Tukumbuke tamthilia ya tausi

Tukumbuke tamthilia ya tausi

Umenikumbusha namna ilivyokuwa ikianzan na kale ka wimbo kake "Tausi ndege wangu, ndege wangu wa fahari.....", na wale jamaa kama kina "kalumanzira...chyaaaaa(anapiga chafya kali xana), wale chokoraaa, siti binti kasri.....ahahahaha umenikumbusha mbali mkuu.
Yaani wakati huo niliku nachelewa kwenda FoE pale UDSM usiku kwa sababu zifuatazo
1. Nilikuwa naanza na Isindingo the need, saa moja na nusu hadi saa mbili
2. Nafuata tausi a.k.a Mjuba, saa tatu
3. Namalizia na acapulco bay ya mara ya kwanza kabla ya kurudiwa

halafu nikiingia FoE, nakuta washikaji wameandika ubaoni eti UE vs MJUBA
 
Acha kabisa! Enzi hizo hatumwi mtoto dukani hata kwa bakora.
 
daaa umekumbukaja lakini mana ni muda sana nakumbuka nipo mkoa
 
duh menikumbusha kitambo aisee..enzi hizo tv moja za kwenda kutazamakwa majirani..
..but kwa tamthilia za nje ilikuwepo passion ..aisee kina Kay,Ethan etc
 
Dah nimekumbuka mbali sana.Karibuni ktk nyumba kumi nyumba moja tu ilikuwa na tv.
Wale Jamaal hata wangekuwa wanauza CD Leo ningenunua
 
me nilikuwa nampenda sana Rukia bint kasri
 
RIP Sitti, japo alichukua maamuzi magumu sana ya kuhujumu nafsi yake.

Enzi hizo Tosamaganga, tuliomba kwa Headmaster Mkanga aturuhusu jumatano akatolea nje, tukawa tunasikiza redioni. kWeli tumetoka mbali sana..
 
namkumbuka yule tausi wa kabla ya tamthilia na kale kawimbo kanako ibwa tauc ndege wang ndege wangu wathamani....wakikaa watu wawil....
 
Nakumbuka Mponda alimuona Sikitu mara ya kwanza. Akaambiwa na Rukia "huyu aitwa Sikitu". Akajibu huyu ni "kitu", maana alikuwa mrembo. Siku nyingi watu waliibiwa sana majumbani.
 
'Enyi mgwirao baharini na nchi kavu! Mumgwire mjuba aje anidondokee!'
Tina.
 
Inanikumbusha Mkwawa High School na couples fulani au wazee wa minazi....:thumbup::thumbup:😀😀
 
Dah!!! Enzi hizo nilikuwa namwaga machozi sana kwa mateso ya Lindi,ila mjuba alikuwa ananifanya nicheke sana
 
Umenikumbusha mbali mkuu! Yan mi nilikuw nampenda sitti tu na mpenzie! Na lindi chokaraa dam! Yan 2nakula mapeeema cku hiyo il 2sichelewe! Afu enzi zile tv kwe2 ilikuw imebomoka baas 2likuwa 2nakusanyana kitaa haooo mtaa wa saba kwa watu mara cku nyngne 2fukuzwe mara 2angalie aisee nikikumbka huwa nacheka saaaana!

Sitti binti Kasri nilisikia alikufa bana mara tu baada ya kuigiza kwenye Tausi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom