GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,571
- 108,922
Ikiwa leo ni Kumbukumbu ya ' Mtaalam ' wa Sanaa za ' Mapigano ' duniani ( Martial Arts ) Hayati Bruce Lee naomba wale wenzangu na Mie ambao tulikuwa tukipenda mno Kuziangalia, Kuiga na kwenda Kuwaonea Wenzetu mitaani na tukawa tunapata ' mirejesho ' ya Kupigwa / Vipigo tujitokeze ili ikibidi tuweze Kujiona jinsi tulivyokuwa Mangumbaru na Mapopoma kipindi hicho.
Binafsi nakumbuka nilikuwa nikipenda sana Kuziangalia na kwenda Kuwaonea ' Madogo ' wenzangu ' Mitaani ' na hata Watu wazima ( akina Kaka )ambao nilikuwa naona nawamudu na hasa kwa ' Mikwara ' yangu iliyotukuka ila kuna Siku moja ' niliyakanyaga ' na mpaka leo sisahau kwa nilichokipata.
Nakumbuka kuna Siku moja nikiwa mitaa fulani kwa Mkubwa mmoja ambaye Kipindi hicho alikuwa akilindwa na Wana Medani Waliotukuka ( Wanajeshi / Wajeda ) hivyo kwa Kujiamini na Sinema za Bruce Lee ambazo nilikuwa naziangalia mara kwa mara na ' Kumuiga ' katika tembea tembea yangu tena nikiwa na Mbwa wangu nikamkuta huyo Mjeda anakojoa pembeni hivi mwa barabara nikaanza kumpiga ' Mkwara ' kama kawaida yangu huku nikilia kama Bruce Lee na ile Sauti yake, mara nikiipindisha Mikono yangu na Miguu utadhani Helikopta ya Polisi inataka Kupaa yaani yote ni ' Minjonjo ' tu ili Jamaa aogope na nijione mbabe nilikuja kupokea Ngumi moja hiyo ' takatifu ' na ' tukuka ' ambayo sidhani hata akina Tyson au Cheka wanaijua inaitwaje ambayo iliniingia kisawasawa na kilichofuata hapo nilikubaliana na yule Mbwa wangu niliyekuwa nae kuwa tugawane zetu tu njia za kurudi Nyumbani japo Yeye ( yule Mbwa ) wakati ' nakandamizwa ' na lile ' Konde ' zito la Kimedani / Kijeshi alikuwa tayari ameshaianza safari yake ya Kunitangulia kurudi Nyumbani.
Ile ngumi hadi leo naikumbuka na kila nikikutana na hawa Mabondia nikiwaelezea na kuwauliza inaitwaje jibu wanalonipa tu ni kwamba ina ' Ngumi ya Kifo ' na kwamba kama ningechelewa au kuzidi kuwepo eneo lile la tukio na yule Mjeda basi kulikuwa na uwezekano mkubwa ile Siku maturubai ya Msiba yangetawala Nyumbani Kwetu.
Ndiyo maana hadi leo hii nikikuta tu Ugomvi wowote ( kwakuwa napenda sana Ugomvi ) ila nikaambiwa anayeuratibu / anayeusimamia ni Mwana Medani / Mwanajeshi Mimi huwa mpole mara moja na ikibidi huwa naanza kuziulizia mapema mno njia za Uchochoro ili ' Kikinuka ' tu basi tuanze kumwambia Mwanariadha Usain Bolt kuwa hata huku Tanzania Vipaji vya Kutoka Nduki ( Kukimbia ) mita 100 vipo lukuki tu sema bado hatujaonekana.
Hivi Wajeda / Wanajeshi zile ngumi zao nani huwa anawafundisha? Na kwanini hata akikupiga huwa zinauma hata kwa miaka 15 hadi 25 ya maisha yako yote? Haya Vijana wa sasa hivi mnaopenda sijui Kuwaangalia akina Vad Damme na Jackie Chan ole Wenu siku mkosee mkajaribu ' Kuziigiza ' kwa Wajeda ndipo mtajua kwanini hata Mimi GENTAMYCINE nawaogopa japo wengi wao ni Marafiki zangu wakubwa na wazuri tu huku hadi Ndugu zangu baadhi nao wakiwa huko ila ' nawaheshimu ' kuliko Kitu kingine chochote kile.
