Tukutane tuliowahi kunusurika na Kifo

Mzurulaji

JF-Expert Member
Sep 25, 2021
284
564
Habari zenu wakuu natumai mu wazima wa Afya.
Wakati tunaendelea kupambana na Uchumi wa kati.
Tujikumbushe tuliowahi kunusurika na Kifo.

Binafsi hii imenikuta mwaka juzi tu hapa. 2020.

Nilipata mualiko wa kwenda kwenye harusi ya ndugu yangu mtoto wa Mamkubwa wangu alikuwa akiolewa.

Binafsi siku hiyo sikuwa na ratiba yoyote ya kutoka lakini kwa sababu ni ndugu yangu na hilo alipingiki. Nilijiandaa kikamilifu. Na kufika eneno husika kwa shughuli hiyo. Hakukuwa mbali na napoishi, nilijongea mpaka eneo husika kwaajili ya kuifurahia shughuli ile. Ukumbuke hapo nilipokuwa nikiishi nilikuwa nimepanga hivyo hata wakati wa kuondoka niliondoka peke yangu.

Shughuli iliendelea kuwa bora na iliotaliwa na uchangamfu mpaka panapo majira ya saa nane usiku.
Wakati wa kuondoka sikuwa peke yangu nilikuwa na vijana wenzangu wengine tunaofahamiana na wote tulikutana eneo husika hii ilitufanya tusiwe na hofu kabisa. Sasa wakati tukiwa njiani kila mtu apate kuifikia nyumba anayoishi ilitubidi tugawane ili kila mtu aende zake kwa maana tulikuwa hatuishi pamoja.

Wakati nikiwa peke yangu huku yakiwa yametimia majira ya saa tisa usiku, nilifika hatua ambayo ni karibu na nyumbani nilichotakiwa kufanya ni kuvuka barabara iliotaliwa na kijigiza hafifu ili niweze kuingia ndani.

Hakika kwa hofu niliokuwa nayo kabla ya kuvuka barabara ilinibidi nitazame upande wa juu wa barabara hiyo kwa usalama wangu. Daah sikuamini macho yangu mtu nisiomfahamu alikuwa akija nilipo kwa kasi sana huku akionekana amedhamiria kunikamata. Nilianza timua mbio na kufanikiwa kufika sehemu ambayo najua nikijitosa navuka ukuta na kuingia nyumbani.

Kupitia kujitosa kule kwa kupanda ukute ule. Nilifanikiwa kuingia ndani ila wakati wa kushuka chini nilianguka vibaya sana. Nilikuja kushtuka ni majira ya saa kumi na moja nipo pale pale huku nikihisi maumivu makali kwenye kichwa changu.

Nyumbani nilifanikiwa kuwapa taarifa na huo ukawa mwisho wangu wa kutoka usiku.

Nawe tiririka na yako ndugu mwana JF. Ahsanteni pia.
 
Tena mtu mmoja na kwa uwoga nawe ukakimbia bila kujiuliza haraka huyu mtu atakuwa na dhamira gani tena jirani na nyumba uliyokuwa ukiishi maanaake wewe ni mwenyeji maeneo hayo.! What if
~ Angekuitia mwizi ungefanyaje?
~ Kama alikuwa anakimbizwa alipokuona wewe akajua amepata msaada muwe wawili kuwakabili hao waliokuwa wakimkimbiza?
 
Habari zenu wakuu natumai mu wazima wa Afya.
Wakati tunaendelea kupambana na Uchumi wa kati.
Tujikumbushe tuliowahi kunusurika na Kifo.

Binafsi hii imenikuta mwaka juzi tu hapa. 2020.

Nilipata mualiko wa kwenda kwenye harusi ya ndugu yangu mtoto wa Mamkubwa wangu alikuwa akiolewa.

