Tujikumbushe wahenga

Tujikumbushe wahenga

Inaendelea...
Hapo nipo ofisi za uhamiaji yule officer alienirudisha zimbabwe nipo kwake tena safari hii anataka show money,na mimi sina, akaniambia vinginevyo huingii Botswana nikachanganyikiwa safari hii ilikuwa zaidi nikawa najiuliza nitapata msaada wapi tena?
Nikaamua kuwa kichaa zaidi nikamfokea sana nikamuuliza una nini na mimi sikumbuki maneno mengine lakini nadhani nilinena kwa lugha(joke)
Mala akanigongea muhuri wa kuniruhusu akiwa na hofu kwa jinsi nilivyobadilika
Sura. Mdogo mdogo nikalielekea lilipo basi tayari kwa safari kwenda Gaberone.
Safari iliendelea tukafika Gaberone alfajiri nikiwa na Mtanzania mwenzangu ambaye baadae nikajua jina lake Ramadhan
Asubuhi tukiwa jijini hatujui wapi pa kuanzia lakini mwenzangu alikuwa akinipa moyo kutokana na vyeti alivyonavyo akiwa na imani kwamba ataanza kupata kazi yeye na atanisaidia
Kumbuka safari yangu ni kwenda SA pale Botswana nina siku tisini tu za kukaa.
Taswila tuliyokuwa kuwa nayo juu ya Gaberone tuliona kama jiji kuubwa kuliko hata Dar, tukajikuta kila tukienda huku tuko nje ya mji yaani mji ni mdogo.
Baada ya mizunguko jioni ikafika hatuna pa kulala na wakati huo ulikuwa ni mwezi mtukufu wa ramadhani, jamaa yangu rama akanishauri twende msikitini tukalale pale, lakini wakati tunatafakari tulikuwa bado tunazurula mtaani nikatoa wazo tofauti.
Nikamwambia moyo unanisukuma twende hiyo nyumba tujieleze kuwa tunatafuta kazi kisha tutawalekeza kuwa tupo msikitini ilikuwa kama saa mbili kasoro usiku,kwa vile pale palionekana kuna ujenzi unaendelea, jamaa kakubali tukajisogeza pale tukagonga hodi ghafla nikaona jambo ambalo sikulitegemea aliekuja kufungua mlango ni john tulieachana nae boda ya Botswana mara ya kwanza. nae aliponiona alifunga mlango kabla hatujaingia nikawa kama naota...
Tutaendelea kesho..

