Titicomb
JF-Expert Member
- Jan 27, 2012
- 11,332
- 17,835
Nimehamasika kuandika uzi huu kutokana na kitabu cha baba wa Taifa Julius K. Nyerere cha mwaka 1962 kiitwacho TUJISAHIHISHE.
Kitabu ni kirefu kuweza kuwekwa hapa kilichomo chote, lakini ni kifupi ukitaka kukisoma kwani kina kurasa 12 tu ktk mfumo wa kielektroniki wa PDF.
Kwa muktadha wa mada yangu na kwa mwenendo wa yanayo endelea kwenye vyama vikubwa vya siasa nchini Tanzania hasa awamu ya kwanza ya uongozi wa Mh. John P. Magufuli nitaenda kuzungumzia kifupi na kunukuu haya ya mwisho ya kitabu husika.
Yapi yanayo endelea kwenye vyama vya siasa kwa sasa? Ni ukweli ulio wazi karibu ndani ya vyama vyote kumetokea kulaumiana na kunyoosheana vidole miongoni mwa wanachama wa kawaida na viongozi wao, au baina ya viongozi wenyewe kwa wenyewe au viongozi wastaafu na walio katika nyadhifa zao wakati huu.
Lawama na manung'uniko haya vimepelekea baadhi ya wanachama kufukuzwa au kujitoa kwenye vyama vyao na kwenda vyama vingine au kukaa pembeni na kutojihusisha na kile wanacho ona sio sahihi.
Msingi wa maridhiano ni kuambiana ukweli na kuoneshana makosa yetu, kisha kujisahihisha.
Mara nyingi watu huoneana aibu, au wengine wapo ngazi za chini hawawezi kupata nafasi ya kuwaeleza viongozi wao yale wanayo ona hao viongozi wanakosea.
Hii sasa ni nafasi hadhimu ya kuwaeleza ukweli.
Kabla ya yote ningeomba ninukuuu hiyo haya niliyosema na ujumbe uliomo ndio uwe msingi wa mjadala wetu yaani tunapotaja makosa ya chama shindani au kiongozi shindani tusisahau kutaja mabaya ya vyama vyetu au viongozi wa vyama vyetu sabubu ya ukaribu wetu au kuogopa kuwachukiza wana JF. n.k.
Maana sasa hivi kumeibuka kikundi cha wanachama flani toka vyama viwili au vitatu vikubwa wa kutukana matusi mazito mtu yeyote anae jaribu kukosoa au kuonesha udhaifu wa kiongozi wao au chama chao, Hivi vyama sio kificho ni CCM, CHADEMA na ACT.
Kuna kundi la vijana kama wameagizwa kuja kutukana yeyote anae toa mawazo kinzani na chama chao au kiongozi wao.
Kujifanya hauoni au kujiaminisha hakuna tatizo kwenye chama chako au kiongozi wako wa ngazi yeyote hakuondoi tatizo husika, na huenda likaleta madhara makubwa na kukikosesha ushindi chama chako au kukisambaratisha kabisa miaka michache ijayo. Waambieni hapa makosa yao viongozi au wanachama wenu wa kawaida.
" ........
Sitaki mtu yeyote afikiri kuwa mimi niliye andika maneno hayo sinayo makosa hayo. Hivyo si kweli. Kosa moja kubwa sana ambalo pia linatokana na unafsi ni kutaja makosa ambayo sisi wenyewe hatunayo, na kuficha makosa ambayo sisi wenyewe tunayo.
Hii ni kosa lile lile linalotufanya tulaumu tusiowapenda, na kutolaumu tunaowapenda, bila kujali ukweli. Nimetaja makosa haya ili yatusaidie, siyo katika kuwahukumu wenzetu tu ambalo ni jambo rahisi, lakini katika kujihukumu sisi wenyewe, ambalo ni jambo gumu na la maana zaidi"
Julius K. Nyerere.
http://hakielimu.org/files/publications/document149tijisahihishe.pdf
KARIBUNI, WELCOME, BIENVENIDOS, BIENVENUE, WILLKOMMEN, BEM-VINDO, RECENTI!