Binafsi siku hiyo sikuwa na ratiba yoyote ya kutoka lakini kwa sababu ni ndugu yangu na hilo alipingiki. Nilijiandaa kikamilifu. Na kufika eneno husika kwa shughuli hiyo. Hakukuwa mbali na napoishi, nilijongea mpaka eneo husika kwaajili ya kuifurahia shughuli ile. Ukumbuke hapo nilipokuwa nikiishi nilikuwa nimepanga hivyo hata wakati wa kuondoka niliondoka peke yangu.

Shughuli iliendelea kuwa bora na iliotaliwa na uchangamfu mpaka panapo majira ya saa nane usiku.
Wakati wa kuondoka sikuwa peke yangu nilikuwa na vijana wenzangu wengine tunaofahamiana na wote tulikutana eneo husika hii ilitufanya tusiwe na hofu kabisa. Sasa wakati tukiwa njiani kila mtu apate kuifikia nyumba anayoishi ilitubidi tugawane ili kila mtu aende zake kwa maana tulikuwa hatuishi pamoja.

Wakati nikiwa peke yangu huku yakiwa yametimia majira ya saa tisa usiku, nilifika hatua ambayo ni karibu na nyumbani nilichotakiwa kufanya ni kuvuka barabara iliotaliwa na kijigiza hafifu ili niweze kuingia ndani.

Hakika kwa hofu niliokuwa nayo kabla ya kuvuka barabara ilinibidi nitazame upande wa juu wa barabara hiyo kwa usalama wangu. Daah sikuamini macho yangu mtu nisiomfahamu alikuwa akija nilipo kwa kasi sana huku akionekana amedhamiria kunikamata. Nilianza timua mbio na kufanikiwa kufika sehemu ambayo najua nikijitosa navuka ukuta na kuingia nyumbani. Kupitia kujitosa kule kwa kupanda ukute ule. Nilifanikiwa kuingia ndani ila wakati wa kushuka chini nilianguka vibaya sana. Nilikuja kushtuka ni majira ya saa kumi na moja nipo pale pale huku nikihisi maumivu makali kwenye kichwa changu.

Nyumbani nilifanikiwa kuwapa taarifa na huo ukawa mwisho wangu wa kutoka usiku.

Nawe tiririka na yako ndugu mwana JF. Ahsanteni pia.
Polee sana mkuu Mzurulaji
 
Habari zenu wakuu natumai mu wazima wa Afya.
Wakati tunaendelea kupambana na Uchumi wa kati.
Tujikumbushe tuliowahi kunusurika na Kifo.

Binafsi hii imenikuta mwaka juzi tu hapa. 2020.

Nilipata mualiko wa kwenda kwenye harusi ya ndugu yangu mtoto wa Mamkubwa wangu alikuwa akiolewa.

Binafsi siku hiyo sikuwa na ratiba yoyote ya kutoka lakini kwa sababu ni ndugu yangu na hilo alipingiki. Nilijiandaa kikamilifu. Na kufika eneno husika kwa shughuli hiyo. Hakukuwa mbali na napoishi, nilijongea mpaka eneo husika kwaajili ya kuifurahia shughuli ile. Ukumbuke hapo nilipokuwa nikiishi nilikuwa nimepanga hivyo hata wakati wa kuondoka niliondoka peke yangu.

Shughuli iliendelea kuwa bora na iliotaliwa na uchangamfu mpaka panapo majira ya saa nane usiku.
Wakati wa kuondoka sikuwa peke yangu nilikuwa na vijana wenzangu wengine tunaofahamiana na wote tulikutana eneo husika hii ilitufanya tusiwe na hofu kabisa. Sasa wakati tukiwa njiani kila mtu apate kuifikia nyumba anayoishi ilitubidi tugawane ili kila mtu aende zake kwa maana tulikuwa hatuishi pamoja.

Wakati nikiwa peke yangu huku yakiwa yametimia majira ya saa tisa usiku, nilifika hatua ambayo ni karibu na nyumbani nilichotakiwa kufanya ni kuvuka barabara iliotaliwa na kijigiza hafifu ili niweze kuingia ndani.

