Wanawake kubalini sogea tuishi hali ni mbaya

lord atkin

Senior Member
Sep 30, 2018
197
683
Ni nani ajitokeze awaambie ukweli hawa wanawake? Hali inatisha kila siku wanalilia kulipiwa mahari na harusi, yaani siku hizi mwanamke anahitaji harusi (sherehe) kuliko anavyohiyaji ndoa (kuishi na mume).

Wanawake wengine wapo radhi wamwache mwanaume wanayempenda kisa hana uwezo wa kuwalipia mahari na harusi ili waolewe na mwanaume mwenye pesa za mahari.

Wakati hayo yakiendelea wazazi nao wamepandisha mahari bei juu, bila milioni tatu nne au tano hupati mke. Utasikia mbona shangazi yangu aliolewa kwa mahari, jamani zamani kila mzazi alikuwa na ng'ombe na wazazi waliwalipia watoto wao mahari leo hii nani analipia mtoto mahari ya milioni tano? Huyu kijana asiye na ajira ndiyo akulipie mahari ya milioni tano kweli?

Ifike wakati sasa wanawake wabadilike hali ya kiuchumi ya vijana wengi wa kitanzania walio katika umri wa kuoa ni mbaya Sana waache kung'ang'ania mahari na maharusi ya kifahari.

Kijana amemaliza chuo mwaka wa tatu huu yupo mtaani hana ajira lakini binti unang'ang'ania aende kwenu akalipe mahari afunge harusi ndiyo mjenge familia ataweza wapi? Atapata wapi milioni nne za kwenda kulipa mahari na milioni 10 za Harusi? Kwanini usimkubalie muanze kuishi pamoja mjenge familia kwanza hayo mambo mengine ya mahari na harusi yafuate baadaye mkishajipanga?

Wanawake badilikeni kuweni waelewa kubalini sogea tuishi vijana hali ya kiuchumi ni ngumu Sana siku hizi.
 
Kwa nn Wanaume wao ndio wabadilike kwani kina mtu analazimishwa na mtu kuoa,hata hivyo ukitaka wa bila mahali pia wapo.
Vilevile,pia sio lazima kuoa,na kama Huna uwezo wa kumtunza mke unaoa ili Iwaje??
Kumtunza na kulipa mahari na harusi ni vitu viwili tofauti, siyo kwamba mtu akishindwa kulipa hiyo milioni tano na Harusi ya milioni kumi kwamba hawezi Kumtunza mwanamke si kweli.

Kuhusu kuoa mwanamke asiyehitaji mahari ndivyo inavyotokea mwisho wa siku maana mtu huwezi ukatoa kitu ambacho huna, wengi wanaachana baada ya kutoka kujitambulisha na kutajiwa mali hailipiki
 
Cku hizi wanatuuzia bei sawa na Bure mkuu .

Ndoa wanakwambia imegeuka ndoano..

Kinachotokea n single mama wanaongezekaa Kwa Kasi ya 5G..single mama ukimpenda nae anakusaliti na mzazi mwezie bac n vurugu tupuu..


Kataa NDOA..
Cha kushangaza mtu umeshamzalisha bado anataka uende kwao la sivyo muachane, nilishangaa Sana kuna rafiki yangu kafunga ndoa kabisa ya bomani na wana mtoto mmoja mke kamkimbia kaondoka na mtoto kisa hajamalizia mahari mambo gani haya?
 
Unaelewa kwa nini mahari hutolewa?
Haijalishi sababu mahari haipaswi kuwa kikwazo cha watu wawili wanaopendana kuoana mkuu. Kama tunavyopinga vita mila potofu kama ukeketaji ndivyo tupinge vita haya mambo ya kukwamisha watu kuunda familia kisa milioni tatu nne, inamsaidia nini mzazi binti yake kuzeekea nyumbani kisa eti anataka mpaka alipwe mamilioni?
Kwanini basi wazazi wasiweke mahari kidogo tu laki mbili au tatu?
 
Haijalishi sababu mahari haipaswi kuwa kikwazo cha watu wawili wanaopendana kuoana mkuu. Kama tunavyopinga vita mila potofu kama ukeketaji ndivyo tupinge vita haya mambo ya kukwamisha watu kuunda familia kisa milioni tatu nne, inamsaidia nini mzazi binti yake kuzeekea nyumbani kisa eti anataka mpaka alipwe mamilioni?
Kwanini basi wazazi wasiweke mahari kidogo tu laki mbili au tatu?
Kwani wazazi walilalamika binti yao kukaa nyumbani?Haupaswi kutafuta vitu rahisirahisi kama ni mwanaume halisi.Mahari ni kipimo cha kujitambua.
 
Cha kushangaza mtu umeshamzalisha bado anataka uende kwao la sivyo muachane, nilishangaa Sana kuna rafiki yangu kafunga ndoa kabisa ya bomani na wana mtoto mmoja mke kamkimbia kaondoka na mtoto kisa hajamalizia mahari mambo gani haya?
Na cc wanaume tushawagundua nikuwachapaa tu nakuzalisha idadi ya wtt unaweza Lea .unachukua wtt wako unaleaa maana cku hz wanawake wenyewe hawatak kulea wtt wao wakuwazaa wanawatelekeza uko kijijin km baba Yao ajawachukuaa..

Mbonaa kazi ipo 50 Kwa 50 ndio imetufikisha hapa ..

Yaan Bado wanaume hatujasema mkuu,yaan mpk tuseme na tuseme tenaa

Kataa NDOA..
 
Ukiona mchumba wako anataka yale usiyokua na uwezo nayo ujue sio wako, hamuendani, wewe kapuku na yeye ni wakishua. Hata wazazi pia hutaka mahari sometimes kubwa ili kupima uwezo wako maka mtotovwao anaenda pazuri au choka mbaya. Hakuna kitu kila mzazi hutamani hasa kama mzazi alimlea vizuri mwanae kama kumkabidhi kwenye mikono salama, na mikono salama ya siku hizi ni uchumi imara. Tuendelee kusaka vibunda wakuu. Kumaliza chuo miaka mitatu iliyopita bado sio umri wa kutaka kuoa hasa kama bado hujajipata
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom