Mokaze
JF-Expert Member
- Aug 3, 2018
- 14,375
- 14,870
Wakuu salaam.
Hebu tujadili hii kauli ya "tuishi nao kwa akili" ilivyokaa.
Mtu kama kafuga na kuishi na nyoka au hata mnyama mkali kama chui, simba nk ukimuuliza ni kwa namna gani ameweza kufuga na kuishi na hao wanyama aghalabu miongoni mwa majibu atakayo kupa ni kwamba; "nawafuga na kuishi nao kwa akili (tahadhari)", kwa jibu hilo inaonyesha wazi kwamba bila kutumia akili bila shaka maisha ya huyo mfugaji yatakuwa hatarini kutokana na hao wanyama.
Tukirudi kwenye msemo unaonukuliwa mara nyingi unaosema kwamba; Tuishi nao (wanawake) kwa akili, je hii sio dharau na udhalilishaji kwa wanawake??-- hii, kwa mawazo yangu, ni sawa na kuwaweka wanawake katika kundi la viumbe hatari mithili ya Nyoka nk. Wanawake ni mama zetu, dada, shangazi nk na hata tunashuhudia mwingine leo hii ni mkuu wa nchi yetu pendwa Bongoland, je naye tuishi naye kwa akili??
Naam, sikatai moja kwa moja kwamba hakuna wanawake wa kuishi nao kwa akili lakini pia tusikatae kwambo wapo pia wanaume wa kuishi nao kwa akili, tena hao ndio wengi zaidi, si ndio hao wamepeleka pesa China!!😏
Mimi nadhani huyo muhenga aliyetunga hiyo kauli siku hiyo aliudhiwa na mkewe ndipo akaamua ku generalise kauli hiyo kwa wanawake wote.
Hebu tujadili hii kauli ya "tuishi nao kwa akili" ilivyokaa.
Mtu kama kafuga na kuishi na nyoka au hata mnyama mkali kama chui, simba nk ukimuuliza ni kwa namna gani ameweza kufuga na kuishi na hao wanyama aghalabu miongoni mwa majibu atakayo kupa ni kwamba; "nawafuga na kuishi nao kwa akili (tahadhari)", kwa jibu hilo inaonyesha wazi kwamba bila kutumia akili bila shaka maisha ya huyo mfugaji yatakuwa hatarini kutokana na hao wanyama.
Tukirudi kwenye msemo unaonukuliwa mara nyingi unaosema kwamba; Tuishi nao (wanawake) kwa akili, je hii sio dharau na udhalilishaji kwa wanawake??-- hii, kwa mawazo yangu, ni sawa na kuwaweka wanawake katika kundi la viumbe hatari mithili ya Nyoka nk. Wanawake ni mama zetu, dada, shangazi nk na hata tunashuhudia mwingine leo hii ni mkuu wa nchi yetu pendwa Bongoland, je naye tuishi naye kwa akili??
Naam, sikatai moja kwa moja kwamba hakuna wanawake wa kuishi nao kwa akili lakini pia tusikatae kwambo wapo pia wanaume wa kuishi nao kwa akili, tena hao ndio wengi zaidi, si ndio hao wamepeleka pesa China!!😏
Mimi nadhani huyo muhenga aliyetunga hiyo kauli siku hiyo aliudhiwa na mkewe ndipo akaamua ku generalise kauli hiyo kwa wanawake wote.