Tujadili, Tangazo la biashara la Coca cola "onja msisimko"

Tujadili, Tangazo la biashara la Coca cola "onja msisimko"

Chililo

Senior Member
Joined
Mar 22, 2013
Posts
150
Reaction score
114
Wadau habarini ya Jumapili!!

Nimeona Leo tujadili kuhusu hili Tangazo la coca cola la onja msisimko.

Kimsingi nimefurahishwa sana na ubunifu uliotumika katika Tangazo hili. Ambalo linaonyesha jinsi vijana wa familia moja ambavyo kaka mkubwa alivyokuwa akimtesa mdogo wake, ambapo katika utoto huwa ni kawaida mkubwa kumnyanyasa mdogo wake kwa ubabe, ambapo kimsingi huwa ni michezo ya utani.

Kwenye tangazo hili, linaonyesha jinsi, kaka anavyomsumbua mdogo wake kwa ufupi wa kimo, pale anapotaka kuchukua earphone ambazo zipo juu ya kabati na mdogo mtu kwa ufupi wake hawezi kufika, Hivyo kaka mtu anaamua kuzihamisha na kuziweka juu zaidi ili dogo ahangaike, pia kaka mtu anamkanyaga miguu mdogo wake wakati wa kula ili kumsulubu tu, na mwisho kaka mtu anakuja kumsaidia mdogo wake pale anaponyanyaswa na watu wengine kwa kumchukulia chupa yake ya Coke!! Dogo haamini wema aliofanyiwa na kaka yake.

My take:
Tangazo hili linanikumbusha jinsi kaka yangu alivyokuwa akinifanyia utemi, kisa yeye ni mkubwa!! Lakini ilipokuwa inatokea nipo shuleni watu wananinyanyasa kaka alikuwa akija kunisaidia ili kuninusuru na kipigo.

Hongera Coca cola kwa ubunifu huu.
Karibuni kwa mjadala wadau.
 
Wadau habarini ya Jumapili!!

Nimeona Leo tujadili kuhusu hili Tangazo la coca cola la onja msisimko. Kimsingi nimefurahishwa sana na ubunifu uliotumika katika Tangazo hili. Ambalo linaonyesha jinsi vijana wa familia moja ambavyo kaka mkubwa alivyokuwa akimtesa mdogo wake, ambapo katika utoto huwa ni kawaida mkubwa kumnyanyasa mdogo wake kwa ubabe, ambapo kimsingi huwa ni michezo ya utani. Kwenye tangazo hili, linaonyesha jinsi, kaka anavyomsumbua mdogo wake kwa ufupi wa kimo, pale anapotaka kuchukua earphone ambazo zipo juu ya kabati na mdogo mtu kwa ufupi wake hawezi kufika, Hivyo kaka mtu anaamua kuzihamisha na kuziweka juu zaidi ili dogo ahangaike, pia kaka mtu anamkanyaga miguu mdogo wake wakati wa kula ili kumsulubu tu, na mwisho kaka mtu anakuja kumsaidia mdogo wake pale anaponyanyaswa na watu wengine kwa kumchukulia chupa yake ya Coke!! Dogo haamini wema aliofanyiwa na kaka yake.
My take:
Tangazo hili linanikumbusha jinsi kaka yangu alivyokuwa akinifanyia utemi, kisa yeye ni mkubwa!! Lakini ilipokuwa inatokea nipo shuleni watu wananinyanyasa kaka alikuwa akija kunisaidia ili kuninusuru na kipigo.
Hongera coca cola kwa ubunifu huu.
Karibuni kwa mjadala wadau.

Hili tangazo linafaa sana kuikumbusha serikali yetu kwamba Watanzania tunapokuwa hapa nchini nyumbani wanaweza wakatunyanyasa sana, lakini pale tunapokuwa nchi za nje na kunyanyaswa huko inapaswa kutusaidia badala ya tabia ya sasa ya ofisi zetu za ubalozi ambapo huwa hawajali kabisa kusaidia Watanzania wanaokumbwa na matatizo wakiwa nje ya nchi. Yaani maofisa katika balozi zetu wapo kwa ajiil ya ulaji na kutengeneza dili tu, usitegemee msaada wa maana toka kwao ukikwama nje ya nchi.
 
Kuona tangazo kwenye TV ni lazima uwe unakunywa Coca? Kweli pombe za kununuliwa zimekuharibu.

Ni aibu kuja mtandaoni kujinadi eti unakunywa mipombe ya mafundi ujenzi ili ulewe haraka.

Sio vizuri mkuu mwenzio mzalendo anakunywa ya kunyumba
Nyie mmezoea ile UEFA champion league pombe inapanda ndege
 
Tangazo zuri sana hasa pale Bro alipo iokoa soda kutoka kwa Madogo wa Kitaa na kuibetua soda wakati Dogo anakunywa.
 
tangazo lenyewe wamechemka..dogo anaonekana anakunywa soda ipo mdomoni anashusha chupa inaonekana bado imejaa..by the way wamejitahidi kuedit
 
tangazo lenyewe wamechemka..dogo anaonekana anakunywa soda ipo mdomoni anashusha chupa inaonekana bado imejaa..by the way wamejitahidi kuedit
ingekua wamefanya bongo movie,makosa yangeonekana mapema na dharau hadi kunakucha
 
Sijawahi kuliona hadi mwisho. Jirani huwa anabadili channel ila linaonekana ni zuri sana.
 
Hili tangazo linafaa sana kuikumbusha serikali yetu kwamba Watanzania tunapokuwa hapa nchini nyumbani wanaweza wakatunyanyasa sana, lakini pale tunapokuwa nchi za nje na kunyanyaswa huko inapaswa kutusaidia badala ya tabia ya sasa ya ofisi zetu za ubalozi ambapo huwa hawajali kabisa kusaidia Watanzania wanaokumbwa na matatizo wakiwa nje ya nchi. Yaani maofisa katika balozi zetu wapo kwa ajiil ya ulaji na kutengeneza dili tu, usitegemee msaada wa maana toka kwao ukikwama nje ya nchi.
Aisee hvi n kweli?
 
tangazo zuri sana.Ubunifu wa hali ya juu umetumika
 
Kwa kweli hata mimi linanikunGa hilo tangazo ni la kawaida ila
Ndio
Mambo tunayoyaishi ni ubunifu hapa watu wa marketing
Wajifunze
Na
Nadhani wamelipata south africa
 
Sijaelewa. Make naona tu "kakamtu" ina mana kuna ambaye sio mtu apo.
 
JAMANI waandishi wa hapa bongo hawana ubunifu sasa mimi
Nawapa kitu cha ubunifu hivi ukifika
Air port arrival nani anajua kwamba alarm
Za
Magali huwa hazifanyi kazi vizuri ukitoka pale zinafanya jaribu siku mojamukilock mlango alarm
Inakataa jaribu siku moja halafu mtupe
Mrejesho jpili njema
 
Back
Top Bottom