Tujadili: Haki ya kukosea, mpaka ni wapi?

Tujadili: Haki ya kukosea, mpaka ni wapi?

Hivi huu usemi bado upo active " kosa si kosa kurudia kosa ndio kosa"
 
Too bad mama yangu aliondoka mapema ila since niko mtoto kulikuwa na constant battle kati yake nami kila nililokuwa nafanya alikuwa anani critisize like nimepata 90 kwenye maths nikija homu na furaha na kumwonyesha utasikia anasema wenzio wanapata mia wewe wa tisini wafurahia nn? Kiukwel ilikuwa inanivunja moyo sana so nilikuwa nafanya mambo mengi kwa juhudi ili nimprove wrong,nilikuwa vizuri kwenye michezo tabia,kanisani nilikuwa mwanakwaya mzuri misa ya watoto nk na wengi walikuwa wananisifu kuwa ni mtoto wa pekee bt to me haikuleta maana, nimekuja kumwelewa mwishoni kuwa alitaka niwe the best among the rest !!!
 
Kwanza sweetie nakupongeza kwa thread nzuri ambayo ni nzuri kwa ajili ya kuboresha malezi ambayo ndio msingi wa tabia zetu.
"
Kimsingi,kila binadamu anakosea na lazima tukubali na ni lazima pia tujifunze kusamehe na kusahau.
"
Tatizo kubwa ni kwamba familia na jamii kwa ujumla zimetufundisha kimakosa kuwa kuna makosa ya kusameheka na yasiyosameheka.
"
Mtu,mtoto unapomuonya kuhusu jambo fulani huwa unajua matokeo hasi ya jambo lenyewe.Tatizo kubwa ni pale unapomwambia mtu ubaya wa jambo analotaka kulifanya kwa kuwa unalifahamu,naye anang'ang'ania kufanya,hapa ndipo vitisho na vipigo kwa watoto hutokea.
"
Tunasahau kuwa hata sisi tunalijua jambo fulani kwa kuwa tumelipitia.
"
Binadamu tuna desturi ya kutokuamini maonyo,hivyo wakati mwingine ni vyema kuwaacha wenzetu nao wajifunze kwa vitendo na wakati wao ili wawe walimu kwao wenyewe na wengine pia
"
Wala tusiwachukie wanapojifunza kwani huo ni ubinadamu!
 
mtoto huwa anaguswa na watu wanaomzunguka zaidi kuliko maarufu.

So katika ukoo kuna wale watu tu waliokengeuka, na anawajua hao hao.

Tatizo mfano mbaya anapokuwa mzazi wake lol

Nimependa njia yako, unatumia mifano ya watu wa karibu, mitaani au macelebrities kuprove points zako?
 
Nakumbuka nimeharibu sana tu, wakati nakua; mama ndugu zangu walikuwa wakiniasa nilikuwa nawaona au wamepitwa na wakati au washamba.

leo kuna mengi nayakumbuka na ninajuta kama kaka yangu alivyowahi kuniambia "Kaunga, kuna muda wa majuto".

Nashukuru Mungu, sijaturn up to be worse (thanks to sala za mama yangu).
Lakini, ningekuwa mbali sana kama ningesikiliza na ku-slow down a bit.

Makosa yangu nimeyachukulia kama funzo, na kila nikipata nafasi nashare uzoefu na watu wengine (wadogo kiumri) na mwanangu pia.

Mara nyingine inakuwa ngumu sana na inauma unapomuona binti, kijana anapoelekea so unatumia hata vitisho (una-exaggerate issue) ili mradi tu asifanye kile unachomkataza (baada ya reasoning kushindikana of course).
Hii ni kutokana na kwamba, niliishi yale maisha once (nilipata nafasi ya kukosea na kujifunza kutokana na makosa hayo)

sasa maswali au changamoto zangu ni kwamba;
-ni kwa mambo gani tunaruhusu wanetu, dependants wetu wakosee hoping watajifunza kutokana na makosa?
-kwa mambo gani tunakuwa strict mpaka mwisho?
-ni sahihi kutumia vitisho (pale inapolazimika) ili kuprove point au kumscare kijana (mf: ushoga)?
-kwa utandawazi, maswala ya dating kwa teenagers tunafanya nini (i started dating when l was a teen)?
-is it fair kumzuia mtoto yale ambayo wewe uliyapitia? au kuna jinsi ya kumguide ili asipate madhara au awe responsible/

karibuni kwa mjadala, na samahani mtiririko unaweza kuwa sio mzuri sana.