R.I.P Bruce Lee
Nawasilisha.
Binafsi nakumbuka nilikuwa nikipenda sana Kuziangalia na kwenda Kuwaonea ' Madogo ' wenzangu ' Mitaani ' na hata Watu wazima ( akina Kaka )ambao nilikuwa naona nawamudu na hasa kwa ' Mikwara ' yangu iliyotukuka ila kuna Siku moja ' niliyakanyaga ' na mpaka leo sisahau kwa nilichokipata.
Nakumbuka kuna Siku moja nikiwa mitaa fulani kwa Mkubwa mmoja ambaye Kipindi hicho alikuwa akilindwa na Wana Medani Waliotukuka ( Wanajeshi / Wajeda ) hivyo kwa Kujiamini na Sinema za Bruce Lee ambazo nilikuwa naziangalia mara kwa mara na ' Kumuiga ' katika tembea tembea yangu tena nikiwa na Mbwa wangu nikamkuta huyo Mjeda anakojoa pembeni hivi mwa barabara nikaanza kumpiga ' Mkwara ' kama kawaida yangu huku nikilia kama Bruce Lee na ile Sauti yake, mara nikiipindisha Mikono yangu na Miguu utadhani Helikopta ya Polisi inataka Kupaa yaani yote ni ' Minjonjo ' tu ili Jamaa aogope na nijione mbabe nilikuja kupokea Ngumi moja hiyo ' takatifu ' na ' tukuka ' ambayo sidhani hata akina Tyson au Cheka wanaijua inaitwaje ambayo iliniingia kisawasawa na kilichofuata hapo nilikubaliana na yule Mbwa wangu niliyekuwa nae kuwa tugawane zetu tu njia za kurudi Nyumbani japo Yeye ( yule Mbwa ) wakati ' nakandamizwa ' na lile ' Konde ' zito la Kimedani / Kijeshi alikuwa tayari ameshaianza safari yake ya Kunitangulia kurudi Nyumbani.
Ile ngumi hadi leo naikumbuka na kila nikikutana na hawa Mabondia nikiwaelezea na kuwauliza inaitwaje jibu wanalonipa tu ni kwamba ina ' Ngumi ya Kifo ' na kwamba kama ningechelewa au kuzidi kuwepo eneo lile la tukio na yule Mjeda basi kulikuwa na uwezekano mkubwa ile Siku maturubai ya Msiba yangetawala Nyumbani Kwetu.
Ndiyo maana hadi leo hii nikikuta tu Ugomvi wowote ( kwakuwa napenda sana Ugomvi ) ila nikaambiwa anayeuratibu / anayeusimamia ni Mwana Medani / Mwanajeshi Mimi huwa mpole mara moja na ikibidi huwa naanza kuziulizia mapema mno njia za Uchochoro ili ' Kikinuka ' tu basi tuanze kumwambia Mwanariadha Usain Bolt kuwa hata huku Tanzania Vipaji vya Kutoka Nduki ( Kukimbia ) mita 100 vipo lukuki tu sema bado hatujaonekana.
Hivi Wajeda / Wanajeshi zile ngumi zao nani huwa anawafundisha? Na kwanini hata akikupiga huwa zinauma hata kwa miaka 15 hadi 25 ya maisha yako yote? Haya Vijana wa sasa hivi mnaopenda sijui Kuwaangalia akina Vad Damme na Jackie Chan ole Wenu siku mkosee mkajaribu ' Kuziigiza ' kwa Wajeda ndipo mtajua kwanini hata Mimi GENTAMYCINE nawaogopa japo wengi wao ni Marafiki zangu wakubwa na wazuri tu huku hadi Ndugu zangu baadhi nao wakiwa huko ila ' nawaheshimu ' kuliko Kitu kingine chochote kile.
R.I.P Bruce Lee
Nawasilisha.