Kitabu ni kirefu kuweza kuwekwa hapa kilichomo chote, lakini ni kifupi ukitaka kukisoma kwani kina kurasa 12 tu ktk mfumo wa kielektroniki wa PDF.
Kwa muktadha wa mada yangu na kwa mwenendo wa yanayo endelea kwenye vyama vikubwa vya siasa nchini Tanzania hasa awamu ya kwanza ya uongozi wa Mh. John P. Magufuli nitaenda kuzungumzia kifupi na kunukuu haya ya mwisho ya kitabu husika.
Yapi yanayo endelea kwenye vyama vya siasa kwa sasa? Ni ukweli ulio wazi karibu ndani ya vyama vyote kumetokea kulaumiana na kunyoosheana vidole miongoni mwa wanachama wa kawaida na viongozi wao, au baina ya viongozi wenyewe kwa wenyewe au viongozi wastaafu na walio katika nyadhifa zao wakati huu.
Lawama na manung'uniko haya vimepelekea baadhi ya wanachama kufukuzwa au kujitoa kwenye vyama vyao na kwenda vyama vingine au kukaa pembeni na kutojihusisha na kile wanacho ona sio sahihi.
Msingi wa maridhiano ni kuambiana ukweli na kuoneshana makosa yetu, kisha kujisahihisha.
Mara nyingi watu huoneana aibu, au wengine wapo ngazi za chini hawawezi kupata nafasi ya kuwaeleza viongozi wao yale wanayo ona hao viongozi wanakosea.
Hii sasa ni nafasi hadhimu ya kuwaeleza ukweli.
Kabla ya yote ningeomba ninukuuu hiyo haya niliyosema na ujumbe uliomo ndio uwe msingi wa mjadala wetu yaani tunapotaja makosa ya chama shindani au kiongozi shindani tusisahau kutaja mabaya ya vyama vyetu au viongozi wa vyama vyetu sabubu ya ukaribu wetu au kuogopa kuwachukiza wana JF. n.k.
Maana sasa hivi kumeibuka kikundi cha wanachama flani toka vyama viwili au vitatu vikubwa wa kutukana matusi mazito mtu yeyote anae jaribu kukosoa au kuonesha udhaifu wa kiongozi wao au chama chao, Hivi vyama sio kificho ni CCM, CHADEMA na ACT.
Kuna kundi la vijana kama wameagizwa kuja kutukana yeyote anae toa mawazo kinzani na chama chao au kiongozi wao.
Kujifanya hauoni au kujiaminisha hakuna tatizo kwenye chama chako au kiongozi wako wa ngazi yeyote hakuondoi tatizo husika, na huenda likaleta madhara makubwa na kukikosesha ushindi chama chako au kukisambaratisha kabisa miaka michache ijayo. Waambieni hapa makosa yao viongozi au wanachama wenu wa kawaida.
" ........
Sitaki mtu yeyote afikiri kuwa mimi niliye andika maneno hayo sinayo makosa hayo. Hivyo si kweli. Kosa moja kubwa sana ambalo pia linatokana na unafsi ni kutaja makosa ambayo sisi wenyewe hatunayo, na kuficha makosa ambayo sisi wenyewe tunayo.
Hii ni kosa lile lile linalotufanya tulaumu tusiowapenda, na kutolaumu tunaowapenda, bila kujali ukweli. Nimetaja makosa haya ili yatusaidie, siyo katika kuwahukumu wenzetu tu ambalo ni jambo rahisi, lakini katika kujihukumu sisi wenyewe, ambalo ni jambo gumu na la maana zaidi"
Julius K. Nyerere.
http://hakielimu.org/files/publications/document149tijisahihishe.pdf
KARIBUNI, WELCOME, BIENVENIDOS, BIENVENUE, WILLKOMMEN, BEM-VINDO, RECENTI!