Wont be the same
JF-Expert Member
- Aug 15, 2024
- 1,564
- 2,483
Taasisi ya Tulia Trust Chini ya Mkurugenzi Wake ambaye ni Mbunge wa Mbeya Mjini, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani(IPU) Dkt. Tulia Ackson imewasaidia mahitaji watoto wa familia moja walioshindwa kuendelea na masomo kwa kukosa vifaa vya shule.
Tulia Trust imewasaidia vifaa vya shule ikiwa ni pamoja na daftari, begi, sare za shule, viatu pamoja na nguo za nyumbani Latifa Mengondele (12) anayesoma darasa la sita na mdogo wake Ivan Mengondele (7) aliyetakiwa kuanza masomo ya chekechea katika shule ya Msingi Hayanga iliyopo kata ya Isyesye jijini Mbeya.
Watoto hao walishindwa kuendelea na masomo kwa kukosa vifaa vya shule baada ya baba yao kufariki huku mama yao akiondoka nyumbani na kwenda kusikojulikana kabla hata ya kifo cha baba yao hivyo kwa sasa wanaishi kwenye nyumba iliyoachwa na baba yao huku wakipata msaada kutoka kwa shangazi yao ambaye hana uwezo.
Tulia Trust imewasaidia vifaa vya shule ikiwa ni pamoja na daftari, begi, sare za shule, viatu pamoja na nguo za nyumbani Latifa Mengondele (12) anayesoma darasa la sita na mdogo wake Ivan Mengondele (7) aliyetakiwa kuanza masomo ya chekechea katika shule ya Msingi Hayanga iliyopo kata ya Isyesye jijini Mbeya.
Watoto hao walishindwa kuendelea na masomo kwa kukosa vifaa vya shule baada ya baba yao kufariki huku mama yao akiondoka nyumbani na kwenda kusikojulikana kabla hata ya kifo cha baba yao hivyo kwa sasa wanaishi kwenye nyumba iliyoachwa na baba yao huku wakipata msaada kutoka kwa shangazi yao ambaye hana uwezo.