Maisha tuliyoishi na maisha ya malezi ya watoto au wadogo wetu wa sasa yameebadilika sana hata kufikia hatua ya kuitwa washamba kwenye kila jambo la msingi tunalolikaripia.....Kuna wale walezi waliamua kuwa bendera kila upepo ulipo nae yupo hawa hawataki kuwaeleza vijana ukweli kwa kuhofia kuonekana washamba ama wazamani....tofauti na mimi na kundi la walenzi wanaotetea maadili hata kama tutaonekana washamba au waliopitwa na sayansi na teknolojia. Hakuna tofauti ya maadili zamani na sasa ila kilichobadilika ni namna ya kutoa ujumbe mfano zamani ilikuwa ukivunja maadili hata asiyekufahamu alikuadhibu na ukifika nyumbani ukasimulia kama ulikera kichapo kinaanza tena ila sasa hata watoto wa dada/kaka yangu wa damu siwezi kuwakaribia au kuwaadhibu, hatari baadhi ya wazazi hawawezi kuwakaripia/kuwaonya watoto waliowazaa.....Ndio maana wakati wako ulitambua makosa na sasa unajutia, ila wa sasa hawayajui makosa na hivyo muda wa kujutia hawaupati na mwisho wanaangamia
 
mie mtoto aliniuliza kuhusu kukiss akiwa 3:5 years. Niliogopa lakini nikasema afadhali nimegundua mapema kuwa anajua na anataka kujua zaidi.

Nilianza kuwa namweleza mambo mengi kwa dozi yake.

Pima umri wa mtoto na umweleae kadiri ya uelewa wake.

Kuna siku pia aliuliza mbona 'yake' inasimama? Ina nini?

Mtoto kama mdadisi, usipompa majibu atayatafuta anakokujua yeye mwenyewe.

Afu shule zenyewe za siku hizi wanafundishwa mambo meeengi wakiwa wadogo bora kwenda nao sambamba tu.

Angalau mzazi utamfundisha ukweli.

Je ni muda (umri) gani wa mtoto unakuwa reasonable kuanza 'mazungumzo' haya? Huwa naogopa sana kuanza akiwa mdogo sana nahisi kama naweza kuwa chachu ya yeye kujaribu, au ni uoga wangu tu?
 
Kwa mtazamo wangu ni hivi, si vizuri kumwacha mtoto apitie yale makosa uliyopitia wewe wkt unakua.ni vema ukae naye/nao na kuwaeleza ukweli wajue positive na negative ya mambo mbali mbali hususani wakiwa wanaelekea ktk teen ages.akishajua positive and negative then risk iko kwake mwenyewe kama ataamua kufanya ama kuavoid.Kuna makosa ambayo tulifanya wakati tunakuwa kwa vile wazazi wetu hawakuwa wazi kutuelekeza what to do,so unajikuta tayari umeshatumbukia ktk tatizo na huna msaada.mi nadhani pamoja na mengineyo ni vzr kuweka wazi kila kitu then maamuzi yabaki kwake.

unalolisema ni la msingi ni muhimu sana wazazi kuwa wazi ili mtoto atakapokosea anatambua kwamba ila hili nilishawai kuonywa pia hata Mungu ametoa agizo''mlee mtoto katika njia impasayo naye hataiacha mpaka uzee'' pia kumchapa wakati mwingine si vibaya kwani ni bora hivyo ili uiokoe nafsi yake japo wakati mwingine hupelekea usugu ndo maana tukaagizwa hivi ''usimnyime mtoto wako mapigo utamuokoa nafsi yake na kuzimu''
 
