Lord Denning
JF-Expert Member
- Jun 3, 2015
- 23,494
- 57,871
Amani ya Bwana iwe nanyi wadau,
Natumai wote mu wazima na mnaendelea vizuri sana. Ikiwa ni siku ya jumapili nikiwa namtafakari raisi wangu mpendwa ndugu John Pombe Magufuli kwa jinsi anavonikosha na utendaji wake uliotukua mara ghafla kuna jambo limenijia kichwani ghafla.
Jambo hili linamuhusu mtu mmoja ambaye hakuwa anafahamika na jamii ya watanzania ila alikuja kujizolea sifa kemkem pale alipoteuliwa kuwa waziri wa nishati na madini. Huyu si mwingine bali ni Prof Muhongo ambaye kwa miaka 2 tu aliyokaa pale nishati na madini tuliona utekelezaji wa kasi wa miradi ya usambazaji umeme vijijini kwa record ambayo nchi haikuwai kuwa nayo, pili tuliona utekelezaji na ukamilishwaji wa ujenzi wa bomba la gesi ambalo leo tumeanza kuona faida yake, tatu tuliona ubanwaji wa mirija ya ufisadi kwenye sekta ya madini na gesi kitu kilichowafanya watu wenye nia mbaya nae wamuundie zengwe na kumtengenezea chuki kwa watanzania hadi akajiuzuru.
Kichwa cha mada kinasema tujiulize kwa pamoja kuwa ni Coincidence au MUNGU ameongea na labda watu wanaweza jiuliza ninataka kusema nini hasa?
Kitu ninachotaka kukisema hapa ni kuwa kuna kitu kimetokea hasa juu ya kundi la watu waliokuwa wanaongoza kumsema Prof Muhongo vibaya, hili kundi lote limekutwa na mambo mazito sana ambayo sidhani kama watanzania wenzangu mmeyaona ila nataka tu kushare nanyi at least na nyie muone alafu tujiulize kwa pamoja kuwa Je ni Coincidence au MUNGU AMEONGEA KUWAJIBU WOTE WALIOKUWA WANAMTENGENEZEA PICHA MBAYA PROF MUHONGO KWA WATANZANIA?
Mimi nimeona list fupi ya watu ambao ngoja niiweke hapa,
1. Christopher Ole Sendeka.
Huyu aliweka chuki ya wazi na Prof Muhongo, huku akipewa airtime kubwa na ITV aliwekeza kumkaanga vibaya sana Prof Muhongo ila leo ubunge kaukosa. Je ni ?coincidence au adhabu toka kwa MUNGU?
2. Reginald Mengi.
Huyu najua kila mtu anajua ugomvi wake na Prof Muhongo na najua kwa ma smart analyist huyu alichangia kama asilimia 85 ya kuangushwa kwa Prof Muhongo kupitia media zake na marafiki zake wa kisiasa ila juzi tu kambi ya mgombea uraisi ambaye inasemwa alijitolea kumsupport imeanguka vibaya na sasa hajui la kufanya kwa sababu ambaye alikuwa hampendi na kumuunga mkono ndugu Magufuli ye ndo kawa raisi. Kwa haya yaliyompata ni coincidence au adhabu toka kwa MUNGU?
3. David Kafulila
Huyu ndo aliwekwa kama mastermind wa kumkaanda Muhongo bungeni ila kilichompata kwenye matokea ya ubunge tunajiuliza kuwa je ni coincidence au ndo adhabu ya MUNGU kwa yale aliyotenda dhidi ya Prof Muhongo???
4. Moses Machali
Huyu naye alihusika sana kumkaanga Prof Muhongo sijui kwa kujua au bila kujua ila yaliyomkuta kuangushwa kwenye ubunge tunajiuliza Je ni coincidence au ndo MUNGU kamjibu?
5. Hamis Kingwalala
Huyu naye alijitolea sana kumsema vibaya na kumkaanga Prof Muhongo, ila kwa kuangushwa na bashe na kuukosa ubunge sote tunajiuliza je ni coincidence au MUNGU ndo amemjibu?
6. Zitto Kabwe
Huyu naye alihusika sana kwa yaliyompata Prof Muhongo ila kwa Chama chake ambacho amekijenga kwa nguvu sana kupata mbunge mmoja tu kwenye uchaguzi huu tunajiuliza naye ni coincidence au MUNGU amemjibu kwa aliyomfanyia Prof Muhongo?
7. Felix Mkosamali
Huyu naye kama machali tu alimshupalia sana Prof Muhongo ila sasa amekosa hata ubunge wenyewe sasa tunajiuliza je ni coincidence au naye MUNGU amemjibu?
8. Deo Filikunjombe.
Huyu sitamzungumzia kwa sababu maadili ya dini yangu hayaniruhusu.
Sasa ndugu zangu kwa haya yote yaliyotokea naomba tujiulize kwa pamoja Je ni Coincidence au MUNGU AMEONGEA?
9. Lembeli
Huyu nae kama kawaida yake kusimama anaposimama mzee machache kulimponza kwa sababu nae alimshupalia Muhongo ila nae amekosa ubunge kabisa
10. James Mbatia
Huyu naye akitegemea cheap popularity alimshupalia sana Prof Muhongo na kilichompata ni kuwa chama anachokiongoza kama mwenyekiti kimepoteza viti katika ngome zake na kwa kifupi amebaki kama mbunge pekee wa chama chake bungeni kutoka kuwa na wabunge 4
MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATANZANIA.
cc. Pasco, Faiza Foxy, Gentamycine, Rweye, Elungata, Lizaboni, Kanone
Natumai wote mu wazima na mnaendelea vizuri sana. Ikiwa ni siku ya jumapili nikiwa namtafakari raisi wangu mpendwa ndugu John Pombe Magufuli kwa jinsi anavonikosha na utendaji wake uliotukua mara ghafla kuna jambo limenijia kichwani ghafla.