Sent from my SM-J730G using JamiiForums mobile app
Daaah hii movie nn
 
Tuendelee..
Kumbe ndani ya ile nyumba walikuwa na mjadala mrefu kuhusu mimi kwa hiyo aliponiona alitahayari na kurudi ndani kuwaeleza kuwa nipo nje.
Alikuja mwenyeji na mke wake wakanihug nikashindwa kuelewa nini kinachoendelea baadae ndio tukapata kujua nini kilimtokea kila mmoja wetu na sasa tupo na rama maisha yaliendelea huku mimi na john tunaendelea kukusanya chochote kwa ajili ya kwenda SA.
Siku moja alikuja ndg mmoja alitoka SA lakini ni mzambia baada ya maongezi mengi alituachia bussness card yake lakini alitusihi kwamba baada ya muda twende SA
Akatuhakikishia atatupa support,ule mwaliko wake hatukuutilia maanani maana tuliamini tungeweza bila msaada wake.
Siku zilivyokaribia kuisha za kukaa Botswana presha ya kuondoka kwenda SA ilizidi kuwa juu ukizingatia sheria zao za ujamiaji ni kama zetu yaani kosa la overstay kwao ni jinai hivyo jela inakahusu.
Sasa mimi nilikuwa tayari kuondoka kwa vyovyote vile,maana naona bora ukamatwe SA utarudishwa kwenu kuliko pale,Hapo shughuli nyingine inaanza tena kumbuka hapo tayari tuna marafiki wenyeji kwa hiyo wengi hawataki tuondoke.
John naye kaingia kwenye mtego kawa mvivu kutoka kila siku anatafuta sababu ili tusiondoke,moyoni nikajiapiza kuondoka peke yangu.
Tulikuwa na hela lakini si nyingi sana na kutoka Gaberone mpaka boda ni karibu sana nikatafuta wenyeji wajanja wanipe ramani jinsi ya kuongia SA bila kupita uhamiaji,wakanielekeza kituo cha kushuka wakaniambia kuna vijana pale unawapa chochote wanakuvusha mpk ng'ambo ya pili.
Nikarudi home nikamuaga john kuwa kesho naondoka nakumbuka kulikuwa na mvutano sana usiku mzima asubuhi nikaanza maandalizi alivyoona nipo sirias naye kaanza maandalizi inafika saa tano asubuhi tupo ndani ya gari kwenda boda.
Dreva alijua tunaposhuka maana wao wanaelewa short cut kama huna pass, tukafika mahali penyewe hatukuwa na haraka mpk baada ya muda wakaja vijana wawili wa kiswana wakataka pesa na baadhi ya nguo ili watuvushe.
Kumbuka sisi tunavaa mitumba ya ulaya kwa hiyo vijana wa kule walikuwa wakipenda zile nguo,tukawapatia baadhi ya nguo na pesa wakatuambia tuwafuate tukaanza kupita katika kijiji hicho ambacho nusu kiko botswana na nusu nyingine SA tuka vuka senyenge sasa tukawa SA nikaona ndoto zinaanza kutimia maana safari ya siku mbili sisi tumetumia miezi mitatu.
Wakati huo kijana mmoja anatangulia mbele kama vile anasoma ramani kisha tunamfuata, tukafika barabarani lakini tunakuwa kichakani kidogo hivyo wakawa wanasimamisha magari kila gari imejaa baadae ikaja gari ndogo datsun milango miwili likasimama,jamaa wakamweleza dreva kuwa tunaenda mji uitwao mafikeng jamaa kakubali tukawaaga vijana kwa furaha tukaingia ndani ya gari tukakaa siti ya nyuma mbele walikuwa wawili yaani dreva na mtu mwingine.
Sasa dreva alikuwa akituuliza vitu vingi kuhusu sisi tukaanza kuangaliana na john kengere ya hatari ilingonga, hisia zetu zilithibitika baada ya kusikia radio call duu kumbe ni askari anaeleza mahali alipo na kwamba anatafuta boda jumpers ghafla anatoa kitambusho katurushia..you guys you are under arrest (mko chini ya ulinzi)..
Itaendelea....

Sent from my SM-J730G using JamiiForums mobile app
 
Tuendelee..
Kumbe ndani ya ile nyumba walikuwa na mjadala mrefu kuhusu mimi kwa hiyo aliponiona alitahayari na kurudi ndani kuwaeleza kuwa nipo nje.
Alikuja mwenyeji na mke wake wakanihug nikashindwa kuelewa nini kinachoendelea baadae ndio tukapata kujua nini kilimtokea kila mmoja wetu na sasa tupo na rama maisha yaliendelea huku mimi na john tunaendelea kukusanya chochote kwa ajili ya kwenda SA.
Siku moja alikuja ndg mmoja alitoka SA lakini ni mzambia baada ya maongezi mengi alituachia bussness card yake lakini alitusihi kwamba baada ya muda twende SA
Akatuhakikishia atatupa support,ule mwaliko wake hatukuutilia maanani maana tuliamini tungeweza bila msaada wake.
Siku zilivyokaribia kuisha za kukaa Botswana presha ya kuondoka kwenda SA ilizidi kuwa juu ukizingatia sheria zao za ujamiaji ni kama zetu yaani kosa la overstay kwao ni jinai hivyo jela inakahusu.
Sasa mimi nilikuwa tayari kuondoka kwa vyovyote vile,maana naona bora ukamatwe SA utarudishwa kwenu kuliko pale,Hapo shughuli nyingine inaanza tena kumbuka hapo tayari tuna marafiki wenyeji kwa hiyo wengi hawataki tuondoke.
John naye kaingia kwenye mtego kawa mvivu kutoka kila siku anatafuta sababu ili tusiondoke,moyoni nikajiapiza kuondoka peke yangu.
Tulikuwa na hela lakini si nyingi sana na kutoka Gaberone mpaka boda ni karibu sana nikatafuta wenyeji wajanja wanipe ramani jinsi ya kuongia SA bila kupita uhamiaji,wakanielekeza kituo cha kushuka wakaniambia kuna vijana pale unawapa chochote wanakuvusha mpk ng'ambo ya pili.
Nikarudi home nikamuaga john kuwa kesho naondoka nakumbuka kulikuwa na mvutano sana usiku mzima asubuhi nikaanza maandalizi alivyoona nipo sirias naye kaanza maandalizi inafika saa tano asubuhi tupo ndani ya gari kwenda boda.
Dreva alijua tunaposhuka maana wao wanaelewa short cut kama huna pass, tukafika mahali penyewe hatukuwa na haraka mpk baada ya muda wakaja vijana wawili wa kiswana wakataka pesa na baadhi ya nguo ili watuvushe.
Kumbuka sisi tunavaa mitumba ya ulaya kwa hiyo vijana wa kule walikuwa wakipenda zile nguo,tukawapatia baadhi ya nguo na pesa wakatuambia tuwafuate tukaanza kupita katika kijiji hicho ambacho nusu kiko botswana na nusu nyingine SA tuka vuka senyenge sasa tukawa SA nikaona ndoto zinaanza kutimia maana safari ya siku mbili sisi tumetumia miezi mitatu.
Wakati huo kijana mmoja anatangulia mbele kama vile anasoma ramani kisha tunamfuata, tukafika barabarani lakini tunakuwa kichakani kidogo hivyo wakawa wanasimamisha magari kila gari imejaa baadae ikaja gari ndogo datsun milango miwili likasimama,jamaa wakamweleza dreva kuwa tunaenda mji uitwao mafikeng jamaa kakubali tukawaaga vijana kwa furaha tukaingia ndani ya gari tukakaa siti ya nyuma mbele walikuwa wawili yaani dreva na mtu mwingine.
Sasa dreva alikuwa akituuliza vitu vingi kuhusu sisi tukaanza kuangaliana na john kengere ya hatari ilingonga, hisia zetu zilithibitika baada ya kusikia radio call duu kumbe ni askari anaeleza mahali alipo na kwamba anatafuta boda jumpers ghafla anatoa kitambusho katurushia..you guys you are under arrest (mko chini ya ulinzi)..
Itaendelea....

