Tujadili: Nani wa kushika bango la vita dhidi ya ufisadi?

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
234
Tujadili: Nani wa kushika bango la vita dhidi ya ufisadi?

Baada ya Reginald Mengi kujitolea kushika bango la vita dhidi ya mafisadi, kuna shutuma kali zimetolewa dhidi yake kwamba ama naye pia ni fisadi, ingawa wanaosema hivyo hawataji ufisadi wake ni upi, ama ni msanii tu na anajipendekeza kwa Kikwete eti tu kwa sababu hajamtaja Kikwete katika ufisadi.

Hawa wanashangaa kwa nini hakumtaja Kikwete kwani yeye ndiyo anawaelea mafisadi kwani ufisadi wao dhidi ya wananchi ndiyo ulimweka madarakani.

Sasa wana JF tujadili ni nani katika wazalendo washike bango la vita hiyo kwa niaba ya wananchi masikini? Wamejitokeza watu wengine pamoja na wanasiasa lakini wote wameishia kushutumiwa hiki au kile, pamoja na wao kuwa mafisadi pia, wanafiki nk nk nk.

Hawa ni pamoja na Dk Slaa, Samuel Sitta, Harrison Mwakyembe, Anne Kilango, Ole Sendeka, Alloyce Kimaro, Lucas Selelii, Mark Mwandosya na wengineo wengi tu. Wote hawa nao wameshutumiwa kwa mambo mbali mbali pamoja na ufisadi.

Watanzania wenzangu, tumefikia njia panda kuhusu vita hii kwani serikali yenyewe ambayo ndiyo ina vyombo vya kisheria kushughulikia suala la ufisadi, nayo iko lawamani kwa kuwaogopa mafisadi, au kwa maafisa wao kununuliwa na mafisadi. Kesi zinazotinga mahakamani ni kiini macho kwani kuna wengine bado hawajakamatwa.

Nawasihi mtoe mawazo yenu.
 
Tujadili: Nani wa kushika bango la vita dhidi ya ufisadi?

Baada ya Reginald Mengi kujitolea kushika bango la vita dhidi ya mafisadi, kuna shutuma kali zimetolewa dhidi yake kwamba ama naye pia ni fisadi, ingawa wanaosema hivyo hawataji ufisadi wake ni upi, ama ni msanii tu na anajipendekeza kwa Kikwete eti tu kwa sababu hajamtaja Kikwete katika ufisadi.

Hawa wanashangaa kwa nini hakumtaja Kikwete kwani yeye ndiyo anawaelea mafisadi kwani ufisadi wao dhidi ya wananchi ndiyo ulimweka madarakani.

Sasa wana JF tujadili ni nani katika wazalendo washike bango la vita hiyo kwa niaba ya wananchi masikini? Wamejitokeza watu wengine pamoja na wanasiasa lakini wote wameishia kushutumiwa hiki au kile, pamoja na wao kuwa mafisadi pia, wanafiki nk nk nk.

Hawa ni pamoja na Dk Slaa, Samuel Sitta, Harrison Mwakyembe, Anne Kilango, Ole Sendeka, Alloyce Kimaro, Lucas Selelii, Mark Mwandosya na wengineo wengi tu. Wote hawa nao wameshutumiwa kwa mambo mbali mbali pamoja na ufisadi.

Watanzania wenzangu, tumefikia njia panda kuhusu vita hii kwani serikali yenyewe ambayo ndiyo ina vyombo vya kisheria kushughulikia suala la ufisadi, nayo iko lawamani kwa kuwaogopa mafisadi, au kwa maafisa wao kununuliwa na mafisadi. Kesi zinazotinga mahakamani ni kiini macho kwani kuna wengine bado hawajakamatwa.

Nawasihi mtoe mawazo yenu.
kwanza kabisa DR SLAA yupo kundi la pekee yake..ni mpambanaji mahiri na mwenye nia ya kweli..

hawa wengine bado nina wasi wasi nao sana kwani ni wapenda sifa tuu kwa wananchi waonekane wamooo.

wengi wao wamo kwenye mfumo kandamizi kimaamuzi na kuchochea umaskini wa kupindukia.

mfano wabunge hao wa CCM ni wapambe wa wizi mkubwa wa fedha za umma katika halmashauri zao kwa kulea kutokuwajibika kwa watumishi na madiwani wapenda dezooo na kudumaza maendeleo..

hawana jipya karibuni wameanza kupata michango ya kufungua SACCOs kwenye majimbo yao kutoka (kwa mengi) ili hali vyama hivyo vyaweza anzishwa na wananchama kwa michango yao wenyewe..

sita tunaye kwa miaka 40 sasa kama kiongozi mwandamizi asiye na jipya wakuvizia nafasi za uongozi tuu ndani ya ccm na serikali yakee...