Jambo hili linamuhusu mtu mmoja ambaye hakuwa anafahamika na jamii ya watanzania ila alikuja kujizolea sifa kemkem pale alipoteuliwa kuwa waziri wa nishati na madini. Huyu si mwingine bali ni Prof Muhongo ambaye kwa miaka 2 tu aliyokaa pale nishati na madini tuliona utekelezaji wa kasi wa miradi ya usambazaji umeme vijijini kwa record ambayo nchi haikuwai kuwa nayo, pili tuliona utekelezaji na ukamilishwaji wa ujenzi wa bomba la gesi ambalo leo tumeanza kuona faida yake, tatu tuliona ubanwaji wa mirija ya ufisadi kwenye sekta ya madini na gesi kitu kilichowafanya watu wenye nia mbaya nae wamuundie zengwe na kumtengenezea chuki kwa watanzania hadi akajiuzuru.
Kichwa cha mada kinasema tujiulize kwa pamoja kuwa ni Coincidence au MUNGU ameongea na labda watu wanaweza jiuliza ninataka kusema nini hasa?
Kitu ninachotaka kukisema hapa ni kuwa kuna kitu kimetokea hasa juu ya kundi la watu waliokuwa wanaongoza kumsema Prof Muhongo vibaya, hili kundi lote limekutwa na mambo mazito sana ambayo sidhani kama watanzania wenzangu mmeyaona ila nataka tu kushare nanyi at least na nyie muone alafu tujiulize kwa pamoja kuwa Je ni Coincidence au MUNGU AMEONGEA KUWAJIBU WOTE WALIOKUWA WANAMTENGENEZEA PICHA MBAYA PROF MUHONGO KWA WATANZANIA?
Mimi nimeona list fupi ya watu ambao ngoja niiweke hapa,
1. Christopher Ole Sendeka.
Huyu aliweka chuki ya wazi na Prof Muhongo, huku akipewa airtime kubwa na ITV aliwekeza kumkaanga vibaya sana Prof Muhongo ila leo ubunge kaukosa. Je ni ?coincidence au adhabu toka kwa MUNGU?
2. Reginald Mengi.
Huyu najua kila mtu anajua ugomvi wake na Prof Muhongo na najua kwa ma smart analyist huyu alichangia kama asilimia 85 ya kuangushwa kwa Prof Muhongo kupitia media zake na marafiki zake wa kisiasa ila juzi tu kambi ya mgombea uraisi ambaye inasemwa alijitolea kumsupport imeanguka vibaya na sasa hajui la kufanya kwa sababu ambaye alikuwa hampendi na kumuunga mkono ndugu Magufuli ye ndo kawa raisi. Kwa haya yaliyompata ni coincidence au adhabu toka kwa MUNGU?
3. David Kafulila
Huyu ndo aliwekwa kama mastermind wa kumkaanda Muhongo bungeni ila kilichompata kwenye matokea ya ubunge tunajiuliza kuwa je ni coincidence au ndo adhabu ya MUNGU kwa yale aliyotenda dhidi ya Prof Muhongo???
4. Moses Machali
Huyu naye alihusika sana kumkaanga Prof Muhongo sijui kwa kujua au bila kujua ila yaliyomkuta kuangushwa kwenye ubunge tunajiuliza Je ni coincidence au ndo MUNGU kamjibu?
5. Hamis Kingwalala
Huyu naye alijitolea sana kumsema vibaya na kumkaanga Prof Muhongo, ila kwa kuangushwa na bashe na kuukosa ubunge sote tunajiuliza je ni coincidence au MUNGU ndo amemjibu?
6. Zitto Kabwe
Huyu naye alihusika sana kwa yaliyompata Prof Muhongo ila kwa Chama chake ambacho amekijenga kwa nguvu sana kupata mbunge mmoja tu kwenye uchaguzi huu tunajiuliza naye ni coincidence au MUNGU amemjibu kwa aliyomfanyia Prof Muhongo?
7. Felix Mkosamali
Huyu naye kama machali tu alimshupalia sana Prof Muhongo ila sasa amekosa hata ubunge wenyewe sasa tunajiuliza je ni coincidence au naye MUNGU amemjibu?
8. Deo Filikunjombe.
Huyu sitamzungumzia kwa sababu maadili ya dini yangu hayaniruhusu.
Sasa ndugu zangu kwa haya yote yaliyotokea naomba tujiulize kwa pamoja Je ni Coincidence au MUNGU AMEONGEA?
9. Lembeli
Huyu nae kama kawaida yake kusimama anaposimama mzee machache kulimponza kwa sababu nae alimshupalia Muhongo ila nae amekosa ubunge kabisa
10. James Mbatia
Huyu naye akitegemea cheap popularity alimshupalia sana Prof Muhongo na kilichompata ni kuwa chama anachokiongoza kama mwenyekiti kimepoteza viti katika ngome zake na kwa kifupi amebaki kama mbunge pekee wa chama chake bungeni kutoka kuwa na wabunge 4
MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATANZANIA.
cc. Pasco, Faiza Foxy, Gentamycine, Rweye, Elungata, Lizaboni, Kanone