Hakika kwa hofu niliokuwa nayo kabla ya kuvuka barabara ilinibidi nitazame upande wa juu wa barabara hiyo kwa usalama wangu. Daah sikuamini macho yangu mtu nisiomfahamu alikuwa akija nilipo kwa kasi sana huku akionekana amedhamiria kunikamata. Nilianza timua mbio na kufanikiwa kufika sehemu ambayo najua nikijitosa navuka ukuta na kuingia nyumbani. Kupitia kujitosa kule kwa kupanda ukute ule. Nilifanikiwa kuingia ndani ila wakati wa kushuka chini nilianguka vibaya sana. Nilikuja kushtuka ni majira ya saa kumi na moja nipo pale pale huku nikihisi maumivu makali kwenye kichwa changu.

Nyumbani nilifanikiwa kuwapa taarifa na huo ukawa mwisho wangu wa kutoka usiku.

Nawe tiririka na yako ndugu mwana JF. Ahsanteni pia.
Nikiwa mtoto wa miaka 6, nikinusurik na kifo baada ya kuruka sarakasi juu angani halafu ukiwa angani unajigeuza kichwa juu miguu chin ndo unatua.

Sasa mimi sijui nilibugi step, niliruka nikaja kutulia shingo, weee, nilipoteza mawasiliano ya ulimwengu huu halisi nikaingia ulimwengu mwingine ambao huwezi kufuny maamuzi binafsi.

Mungu mwema baada ya nusu saa nikaanza kuuona ulimwengu tena halisi.
From there sijawahi kuruka hizo sarakasi, halafu nimekumbuka ngoja nimuite mwanangu nimkanye asije jaribu huu ujinga.
 
Ngoja nianze na hili kwanza nakumbuka mwaka 1994 nipo darasa la pili niliwahi kudondoka bila sababu yeyote sehemu fupi sana ila nilibilingita kwa umbali mrefu kwenda vichakani nikapoteza fahamuwatoto wenzangu kwa uoga wakakimbilia makwao bila kutoa taarifa makwao home walikaa mpaka saa nne usiku kuna braza jirani alikuwa katoka kwa demu wake ndio kama bahati akaniona akaenda kutoa taarifa home nikabebwa msobemsobe hata sina fahamu na mwili umeshakuwa bariidii kifuani tu ndio kulikuwa na joto kwa mbali na pumzi kwa mbaali sema pale home kulikuwa kunauza pombe "wanzuki" walevi wote nduki home bimkubwa akaanza kulika anajua nishakata moto zikaanza harakati za msiba kuna mzee baada ya kuona hali ile faster akakimbia kwake akaja kwa maelezo akaomba anyone akanivutisha sijui vitu gani msela chafya kama zote nikazinduka sema vitu vyote nilivyokula siku hiyo vikatoka ila baada ya hapo nikawa poa na kesho nikaenda shule.

Kisa kingine juzi tu hapa mwaka huu mwanzoni nilisafiri kikazi kwenye Kanda ya ziwa siku ya kurudi nimeshuka mitaa ya mbezi nikamuunganishia mpka home pembeni ya Jiji la makalla nimeshuka kwenye usafiri wa umma natembea kwenda home nikakutana na vijana kama wanne hivi wakaniweka mtu kati wanataka niwape kila nilichonacho wana visu na mapanga wakachukua bag ya laptop,simu na wallet kitu ambacho hawakujua kuwa nana "mkwaju" kiunoni hivyo sikuwa na haraka nao wakaniamrisha haya potea halafu wa mdogomdogo nilipopata chance kabla nikachomoa "mkwaju" nikawaamrisha kurudisha vitu vyangu vingine "bengo zetafongoka" kwa ajiri yao kajua natania nikatuma "njugu" moja kwanza hewani ile sound wote wakatulia na kwa upole kunikabidhi mali zangu baadhi ya majirani walikuwa wameshaanza kuamka akapigiwa mjumbe akakabidhiwa watu hata sijui walimalizana vipi maana mie mtu wa kusafiri ila nikajiuliza bila "mkwaju" wapuuzi wale wangeniibia huenda na kunidhuru pia
 
