mwaka Jana na Bahati mbaya mazishi yake sikushiriki kutokana na I misuko suko ya dunia hii ila daima

Mwingne nimempoteza mwaka huu huyu nimeshiriki kuanzia kuumwa mpaka kuzika

Ila huwa naishia kusema mungu hutupa nafasi Fulani katika maisha ya watu kwa sababu Fulani

Siwez kulipa wema wao ila yanipasa kutenda wema kwa watu wengne

Maana hawapo tena

Mungu azilaze roho zao mahali pema peponi

AMEN
 
shangazi yangu alinilea kama binti yake,hakujaaliwa mtoto wa kike nami nikawa binti yake wa pekee,hii nayo imekuwa ni changamoto make sina strong bond na mama yangu ko nachofanya nabalance huku na huku

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu wema kwangu nimewapoteza wote

Mmoja mwaka Jana na Bahati mbaya mazishi yake sikushiriki kutokana na I misuko suko ya dunia hii ila daima

Mwingne nimempoteza mwaka huu huyu nimeshiriki kuanzia kuumwa mpaka kuzika

Ila huwa naishia kusema mungu hutupa nafasi Fulani katika maisha ya watu kwa sababu Fulani

Siwez kulipa wema wao ila yanipasa kutenda wema kwa watu wengne

Maana hawapo tena

Mungu azilaze roho zao mahali pema peponi

AMEN
Ameen
 
Mimi hapa ni mmoja wao. Nimekulia kwa dada. Shem kanilea toka darsa la kwanza mpk leo. Namuitaga mzee. Nini cha shule niskipate. Baba mzazi alikuwepo ila sasa kafariki huyu shem wangu alimuomba mzee niishi naye. Kanilea kanifundsha kilimo, uanaume, kazi na mambo mengine. Ana watoto wa kike wako sekondari ila mimi ni wa kiume so anaonaga me ndio jembe.

Nimeanza life langu binafsi lakn utakuta ananiagizia chakula kwa basi na Makorokoro kibao.

I love him. Yuko kwenye mid 50s. Vitu vingi vya maendeleo ananambia vzr. Kbla sijapata kazi mwaka huu nimemaliza chuo yeye ni mfariji hakuniona kama mzigo lkn pia me nilikuwa najongeza kufanya kazi za home sijawahi leta uhuni wwte au kuleta kesi. Kanipa eneo kubwa nikajiongeza nikachoma mkaa.

Darsani sikuwahi kumuangusha.

Ninaongea nae kwenye simu mara kwa mara. Sometimes utakuta kapiga tu afu haongei najua huyu kanimiss baadaye utakuta ananipa taarfa za pale home anafanya nini. Tunacheka nk.

Niombeeni siku nimuanzishie uzi humu.
 
Back
Top Bottom