Tukumbushane changamoto za Usafiri katika kuvuka mito korofi

Obimbo

Member
Nov 17, 2020
35
36
Amani ya Bwana iwe nanyi,

Tunamshukuru Muumba kwani nchi yetu imejaaliwa kuwa na mito mingi mikubwa kwa midogo, ile ya msimu na isiyo ya msimu. Mito hii licha ya kupendezesha sura ya nchi imeleta pia changamoto za usafiri tokea upande mmoja kwenda upande mwingine.

Nilipokuwa kijana mdogo nlikuwa nikuvutiwa kusikiliza sana story. Ndipo siku moja mama yangu alinisimulia walivyokuwa wakienda shule kwa mabasi ya serikali, hakusita kuniambia adha ya Usafiri hasa kuvuka mto Mara kwa Panton kwani alikua akitokea Tarime kwenda shuleni kwao Weruweru.

Ikumbukwe kuwa eneo hilo ni mahali ambapo mto hukutana na ziwa hivo kasi ya maji inakuwa kubwa, hivyo iliwalazimu manahodha wa Panton kuwa makini japo changamoto hazikuisha, kunanyakati nyingine malori kwa mabasi yalitumbukia katika eneo lile na kupelekea upotevu wa mali pamoja na ndugu zetu.

Kama eneo lile lionekanavyo limezungukwa kwa matete mengi hivo samaki hupenda kuzaliana maeneo hayo vile vile na majoka makubwa pia hayakosi kwani hujipatia kitoweo chao katika mazingira hayo. Siku moja wakiwa tayar wameshaingia ndani ya Panton na nahodha akiwa anajiandaa kukivusha chombo ghafla joka kubwa lilitokea katika matete na kuelekea kuingia katika Panton, taharuki ilikuwa kubwa ilopelekea watu kutaka kujirusha majini lakini kwa namna ya ajabu Muumba aliwaokoa watu wake kwani joka lile lilikaa pale kwa muda na Kisha kurudi majini lenyewe.

Karibu tupeane visa katika kuvuka mito korofi
 
Unavuka mto Mara kwa Pantoni?

mto una upana wa mita 20 mpaka 25 ndio uvuke kwa Pantoni?

mzazi wako amekulisha tango pori hapo mkuu au wewe ndio hujui ulichokiandika😅😅😅
 
Kuna siku tulikua tunacross mto ruaha tunaenda ihefu tukitoka ubaruku na usafiri ni mtumbwi ilikua kamaa saa 2 hivi(usiku)..tulipoingia ndani kama mit 30,tulifika eneo mtumbwi ulikua unazunguka hapohapo na nahodha alivotutia wenge aliacha kupga kasia...kumbe chini kulikua na boko linacheza na watoto. duh haya maish achen wakuu
 
Kuna siku tulikua tunacross mto ruaha tunaenda ihefu tukitoka ubaruku na usafiri ni mtumbwi ilikua kamaa saa 2 hivi(usiku)..tulipoingia ndani kama mit 30,tulifika eneo mtumbwi ulikua unazunguka hapohapo na nahodha alivotutia wenge aliacha kupga kasia...kumbe chini kulikua na boko linacheza na watoto. duh haya maish achen wakuu
Duuuh poleni sana mkuu
 
Kwao na shemeji yangu ni wafugaji, kama tujuavyo katika msimu wa kiangazi sehemu za malisho kwa mifugo huwa changamoto.

Katika kusaka machimbo ya kulisha mifugo wakabaini ya kuwa upande wa pili wa mto mara kunamajani mengi yanayowafaa mifugo yao. Hivo wakawa wanavuka mto na mifugo na kwenda kuchunga upande wa pili na kurudi jioni nyumbani kwani wakati wa kiangazi maji hupungua sana na Katika baadhi ya maeneo maji hufika hadi magotini.

Basi siku hiyo shemeji na mdogo wake wakaenda kuchunga (huwa wanaenda wawili wawili maana mifugo ni wengi) baadae mida ya alasiri walishtuka kuona maji kufika maeneo walipokuwa wanachunga, kaka mtu akashtuka akamwambia dogo mto umejaa, kumbe mvua kubwa imenyesha huko Kenya kwenye vyanzo vya mto Mara na maji yote kusombwa kuja Tz, harakati za kurudi nyumbani zikaanza.

Kama mjuavyo ng'ombe wanaweza ogelea fresh kabisa, hivo wakapata wazo la kudandia juu ya migongo ya ng'ombe daaaah, inauma dogo mtu alifariki ktk juhudi za kuvuka mto, kwani spidi ya maji ilikuwa kubwa na ng'ombe alopanda juu yake kushindwa kumbeba.
 
Huu mto ni balaaa mvua inanyesha huko mbali mnashtukia umefurika halafu hapo kati una kina kirefu pia unakuja na maporomoko ya mawe na magogo.Upo huko kilosa wanapoishi wakaguru kunakolimwa tangawizi nshasahau.
20190118_150627.jpg
 
Sijakataa lakini, Lejea kauli Yako hapo juu , ukihoji 25 m kua na Panton.

Ndipo nikakuuliza Panton inatakiwa kwa umbali gani?
Mkuubsi ukafanye utafiti pale kigamboni mbona kelele...

pantoni mwendo wake from point A to B inatumia hadi dakika 20.

Wakati kuvuka mto kwa mtumbwi ni dakika 2. Je pantoni inaweza kuapply hapo?
 
Back
Top Bottom