SINA IMANI NAO WOTE ZAIDI YA DK SLAA..
 
Ni rais wa nchi na serikali yake. Huyu asipofanya kazi yake sisi wengine tutaonekana wapiga kelele na watafuta sifa tu. Namshukuru sana Mengi kwa kulianzisha, lakini mafisadi wanakula sahani moja na mkuu wa nchi kwa hiyo sioni matokeo yoyote ya mpambano huu. Wapinzani wabunge ndio hivyo wameshanyamazishwa kwa tishio la nyaraka za wizi wa siri za serikali, hivyo nguvu yao ya kushika bango imepunguzwa makali. Suluhisho ni mtu safi kuchukua nchi tu.
 
Ni rais wa nchi na serikali yake. Huyu asipofanya kazi yake sisi wengine tutaonekana wapiga kelele na watafuta sifa tu. Namshukuru sana Mengi kwa kulianzisha, lakini mafisadi wanakula sahani moja na mkuu wa nchi kwa hiyo sioni matokeo yoyote ya mpambano huu. Wapinzani wabunge ndio hivyo wameshanyamazishwa kwa tishio la nyaraka za wizi wa siri za serikali, hivyo nguvu yao ya kushika bango imepunguzwa makali. Suluhisho ni mtu safi kuchukua nchi tu.

Raisi peke yake hataweza kupambana na MAFISADI, sisi wananchi tunatakiwa kushirikiana nae katika swala hili. Mengi ameshafungua njia kilichobaki ni sisi wengine kumunga mkono.
 
Raisi peke yake hataweza kupambana na MAFISADI, sisi wananchi tunatakiwa kushirikiana nae katika swala hili. Mengi ameshafungua njia kilichobaki ni sisi wengine kumunga mkono.

Mkuu Mkulima, kwa vipi sasa tushirikiane naye? Hiyo ndiyo mada. Je ni kwa kutoa ushaidi pale utakapohitajika, ama ni kwenda kufungua kesi mahakamani, au ni kwa kujadili tu kwenye majukwaa na kwenye meza ndefu, au ni kwa kuwanyima kura, ama ni kwa kuchukua sheria mikononi? Rais ni taasisi ambayo ina uwezo wa kuyakabili yote haya. Swala ni je ari, kasi na nguvu ya kuyatenda huyo unaye taka tumuunge mkono ameshaanza? Angalia jirani zetu Malawi na Zambia ndipo utagundua tuko miaka mingi nyuma kuweza kuthubutu.
 
Raisi peke yake hataweza kupambana na MAFISADI, sisi wananchi tunatakiwa kushirikiana nae katika swala hili. Mengi ameshafungua njia kilichobaki ni sisi wengine kumunga mkono.


Mada inazungumzia 'kushika bango'. Mimi nimeelewa nani wa kuwa pale mstari wa mbele! Ndio maaana nikasema ni raisi na serkali yake. Wakishatangulia hao sisi wanachi wazalendo tutafuata automatically. Lakini Mengi akiachiwa bango, na wachache wenye ujasiri kama yeye, kama serikali isipotoa ushirikiano usitegemee kuvuna chochote hapo.
 
Ufisadi unatuathiri Watanzania wote kwa nchi yetu kubaki nyuma kimaendeleo pamoja na kuwa na rasilimali chungu nzima, na kupata mikopo na misaada toka nchi na mashirika mbali mbali duniani. Hivyo Watanzania wote wenye mapenzi ya kweli na nchi yetu inabidi tulibebe bango hilo bega kwa bega na akina Slaa na Mengi, vinginevyo ufisadi utaendelea kukithiri kila kukicha.
 
Kila mwenye nia njema na nchi hii lazima ashike bango dhidi ya mafisadi.
 
"Kila mwenye nia njema na nchi hii lazima ashike bango dhidi ya mafisadi."

*******************************

Msanii: Tatizo ni kwamba yeyote yule atakayejitokeza kushika bango, hata kama ana nia njema, ataandamwa na kutafutiwa tuhuma mbali mbali pamoja na za ufisadi. Tanzania ndiko ilifikia ktk suala la ufisadi -- hatuendi popopte! Inasikitisja!
 
Mkuu ZAK
naamini endapo usalama wa taifa au vyombo vya dola wakiamua kulivalia njuga ishu ya ufisadi sidhani kama kutakuwa na mtu atakayewanyooshea vidole maana bado wananchi tuna imani (ingawa chache) nao.
 
Back
Top Bottom