Sent from my SM-J730G using JamiiForums mobile app
Mmeingia mikononi kwa kunguru
 
Tuendelee..
Kumbe ndani ya ile nyumba walikuwa na mjadala mrefu kuhusu mimi kwa hiyo aliponiona alitahayari na kurudi ndani kuwaeleza kuwa nipo nje.
Alikuja mwenyeji na mke wake wakanihug nikashindwa kuelewa nini kinachoendelea baadae ndio tukapata kujua nini kilimtokea kila mmoja wetu na sasa tupo na rama maisha yaliendelea huku mimi na john tunaendelea kukusanya chochote kwa ajili ya kwenda SA.
Siku moja alikuja ndg mmoja alitoka SA lakini ni mzambia baada ya maongezi mengi alituachia bussness card yake lakini alitusihi kwamba baada ya muda twende SA
Akatuhakikishia atatupa support,ule mwaliko wake hatukuutilia maanani maana tuliamini tungeweza bila msaada wake.
Siku zilivyokaribia kuisha za kukaa Botswana presha ya kuondoka kwenda SA ilizidi kuwa juu ukizingatia sheria zao za ujamiaji ni kama zetu yaani kosa la overstay kwao ni jinai hivyo jela inakahusu.
Sasa mimi nilikuwa tayari kuondoka kwa vyovyote vile,maana naona bora ukamatwe SA utarudishwa kwenu kuliko pale,Hapo shughuli nyingine inaanza tena kumbuka hapo tayari tuna marafiki wenyeji kwa hiyo wengi hawataki tuondoke.
John naye kaingia kwenye mtego kawa mvivu kutoka kila siku anatafuta sababu ili tusiondoke,moyoni nikajiapiza kuondoka peke yangu.
Tulikuwa na hela lakini si nyingi sana na kutoka Gaberone mpaka boda ni karibu sana nikatafuta wenyeji wajanja wanipe ramani jinsi ya kuongia SA bila kupita uhamiaji,wakanielekeza kituo cha kushuka wakaniambia kuna vijana pale unawapa chochote wanakuvusha mpk ng'ambo ya pili.
Nikarudi home nikamuaga john kuwa kesho naondoka nakumbuka kulikuwa na mvutano sana usiku mzima asubuhi nikaanza maandalizi alivyoona nipo sirias naye kaanza maandalizi inafika saa tano asubuhi tupo ndani ya gari kwenda boda.
Dreva alijua tunaposhuka maana wao wanaelewa short cut kama huna pass, tukafika mahali penyewe hatukuwa na haraka mpk baada ya muda wakaja vijana wawili wa kiswana wakataka pesa na baadhi ya nguo ili watuvushe.
Kumbuka sisi tunavaa mitumba ya ulaya kwa hiyo vijana wa kule walikuwa wakipenda zile nguo,tukawapatia baadhi ya nguo na pesa wakatuambia tuwafuate tukaanza kupita katika kijiji hicho ambacho nusu kiko botswana na nusu nyingine SA tuka vuka senyenge sasa tukawa SA nikaona ndoto zinaanza kutimia maana safari ya siku mbili sisi tumetumia miezi mitatu.
Wakati huo kijana mmoja anatangulia mbele kama vile anasoma ramani kisha tunamfuata, tukafika barabarani lakini tunakuwa kichakani kidogo hivyo wakawa wanasimamisha magari kila gari imejaa baadae ikaja gari ndogo datsun milango miwili likasimama,jamaa wakamweleza dreva kuwa tunaenda mji uitwao mafikeng jamaa kakubali tukawaaga vijana kwa furaha tukaingia ndani ya gari tukakaa siti ya nyuma mbele walikuwa wawili yaani dreva na mtu mwingine.
Sasa dreva alikuwa akituuliza vitu vingi kuhusu sisi tukaanza kuangaliana na john kengere ya hatari ilingonga, hisia zetu zilithibitika baada ya kusikia radio call duu kumbe ni askari anaeleza mahali alipo na kwamba anatafuta boda jumpers ghafla anatoa kitambusho katurushia..you guys you are under arrest (mko chini ya ulinzi)..
Itaendelea....

