Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Tujadili: Nani wa kushika bango la vita dhidi ya ufisadi?
Baada ya Reginald Mengi kujitolea kushika bango la vita dhidi ya mafisadi, kuna shutuma kali zimetolewa dhidi yake kwamba ama naye pia ni fisadi, ingawa wanaosema hivyo hawataji ufisadi wake ni upi, ama ni msanii tu na anajipendekeza kwa Kikwete eti tu kwa sababu hajamtaja Kikwete katika ufisadi.
Hawa wanashangaa kwa nini hakumtaja Kikwete kwani yeye ndiyo anawaelea mafisadi kwani ufisadi wao dhidi ya wananchi ndiyo ulimweka madarakani.
Sasa wana JF tujadili ni nani katika wazalendo washike bango la vita hiyo kwa niaba ya wananchi masikini? Wamejitokeza watu wengine pamoja na wanasiasa lakini wote wameishia kushutumiwa hiki au kile, pamoja na wao kuwa mafisadi pia, wanafiki nk nk nk.
Hawa ni pamoja na Dk Slaa, Samuel Sitta, Harrison Mwakyembe, Anne Kilango, Ole Sendeka, Alloyce Kimaro, Lucas Selelii, Mark Mwandosya na wengineo wengi tu. Wote hawa nao wameshutumiwa kwa mambo mbali mbali pamoja na ufisadi.
Watanzania wenzangu, tumefikia njia panda kuhusu vita hii kwani serikali yenyewe ambayo ndiyo ina vyombo vya kisheria kushughulikia suala la ufisadi, nayo iko lawamani kwa kuwaogopa mafisadi, au kwa maafisa wao kununuliwa na mafisadi. Kesi zinazotinga mahakamani ni kiini macho kwani kuna wengine bado hawajakamatwa.
Nawasihi mtoe mawazo yenu.
Baada ya Reginald Mengi kujitolea kushika bango la vita dhidi ya mafisadi, kuna shutuma kali zimetolewa dhidi yake kwamba ama naye pia ni fisadi, ingawa wanaosema hivyo hawataji ufisadi wake ni upi, ama ni msanii tu na anajipendekeza kwa Kikwete eti tu kwa sababu hajamtaja Kikwete katika ufisadi.
Hawa wanashangaa kwa nini hakumtaja Kikwete kwani yeye ndiyo anawaelea mafisadi kwani ufisadi wao dhidi ya wananchi ndiyo ulimweka madarakani.
Sasa wana JF tujadili ni nani katika wazalendo washike bango la vita hiyo kwa niaba ya wananchi masikini? Wamejitokeza watu wengine pamoja na wanasiasa lakini wote wameishia kushutumiwa hiki au kile, pamoja na wao kuwa mafisadi pia, wanafiki nk nk nk.
Hawa ni pamoja na Dk Slaa, Samuel Sitta, Harrison Mwakyembe, Anne Kilango, Ole Sendeka, Alloyce Kimaro, Lucas Selelii, Mark Mwandosya na wengineo wengi tu. Wote hawa nao wameshutumiwa kwa mambo mbali mbali pamoja na ufisadi.
Watanzania wenzangu, tumefikia njia panda kuhusu vita hii kwani serikali yenyewe ambayo ndiyo ina vyombo vya kisheria kushughulikia suala la ufisadi, nayo iko lawamani kwa kuwaogopa mafisadi, au kwa maafisa wao kununuliwa na mafisadi. Kesi zinazotinga mahakamani ni kiini macho kwani kuna wengine bado hawajakamatwa.
Nawasihi mtoe mawazo yenu.