Mara moja katika maisha yangu nilianguka kutoka ghorofa ya tatu hadi ground level..ajabu ni kuwa sikuteuka hata kidole, ukiacha ndugu yangu wanaofahamu watu wengne huwa hawaamini
 
Tena mtu mmoja na kwa uwoga nawe ukakimbia bila kujiuliza haraka huyu mtu atakuwa na dhamira gani tena jirani na nyumba uliyokuwa ukiishi maanaake wewe ni mwenyeji maeneo hayo.! What if
~ Angekuitia mwizi ungefanyaje?
~ Kama alikuwa anakimbizwa alipokuona wewe akajua amepata msaada muwe wawili kuwakabili hao waliokuwa wakimkimbiza?
Mkuu akili ya haraka haraka hapo wewe ungefanyeje ungesimama?
 
Nikiwa mtoto wa miaka 6, nikinusurik na kifo baada ya kuruka sarakasi juu angani halafu ukiwa angani unajigeuza kichwa juu miguu chin ndo unatua.

Sasa mimi sijui nilibugi step, niliruka nikaja kutulia shingo, weee, nilipoteza mawasiliano ya ulimwengu huu halisi nikaingia ulimwengu mwingine ambao huwezi kufuny maamuzi binafsi.

Mungu mwema baada ya nusu saa nikaanza kuuona ulimwengu tena halisi.
From there sijawahi kuruka hizo sarakasi, halafu nimekumbuka ngoja nimuite mwanangu nimkanye asije jaribu huu ujinga.
Inafurahisha ulivyoelezea ila pole mkuu.
 
Ngoja nianze na hili kwanza nakumbuka mwaka 1994 nipo darasa la pili niliwahi kudondoka bila sababu yeyote sehemu fupi sana ila nilibilingita kwa umbali mrefu kwenda vichakani nikapoteza fahamuwatoto wenzangu kwa uoga wakakimbilia makwao bila kutoa taarifa makwao home walikaa mpaka saa nne usiku kuna braza jirani alikuwa katoka kwa demu wake ndio kama bahati akaniona akaenda kutoa taarifa home nikabebwa msobemsobe hata sina fahamu na mwili umeshakuwa bariidii kifuani tu ndio kulikuwa na joto kwa mbali na pumzi kwa mbaali sema pale home kulikuwa kunauza pombe "wanzuki" walevi wote nduki home bimkubwa akaanza kulika anajua nishakata moto zikaanza harakati za msiba kuna mzee baada ya kuona hali ile faster akakimbia kwake akaja kwa maelezo akaomba anyone akanivutisha sijui vitu gani msela chafya kama zote nikazinduka sema vitu vyote nilivyokula siku hiyo vikatoka ila baada ya hapo nikawa poa na kesho nikaenda shule.

Kisa kingine juzi tu hapa mwaka huu mwanzoni nilisafiri kikazi kwenye Kanda ya ziwa siku ya kurudi nimeshuka mitaa ya mbezi nikamuunganishia mpka home pembeni ya Jiji la makalla nimeshuka kwenye usafiri wa umma natembea kwenda home nikakutana na vijana kama wanne hivi wakaniweka mtu kati wanataka niwape kila nilichonacho wana visu na mapanga wakachukua bag ya laptop,simu na wallet kitu ambacho hawakujua kuwa nana "mkwaju" kiunoni hivyo sikuwa na haraka nao wakaniamrisha haya potea halafu wa mdogomdogo nilipopata chance kabla nikachomoa "mkwaju" nikawaamrisha kurudisha vitu vyangu vingine "bengo zetafongoka" kwa ajiri yao kajua natania nikatuma "njugu" moja kwanza hewani ile sound wote wakatulia na kwa upole kunikabidhi mali zangu baadhi ya majirani walikuwa wameshaanza kuamka akapigiwa mjumbe akakabidhiwa watu hata sijui walimalizana vipi maana mie mtu wa kusafiri ila nikajiuliza bila "mkwaju" wapuuzi wale wangeniibia huenda na kunidhuru pia
Hii imenifanya nitamani mkwaju ndugu. Kwaajili ya usalama wangu.
 
