Tukumbushane kidogo ghetto time!

Tulianza wawili mwisho nikajikuta wamefika 5.
Geto halikatiki mademu wapya wapya tu.
Tatizo majukumu ya getho anaachiwa mwenye geto. Chakula na kodi na bill ndogo ndogo husaidiwi hata kidogo.

Geto lilipoanza kuonekana kama la Bob Marley nilibadilika nikaanza kuwaambia wapange maana kama pesa sote tulizipata na tulikuwa twafanya kazi pamoja.
 
Mambo ya kuishi na masela ni ya kijinga sana.

Kuna jamaa wawili niliwahifadhi ghetto kwangu kwa kama miezi 6 hivi, Wanakula, vyombo vinakaa hata wiki hawaoshi hadi nioshe mimi, Ndani vumbi linajaa, michanga wanakaa tu, hamna wa kujishughulisha nna Usafi isipokuwa mimi. Ilikua inanikera sana.

Watu wanabeba Viepe wanakula wanaacha mifuko na makaratasi juu ya meza, maganda ya ndizi.

Nilivumilia nikashindwa, siku moja nikawatolea uvivu, ila nikaonekana nawanyanyasa na kuwababaisha kisa wanaishi kwangu. Nikawaambia kama hawawezi kubadilika wasepe, Baada ya muda Wakasepa. Hivi sasa naishi mwenyewe mambo safi.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…