Sent from my SM-J730G using JamiiForums mobile app
Duuuh harakati zote hizo mnaishia kwenye mikono ya polisi aisee
 
Mimi nipo naishi huku mkuu nataka kufahamu ulifika MJI gani hapa South Africa
 
Inaendelea....
Yule polisi baada ya kuturushia kitambulisho na kutuambia you are under arrest tukaona sasa tumekwisha.
Lakini binafsi moyoni mwangu nikajisemea potelea mbali maana tayari nipo SA sheria zao wanakurudisha kwenu, lakini tulindelea kubembeleza hapo kimombo kimeanza kupanda kidogo,john anasomesha na mimi ninasomesha tukaanza kuomba tumpe chochote nakumbuka tulitaka kumpa pula 100 akakataa tukapanda dau 200 kagoma tukaona tumpe yote tuliyonayo yaani pula 300 hapo hatutabakiwa na hela yoyote kakubali bwana,,
Wakati huo gari ipo speed tunaitafuta mafikeng ambao ni mji wa kwanza unapoingia SA,tukakatiza baadhi ya mitaa, mwisho katupeleka stendi ya mabasi yanayoenda joberg(johansberg)
Moja kwa moja katushusha jirani kabisa na moja ya mabasi yanayoenda Jobeg katuacha pale, kumbuka hela yote tumempa hatuna nauli na pale watu wa uhamiaji wapo kila kona ni saa kumi jioni hiyo.
Tukashauriana chap chap tutoke twende uelekeo nje ya mji tukajipange huko tulitembea mwendo wa km dkk 40 tukaona tupo salama ila hela hatuna na mara ya mwisho kula ilikuwa asubuhi.
Siku hiyo ni katika siku ambazo ilikuwa ngumu sana kwetu maana hakuna pori la kujihifadhi tukatafuta sehemu ina kama kadimbwi kaliko kauka pale tukaona salama hatua chache toka barabara kuu kwa mbali kidogo kuna makazi ya watu.
Wakati huo kigiza kimeanza magari ya patroo yanapishana tuu tukaona hapa panafaa tuu,baada ya muda waliibuka mbu ka vile ni kiwanda tukaona isiwe taabu tukavaa manguo mengi ili tuwadhibiti,tukafanikiwa kiasi tukaendela kupiga story za mafanikio na ndoto za maisha yajayo,mwenzangu alikuwa akimwongelea sn mpenzi wake ambaye leo ni mke wake(atanisamehe john km anasoma story hii)
Baada ya muda kama saa 8 usk tukasikia muungurumo wa mvua kwa mbali sana tukashtuka,duu kama nusu saa ilishuka mvua si ya kawaida ndani ya dkk 10 tukawa tumelowa chapachapa na tulipokuwa ilikuwa bwawa la maana tukatafuta mahali palipoinuka kidogo , tuliloa kwa maana ya kulowa mabegi yaligeuka ndoo. kwa kwa kweli tulilia usiku huo kila mtu akiongea lake...
Itaendelea soon..