Too bad mama yangu aliondoka mapema ila since niko mtoto kulikuwa na constant battle kati yake nami kila nililokuwa nafanya alikuwa anani critisize like nimepata 90 kwenye maths nikija homu na furaha na kumwonyesha utasikia anasema wenzio wanapata mia wewe wa tisini wafurahia nn? Kiukwel ilikuwa inanivunja moyo sana so nilikuwa nafanya mambo mengi kwa juhudi ili nimprove wrong,nilikuwa vizuri kwenye michezo tabia,kanisani nilikuwa mwanakwaya mzuri misa ya watoto nk na wengi walikuwa wananisifu kuwa ni mtoto wa pekee bt to me haikuleta maana, nimekuja kumwelewa mwishoni kuwa alitaka niwe the best among the rest !!!

Pole about your loss my dear.

Alitaka uwe the best among the best.
Nina uhakika wazazi wote wanataka the best kwa watoto wao, approach tu ndiyo yatofautiana. Kuna baadhi ambao hucapitalize kwenye mabaya (kukemea mabaya ili afanye mazuri) wengine hucapitalize kwenye mazuri (kusifia mazuri ili uzidi kufanya mazuri na automatically uache mabaya) na kuna kama mama lara ambaye anakupa black and white (huku akiisagia black in a way) ili uchague mwenyewe na hence uboost your confidence na usipate wa kumlaumu mwisho wa siku.

I think, to be in the safe side bora kutumia a bit of every approach cha muhimu ni kujua when to you use which.
 
Maisha tuliyoishi na maisha ya malezi ya watoto au wadogo wetu wa sasa yameebadilika sana hata kufikia hatua ya kuitwa washamba kwenye kila jambo la msingi tunalolikaripia.....Kuna wale walezi waliamua kuwa bendera kila upepo ulipo nae yupo hawa hawataki kuwaeleza vijana ukweli kwa kuhofia kuonekana washamba ama wazamani....tofauti na mimi na kundi la walenzi wanaotetea maadili hata kama tutaonekana washamba au waliopitwa na sayansi na teknolojia. Hakuna tofauti ya maadili zamani na sasa ila kilichobadilika ni namna ya kutoa ujumbe mfano zamani ilikuwa ukivunja maadili hata asiyekufahamu alikuadhibu na ukifika nyumbani ukasimulia kama ulikera kichapo kinaanza tena ila sasa hata watoto wa dada/kaka yangu wa damu siwezi kuwakaribia au kuwaadhibu, hatari baadhi ya wazazi hawawezi kuwakaripia/kuwaonya watoto waliowazaa.....Ndio maana wakati wako ulitambua makosa na sasa unajutia, ila wa sasa hawayajui makosa na hivyo muda wa kujutia hawaupati na mwisho wanaangamia

Unajua utandawazi umekuja na bad sides zake, zamani ilikuwa rahisi kudanganywa na tukadanganyika. Lakini sasa hivi bila kureason na mtoto kwa kumpa both sides za coin in black and white, anakuchora tu. Yaani nimepata shida sana na niece na nephews zangu, tena hasa niece. Yaani tulifikia (na mama yake) hatua hadi ya kumuweka ndani, lkn haikusaidia kitu, aivyokuja tulia ni miracle yaani.
 
Do people plan on making mistakes or its just something that occurs spontaneous? and to the kids, making mistakes is the part of learning and growing process

Watoto sometimes do things just to check the outcome; au kushindana tu na mkubwa; pia wakati mwingine ni kwa kutokujua.

Wakubwa tunaplan na tunaexecute hiyo mission!
 
Afu shule zenyewe za siku hizi wanafundishwa mambo meeengi wakiwa wadogo bora kwenda nao sambamba tu.

Angalau mzazi utamfundisha ukweli.

Ukweli ndo muhimu wa watoto haswa wa umri huo..Ila unautoa vipi hapo ndo tatizo.Hatuna budi kuwaelekeza kadri kwa kadri jinsi anavyokua ajifunze kujitegemea na kuwa na maamuzi yake yaliyo sahihi kila mara..watoto wengine wadadisi mno na lazima wakati unarudi nyumbani uwe umeandaa majibu yenye maana kwake la sivyo utaabika.!
 
Back
Top Bottom