sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,408
- 19,033
- Elimu yake watu hawana muda nayo kujua alisomea wapi maana balaa analofanya mbele ya macho yetu ni ushahidi tosha shughuli imempata anaeiweza, wapo kina gift macha wana degree zao lakini wamezimwa na nyota kali ya Manara.
- Manara ndie msemaji anaelipwa mno, milioni 9 kwa mwezi, huu ni mshahara wa miezi miwili ama mitatu ya mwalimu wa chuoni, hapohatujagusia mpunga anaopokea kwenye ubalozi wa azam, gsm na asas, pesa iliyokuwa inamtunza zaidi kuzidi ule mshahara wa laki 7
- Manara ndie msemaji anaekera zaidi upinzani lakini cha ajabu wanaendelea kumfollow hawataki kumu unfollow
- Manara ndie msemaji anaeweza kufanya promo za kujaza dimba.
- Manara ndie msemaji anaeweza kuukera upinzani kwa kiwango cha juuu (kuwakera, maneno ya shombo, kebehi, n.k. ) leo hii tayari mtu akisema "KOLO" picha inakuja ya simba