Sent from my SM-J730G using JamiiForums mobile app
 
  • Thanks
Reactions: Lee
Inaendelea...
Toka saa 8 usiku mpk asubuhi tulisimama maana tumelowa balaa, ilipofika asubuhi tukaona njia pekee ya kukauka ni kutembea mwendo mwingine kutoka nje ya mji ili muda tukianza kurudi mpaka tunafika mjini tutakuwa tumekauka.
Kweli tulifanikiwa kwa kiasi japo mabegi yalikuwa bado,mida ya saa nne asubuhi tukawa mjini tena tumetulia mahali japo uhamiaji kila dkk wanapita kilicho tusaidia tulikaa na jamaa mmoja anauza dawa za asili kwa hiyo wakipita uhamiaji alikuwa akiongea kiswana kwa sauti kwa hiyo wengi walijua na sisi ni waswana hiyo ilituokoa kwa sehemu.
Masaa yanaenda inafika usiku hatuna jibu na njaa imepamba moto, nakumbuka ilikuwa usiku saa mbili nikasogea karibu na msikiti pembeni namwona mzungu mrefu kashiba nikaona nikajieleze atupe chochote (hapa nikukumbuka huwa nacheka peke yangu)
Nikamsogelea nikamwambia "GOOD MORNING SIR" kumbuka ni saa mbili usiku yule jamaa alinikazia macho kama dkk 5 hivi bila kupepesa macho,mie huyooo mdogomdogo...
Nikamfuata john tukalekea pale pale tulipolala jana ila leo palikuwa pamekauka story nyiingi mpaka asubuhi ila sasa nguvu zimeanza kutuishia maana tunaingia siku ya pili bila kula chochote
Kama kawaida tukarudi kijiweni kwetu tulipokuwa jana mida inaenda njaa imepamba moto hatujui tufanyeje miili haina nguvu,
Wazo linatujia tunamkumbuka yule jamaa mzambia alietuachia bussness card tena alisema anakaa mji ule tukaanza kutafuta ile card tukajaikuta ila imeharibika kwa kulowa na namba zake zinaonekana kwa shida kdg tukamshukuru Mungu.
Wakati huo simu zilikuwa za box yaani unatumbukiza coin ndio unapiga simu(vijana wa sasa hamtaelewa) tukamuomba yule mtu aliekuwa anauza dawa za asili atusaidie hela kdg ili tupate mawasiliano.
Jamaa katoa hela tukaamua kupiga ile namba daa kapokea mdada anaongea lugha ya huko na sisi hatuelewi na hela inakata.
Wakati tunaangaliana usoni katokea jamaa mmoja ni mmoja wa madereva wa tax(daradara za kule) kuna kitu aligundua katuuliza kulikoni ndugu tukamweleza jamaa kachukua ile namba kaweka coin yake kapiga simu wakaongea kirefu na upande wa pili.akatwambia yule ni secretary wa huyo mzambia ss mmoja wenu nitampa maelekezo dreva atakushusha pale pale.
Kura ikamwangukia john aende mimi nikabaki kijiweni ila nguvu sina kwa njaa nilokuwa nayo ni sa 8 mchana.
Saa 10 jioni namuona john amakuja kunichukua tabasamu linarudi maana namuona mwenzangu ana uso wa nuru.
Hatukua na muda wa kukaa tukapanda gari haoo kwa mwenyeji wetu yeye hakuwepo tulimkuta mke na watoto japo alipata habari zetu.
Mwenzangu alisha kula mwanzo mimi wakaniandalia matunda wakati nasubiri chakula matunda ya mananasi,hapo nahisi roho inataka kuchomoka kwa njaa,ile naweka kipande cha kwanza tuu mdomoni nilitoa sauti ya kelele nilihisi kama wembe unakata koo niliumia sana.
Hapa wataalam wa lishe watatusaidia....
Itaendelea


Sent from my SM-J730G using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom