abdulhamis
JF-Expert Member
- Aug 2, 2019
- 1,422
- 2,301
_mnakula pamoja mfano ugali, mtu aacha kula upande wake anakuja kumega upande wako
_mnakula pamoja , ghafla mtu anastop anaenda msalani akirudi anaendeleza kupiga menu na mnashea
_mnakula mfano nyama, mtu anachagua chagua ,badae anaona kipande kinachomfaa ndio anakichukua
_mnakula pamoja, mtu anapiga chafya hazibi mdomo, particles zinawarukia
_mnakula wali maharage may be na mchuzi wa nyama, vimechanganywa kwenye sinia, mtu anafinyanga Kama tonge adi michuzi inachuruzika kwenye kiganja , inatia kinyaa
Ongezea nyingezo
Khaa! Kumbe kuna watu bado wana hii tabiaNjooni huku pwani muone mpaka leo bado watu wananawa sehemu moja ,yaani anaanza baba anatia mikono kwenye beseni wanafuata watoto na kula kwenye sinia moja,tena wanaona kawaida sana!
Mkuu umeua, pata coke Baridi hapo kwa mangi1) Mfano mnakunywa chai ya Ofisi, Miakte labda inanunuliwa minne. Mmoja ushafunguyliwa na haujaisha but mtuu anakuja anafungua mwengine.
2) Hapo juu mtu anafungua mkate anatoa vipande vyake na haufungu uliobaki, bila kujali Mende na Hewa vyaweza kuingia ukaharibika.
3) Labda vijiko vya chai viko vichache. Mtu anakoroga chai kisha anaonja na kurudishia kijiko kwenye sukari. Kawaida inabid ujue saizi yako, hakuna kuonja kama vijiko ni vya kushea.
4) Mnakula wengi kwenye sahani moja (mtu Kati). Mtu anafinyanga wali akishautia mdomoni anakung'utia mkono kwenye sinia yale mabaki. Kisha anendelea kula.
5) Mchuzi umemiminiwa kwenye wali sahani nzima. Inabidi ule wali kulingana na mchuzi uliomiminwa (Vertically). Sasa wewe unakula kwa kukwangua juu juu (Horizontally) ule wenye mchuzi. Matokeo yake unabakia wa chini ambao hauna mchuzi.
Mbinu na kijesi!plus uchoyo...mnakula unapega jamasi unafuta then unarudi kwenye sinia. Lazima waondoke mezani
Kinyaa, wanalishana uchafuNjooni huku pwani muone mpaka leo bado watu wananawa sehemu moja ,yaani anaanza baba anatia mikono kwenye beseni wanafuata watoto na kula kwenye sinia moja,tena wanaona kawaida sana!
Kuku nusu humalizi mkuu ??Mnakula mtu anamaliza kuku nusu na chips daaah kuna watu wanakula jamani
Ndio mnaanza kula ugali na kuku-jogoo mchuzi, ghafla jirani anaingia na kukaribishwa kwa heshima na taadhima. Anajibu: " Aaaa, nimeshiba, nimetoka kula muda si mrefu uliopita, lakini ngoja nitie baraka kidogo" anamega tonge mbili halafu anageukia bakuli la finyago na kuchukua bonge la paja!! Halafu: Aaa! asanteni nimeshiba" Ananawa mkono na kuodoka akimung'unya paja la jogoo!
Kinyaa !!!Mnakula lnatokea jitu lina mafua linaanza kuyavuta ile sauti inakeraaa. Unataman umwambie akayatoe na asirudi mana n kama atarudi na uchafu
Inakera sanaKinyaa !!!
Daaa! Umenikumbusha mbali sana. Bibi yangu mzaa baba alikuwa anakasirika kweli. Anakufokea mpaka chai/uji unaona una radha ya chloroquineUnakunywa chai/uji alaf unaivuta kwa mdomo hadi unaskia frrrrrrriiii ... Siyo ustaarabu acha ushamba