Mara moja katika maisha yangu nilianguka kutoka ghorofa ya tatu hadi ground level..ajabu ni kuwa sikuteuka hata kidole, ukiacha ndugu yangu wanaofahamu watu wengne huwa hawaamini
Mungu yupo pamoja nawe mkuu.
 
Ngoja nianze na hili kwanza nakumbuka mwaka 1994 nipo darasa la pili niliwahi kudondoka bila sababu yeyote sehemu fupi sana ila nilibilingita kwa umbali mrefu kwenda vichakani nikapoteza fahamuwatoto wenzangu kwa uoga wakakimbilia makwao bila kutoa taarifa makwao home walikaa mpaka saa nne usiku kuna braza jirani alikuwa katoka kwa demu wake ndio kama bahati akaniona akaenda kutoa taarifa home nikabebwa msobemsobe hata sina fahamu na mwili umeshakuwa bariidii kifuani tu ndio kulikuwa na joto kwa mbali na pumzi kwa mbaali sema pale home kulikuwa kunauza pombe "wanzuki" walevi wote nduki home bimkubwa akaanza kulika anajua nishakata moto zikaanza harakati za msiba kuna mzee baada ya kuona hali ile faster akakimbia kwake akaja kwa maelezo akaomba anyone akanivutisha sijui vitu gani msela chafya kama zote nikazinduka sema vitu vyote nilivyokula siku hiyo vikatoka ila baada ya hapo nikawa poa na kesho nikaenda shule.

Kisa kingine juzi tu hapa mwaka huu mwanzoni nilisafiri kikazi kwenye Kanda ya ziwa siku ya kurudi nimeshuka mitaa ya mbezi nikamuunganishia mpka home pembeni ya Jiji la makalla nimeshuka kwenye usafiri wa umma natembea kwenda home nikakutana na vijana kama wanne hivi wakaniweka mtu kati wanataka niwape kila nilichonacho wana visu na mapanga wakachukua bag ya laptop,simu na wallet kitu ambacho hawakujua kuwa nana "mkwaju" kiunoni hivyo sikuwa na haraka nao wakaniamrisha haya potea halafu wa mdogomdogo nilipopata chance kabla nikachomoa "mkwaju" nikawaamrisha kurudisha vitu vyangu vingine "bengo zetafongoka" kwa ajiri yao kajua natania nikatuma "njugu" moja kwanza hewani ile sound wote wakatulia na kwa upole kunikabidhi mali zangu baadhi ya majirani walikuwa wameshaanza kuamka akapigiwa mjumbe akakabidhiwa watu hata sijui walimalizana vipi maana mie mtu wa kusafiri ila nikajiuliza bila "mkwaju" wapuuzi wale wangeniibia huenda na kunidhuru pia
Mkwaju ulikuokoa mkuu...
 
Mimi nilipata ajali ya Gari likasagika lote nikachomoka,nikawahi lift ya Ndege ikaanguka baharini ikateketea nikadandia Meli ikazama,nikaruka nikazama kwenye Mdomo wa Papa bahati mbaya akaninya nikarushwa ng'ambo ya Bahari na Mawimbi,Sitaki kukumbuka nilivyonusurika ukiangalia kwa undani ni Mipango tu ya Mungu.
 
Back
Top Bottom