Jamaa_Mbishi
JF-Expert Member
- Jun 15, 2013
- 10,185
- 7,367
Mkeo kaleta wali na nyama, mgeni analazimisha kunawa na kuomba aongezewe nyama. Mnaanza kula tu, yeye anatafuta nyama kubwa kubwa huku akiongea kwa furaha kana kwamba yuko kwake na kulalamika kuwa chakula ni kidogo hamta shiba huku akimuita mkeo. Shemeji mbona hiki chakula umepakua kidogo hivi, hakuna kilichobaki huko jikoni?_mnakula pamoja mfano ugali, mtu aacha kula upande wake anakuja kumega upande wako
_mnakula pamoja , ghafla mtu anastop anaenda msalani akirudi anaendeleza kupiga menu na mnashea
_mnakula mfano nyama, mtu anachagua chagua ,badae anaona kipande kinachomfaa ndio anakichukua
_mnakula pamoja, mtu anapiga chafya hazibi mdomo, particles zinawarukia
_mnakula wali maharage may be na mchuzi wa nyama, vimechanganywa kwenye sinia, mtu anafinyanga Kama tonge adi michuzi inachuruzika kwenye kiganja , inatia kinyaa
Ongezea nyingezo![]()




