Tujikumbushe: Jeshi la Marekani Latungua Ndege ya Abiria ya Iran Makusudi na Kuua Abiria Wote 290

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Leo hii Marekani ni kinara wa kuisakama Urusi juu ya kutunguliwa kwa ndege ya abiria ya Malaysia na kuua watu wote 296. Japokuwa sote tunalaani kitendo cha ndege ya abiria kutunguliwa na abiria wasio na hatia kuuawa, huenda watu wasichokumbuka au walichosahau ni kwamba tarehe 3 July 1988 Meli ya kivita ya Marekani, kwa makusudi kabisa, na ikiwa katika eneo la maji la Iran, iliitungua ndege ya abiria Iran Airflight 655 aina ya Airbus A300 B2-203, na kuua abiria wote 290 waliokuwa kwenye ndege hiyo, kutia ndani watoto 66 na wafanyakazi wa ndege 16. Ndege hiyo ya Iran ilikuwa ikisafiri toka Teheran kwenda Dubai.



Iran Air Flight 655
Walipoulizwa juu ya hili na Mahakama za Kimataifa, Wamerakani walijibu kwamba walidhani hiyo ndege ya abiria ya Iran ilikuwa ni ndege ya kivita. Wamarekani hawajawahi kuomba msamaha juu ya jambo hili hadi leo, japo walikubali kulipa $213,103.45 kwa kila abiria aliyekufa. Hakuna hatua zozote za kimataifa zilizochukuliwa dhidi ya Marekani kwa tukio hili.

Iran walichapisha stemp za kumbukumbu ya tukio hili





Abiria waliokufa katika tukio hilo ni kama ifuatavyo;


NationalityPassengersCrewTotal
23px-Flag_of_Iran.svg.png
Iran
23816254
23px-Flag_of_the_United_Arab_Emirates.svg.png
United Arab Emirates
13013
23px-Flag_of_India.svg.png
India
10010
23px-Flag_of_Pakistan.svg.png
Pakistan
606
23px-Flag_of_SFR_Yugoslavia.svg.png
Yugoslavia
606
23px-Flag_of_Italy.svg.png
Italy
101
Total27416290
Source: Wikipedia
 
Taifa la marekani limetengenezwa kwa mauaji ya watu wengi sana na uwepo wake lazima wengi wafe.ila yana mwisho
 
dah halaf eti usa ndo kinara wa haki za binadamu
https://jamii.app/JFUserGuide usa
 
dah halaf eti usa ndo kinara wa haki za binadamu...

Ingawa sikubaliani na msimamo wa AU kujitoa ICC, lakini vitu kama hivi ndio vimekuwa vikichochea mataifa ya Afrika kukataa kuwakamata watu kama Ab Bashir wakashitakiwe ICC.
 
Back
Top Bottom