Nina ndugu yangu wa kike amebadili dini kuwa muislamu kisa kapata mwanaume wa kiislamu na ili wafunge ndoa ilimbidi abadili dini.Wale ukikubali tu unasilimishwa haraka sana. Na kama unataka mke utampata na ndoa ya kiislam kufungwa haraka sana bila kujali sherehe na shamrasha
Asante Sana Kaka...Nina ndugu yangu wa kike amebadili dini kuwa muislamu kisa kapata mwanaume wa kiislamu na ili wafunge ndoa ilimbidi abadili dini.
Huyu Binti maisha yake tangu awe muislamu haishi kiislamu. Anaecti uislamu machoni pa watu,amebadili mavazi( anavaa mabaibui na manguo ya kiislamu) ,anaswali swala 5,anafunga,ila akija home anakula kitimoto na tunasali nae sala zote za kikristo.
Mimi na huyo Binti hatuelewani maana Huwa namchana ukweli kuwa sipendi watu wanafiki wa dini(wafarisayo) wenye kufanya matendo ya kidini ili waonekane watu wa Mungu machoni pa watu kumbe Mungu anawahesabu kama makaburi yaliyonakshiwa kwa nje ila ndani yamejaa mifupa na uchafu. Na yeye hunijibu "sasa ningefanyaje wakati jamaa ana Hela na Mimi nilitaka kuolewa".
Watu wa aina hii ya sista angu wapo wengi sana,hasa Hawa wanabadili dini kirahisi kuwa waislamu(kwa sababu ni rahisi kwa mkristo kubadili dini kuwa muislamu,na ni ngumu na mara chache sana kwa muislamu kubadili kuwa mkristo). Na mara nyingi watu wa aina hiyo hufanya hivyo ili kuendana na mifumo ya mahali husika au kutafuta ndoa.
Hawa watu Huwa wanafiki sana ni watu hatari.
Nikola Tesla kama wewe uwe Mwislamu,haifai.Jana Mida ya Saa 8. Nilitoka Nje ya sehemu Yangu ya kibiashara(Ninapotafutia Ridhiki)
Kuna Watu walikua wanacheza Draft wanachangamsha Akili, Miongoni mwao alikuepo mzee mmoja ambae ni kiongozi ktk msikiti fulani.
Mara Nyingi huwa nafanya Baadhi ya Mambo ktk huo msiki ikinipendeza kufanya, na Huyo Mzee alishawishika kuniambia wanitie maji akimaanisha nisilimu, niwe muislamu.
Watu wengi wanaonizunguka na sehemu ninayofanyia bishara Ina milikiwa na mzee wa kiisilamu, shughuli Zao za kidini huwa natoa saport pale panapoitaji saport na ikiwa iko ndani ya uwezo wangu.
Kwa kuwa Huyo Mzee alinieleza Suala la kubadili Dini. Aliliongea hilo Jambo Mbele za watu wengi na waliosikia ni wengi, nilitafakari kwa muda jibu la kumpa.
Ila nilipata jibu la kumpa ambalo nilihisi litakua sahihi.
Jibu langu nilisema hivi.
"Nashukuru kwa ulichoniambia Ila Mungu ni mwingi wa rehema na rehema zake hazichunguziki, panapo majariwa ya Mungu Kama amepanga Hilo litokee litatokea Ila tuendelee kuombeana, na Naimani siku Moja Mungu atatenda lipaswalo kutenda".
Baada kua nimeongea Maneno hayo nilikaa dakika chache nikaondoka eneo Hilo.