tujikumbushe maneno ya wahenga!

tujikumbushe maneno ya wahenga!

Head current

JF-Expert Member
Joined
Jan 17, 2013
Posts
479
Reaction score
128
wahenga walisema chanda chema huvikwa pete na mchagua jembe si mkulima! na pia aliye juu mngoje chini! hembu na wewe tupia ya kwako ya wahenga! karibu....
 
Vyakutwanga vianike angali jua lingalipo! 2.mchuzi wa mbwa unywe ungali wa moto. 3. Raha ya sebene mtu uichezee kenele 4. Kina cha fikra hakipimwi kwa kamba. 5. Mchuzi wa kibua mkabidhi mzigua
 
samaki mkunje angali mbichi, 2.haba na haba hujaza kibaba, 3.chururu si ndo ndo ndo, 4.akufukuzaye akwambii toka, 5.hakuna marefu yasiyo na nchi, 6.mkataa pema pabaya pana mwita, 7.dalili ya mvua ni mawingu, 8.nyota njema huonekana asubuhi, 9.fimbo ya mbali haiuwi nyoka, 10.simba mwenda pole ndo mla nyama!
 
Gogo halikumwi kwa mkojo!,
tembele haliuzwi buchani,
kupenda usipopendwa,ni sawa na kusubir boti airport!!
Daily news halisomwi tandale kwa mtogole!!!

aaash samahani unataka za kizamani sory ntarud baadae ngoja nikachek daftar yangu ya std 6!!!!
 
haba na haba hujaza kibaba! asiyeskia la mkuu, huvunjika guu! mbio za sakafuni, huishia ukingoni! heri nusu shari kuliko shari kamili! majuto ni mjukuu!
 
Uzi huu ungefaa sana kule jukwaa la lugha, mi naona ndo mahala pake. Hata hivyo nachangia:
1. Mwenye dada hakosi shemeji.
2. Angaruka juu kipungu hafiki mbinguni.
3. Mwenda tezi na omo marudio ngamani.
4. Ukitaka kuruka agana na nyonga.
5. Mbaazi ukikosa maua husingizia jua.
6. Mchelea mwana kulia hulia yeye.
 
Ganda la mua la jana chungu huona kivuno
Adhabu ya kaburi aijuae maiti
Sumu mpe paka mwenye roho ngumu ukimpa mbuzi utamdhulumu
 
tulishahada nashusha hada yani ukisusa wenzio twala. Wahenga hao
 
Back
Top Bottom