Tujadili na toa ushauri

Gor

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
2,791
Reaction score
850
Baba yangu mzazi ambaye kwa 100% ananitegemea leo asubuhi nimepata habari kuwa amevunjika mkono wakati anatoka ktk kampeni ya CCM huko Rorya wa mbunge Airo.Cha kushangaza baba yangu tayari ni mzee sana na walichukuliwa na gari toka Kata ya ikoma na kusafiri mpaka maeneo ya bugombi karibu na shirati yapata 40km.Anasema walianguka kwenye gari kutokana na bara bara mbovu....sasa mimi ni chadema damu damu na napigania mabadiliko ili yaje mawazo mapya,watu wapya na sera mpya na hapa napigiwa simu nitoe fedha apelekwe hospitalini but sijisikii kusaidia hilo maana tuko maskini na yeye yuko hivyo(maskini) kwa sb ya sera mbovu za ccm.Je nimsaidie au nichune Nape au Airo amtumie?
 
Baba ana haki ya kuchagua ni mgombea gani anampenda na ni chama gani akiunge mkono hiyo ndiyo demokrasia na hii ni kwa mwanafamilia yeyote hata mke wako anao uhuru wa kuwa na mtazamo unaokinzana na wewe. Hiyo ni siasa na inapaswa kutenganishwa na maswala mengine ya kimaisha. Hebu fikiria kama watu wote wangekua kama wewe unavyotaka dunia ingekuwaje?

Kama unaona unawajibu wa kumsaidia mzazi kama mwanafamilia unapaswa kufanya hivyo bila kujali itikadi zenu. Hilo linaweza kukutokea hata wewe inamaana uko tayari wote wanaokwenda kinyume na mtazamo wako kisiasa wasishirikiane na wewe?

Ni mtazamo tu
 
kwa vipi atabadilika na njia na penye mwanga tunamwonyesha......katika eneo letu hatuna maji ya kunywa toka dunia hii iumbwe,hatuna barabara.....na mwona kama adui na hii ni vita...nadhani ccm wamsaidie sina fedha ya kumsaidia miccm
 
Naachana na ushabiki wa kisiasa lakini hapo ulipofikia tu kujadili umjali au usimjali basi una dhambi kwa muumba wako. Kwanza hakufanya jambo la kumuudhi mungu kwa nini usite kumsaidia mzazi wako?
 
makubwa! kumsaidia mzazi wako unauliza mtandaoni,
Eti yeye chama kingine wewe kingine, kuwa tofauti kisiasa kuna uhusiano gani na vinasaba?
Haya kama una watoto waulize hilo swali wakupe jibu.
 
Apo kwenye ugonjwa saidia tu kamanda maana ni baba ila me nimegoma kutowa pesa kabisa kwa mtu yeyote anaye jihusisha na wanyanganyi ccm!
 
Acha mambo ya ajabu, embu msaidie mzazi wako! Bila ya yey kukuzaa na kukulea vema hadi hapo ulipo hyo chadema ungeijulia WAP???? Vitu vingne vya kufikiria tu co vya kuomba ushauri. USIWE MVIVU WA KUFIKIRI.
 
mwache afe tu ili ukalibishwe ikulu wewe ndio kamanda wa ukweli!.UNYUMBU upstairs
 

Mpatie matibabu akishapona ndipo uongeenaye kwa upole na umshawishi aje upinzani na umwambie kuwa ccm wanampenda akiwa mzima wa afya akipata tatizo wanaachana nae na ccm ina wenyewe na wenyewe ndio wao sio yeye
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…