Tuendelee kumchangia Lissu tuachane na CCM

Maneno mengi wakati msaada mnataka....hela ya kumtibu marekani kamwe hamna ndio maana mliandika barua umoja wa ulaya....
Ujinga tuu ndio mwajua..
 
Ni kweli kabisa. Na tulishawapuuza hao ccm. Mimi nimeishachanga na napanga tena wiki ijayo nikachange nyingine na ntaendelea kuchanga.
 
Sielewi ni kwa nini Lissu amekuwa akiwaita CCM "Ma-CCM" kwenye hotuba zake nyingi, lakini hata sasa sioni kama alikuwa anakosea kuwaita ivo.

Leo Mkuu wa Mkoa wa Tanga na Mjumbe wa Kamati ya siasa ya CCM Mkoa huo, Martine Shighela amesema serikali wanataka kuzuia watanzania kutapeliwa na watu wanaochangisha michango ya matibabu ya Lissu. Kwa maelezo ya Shighela hela zinazochangishwa haziendi kwenye matibabu ya Lissu bali zinatumika kuimarisha chama (CHADEMA?)

Job Ndugai Spika wa Bunge na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM akizungumzia matibabu ya Lisu Nairobi alisema Bunge halitahusika na matibabu ya Lissu kwa kuwa ni CHADEMA na familia ya Lissu ndiyo waliamua kumpeleka Nairobi.

Lakini akijua yote hayo Waziri wa Afya Ummy Mwalimu, amesema kwamba serikali iko tayari kutoa hela ili Lisu akatibiwe kokote kule na kwenye hospitali yoyote ile duniani. Hivi Ummy wakati anatoa taarifa yake hiyo hakujua kwamba msimamo wa Bunge kuhusu matibabu ya Lissu ukoje?

Lakini inavoonekana CCM wamekerwa kutokana na kuona maelefu ya watanzania wanachangia matibabu ya Lissu bila ya kutetereka. Lengo lao la kwanza ni kuzuia uchangishaji huo kipropaganda lakini ikishindikana lazima litatoka "tamko la serikali" kuzuia kumchangia Lissu.

Inavoonekana CCM imebuni njia ya kuwachonganisha CHADEMA na wananchi baada ya kuona CHADEMA wamegoma kuwapigia magoti na wanyonge wa kweli wa nchi hii wamekataa kukatishwa tamaa na CCM na badala yake kila siku wanazidi kuchangia matibabu ya Lissu.

Lengo la kukusanya dolar 50,000 lililowekwa inavoonekana muda si mrefu litafikiwa na bila shaka wanaona watu wanavyochanga na wao wanafedheheka. Hawa waliokataza Lissu asifanyiwe maombi ndiyo leo wanajifanya wanataka kulipia matibabu popote na kwenye Hospitali yoyote ile duniani, KULIKONI?
Hata wasemeje sisi tutachanga tu.
 
Ni kwel kabisa,Ccm ni wanafiki sijapata ona,maombi yenyewe yamezuiwa sembuse gharama za matibabu,hayo ni maaigizo
 
Sielewi ni kwa nini Lissu amekuwa akiwaita CCM "Ma-CCM" kwenye hotuba zake nyingi, lakini hata sasa sioni kama alikuwa anakosea kuwaita ivo.

Leo Mkuu wa Mkoa wa Tanga na Mjumbe wa Kamati ya siasa ya CCM Mkoa huo, Martine Shighela amesema serikali wanataka kuzuia watanzania kutapeliwa na watu wanaochangisha michango ya matibabu ya Lissu. Kwa maelezo ya Shighela hela zinazochangishwa haziendi kwenye matibabu ya Lissu bali zinatumika kuimarisha chama (CHADEMA?)

Job Ndugai Spika wa Bunge na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM akizungumzia matibabu ya Lisu Nairobi alisema Bunge halitahusika na matibabu ya Lissu kwa kuwa ni CHADEMA na familia ya Lissu ndiyo waliamua kumpeleka Nairobi.

Lakini akijua yote hayo Waziri wa Afya Ummy Mwalimu, amesema kwamba serikali iko tayari kutoa hela ili Lisu akatibiwe kokote kule na kwenye hospitali yoyote ile duniani. Hivi Ummy wakati anatoa taarifa yake hiyo hakujua kwamba msimamo wa Bunge kuhusu matibabu ya Lissu ukoje?

Lakini inavoonekana CCM wamekerwa kutokana na kuona maelefu ya watanzania wanachangia matibabu ya Lissu bila ya kutetereka. Lengo lao la kwanza ni kuzuia uchangishaji huo kipropaganda lakini ikishindikana lazima litatoka "tamko la serikali" kuzuia kumchangia Lissu.

Inavoonekana CCM imebuni njia ya kuwachonganisha CHADEMA na wananchi baada ya kuona CHADEMA wamegoma kuwapigia magoti na wanyonge wa kweli wa nchi hii wamekataa kukatishwa tamaa na CCM na badala yake kila siku wanazidi kuchangia matibabu ya Lissu.

Lengo la kukusanya dolar 50,000 lililowekwa inavoonekana muda si mrefu litafikiwa na bila shaka wanaona watu wanavyochanga na wao wanafedheheka. Hawa waliokataza Lissu asifanyiwe maombi ndiyo leo wanajifanya wanataka kulipia matibabu popote na kwenye Hospitali yoyote ile duniani, KULIKONI?
Kwa niaba ya waziri ummwi, nawatakieni usiku mwema
 
Kukubali kusaidia na adui yako ni kukubali kwamba kakushinda kwa kila kitu. Je ni kweli ccm imetushinda kwa kila kitu?? Tukatae hapana tena big HAPANA
 
Maneno mengi wakati msaada mnataka....hela ya kumtibu marekani kamwe hamna ndio maana mliandika barua umoja wa ulaya....
Ujinga tuu ndio mwajua..
Mnatukera sana nyie watu, yaani ni kama vile serikali ni mali ya hicho chama chenu. Hivi huwa hamjui kama na sisi tusio CCM huwa tunalipa kodi?
 
CCM wanaendelea na mission yao kuhakikisha Lissu anakufa kwa namna yoyote wanayoona inafaa.
Lissu atauawa kwa michango yenu ya jero jero.Kubalini mlikosea sana kukataa matatibabu ya serikali kwa kisingizo cha kuwa atauawa.
Sasa hivi hali imekua ngumu,mgonjwa anahitajika kusafirishwa nje,uwezo wa madaktari wa kenya umefika ukomo,bili inazidi kupaa,badala ya hata mkakope benki au mtumie ruzuku kumpeleka ughaibuni,mnafanya siasa
 
Lissu atauawa kwa michango yenu ya jero jero.Kubalini mlikosea sana kukataa matatibabu ya serikali kwa kisingizo cha kuwa atauawa.
CCM inamuona Lissu ni msaliti na kila mara mnauliza "msaliti huwa anafanywa nini" na kila mtu anajua nini mnachomaanisha.

Sasa hivi hali imekua ngumu,mgonjwa anahitajika kusafirishwa nje,uwezo wa madaktari wa kenya umefika ukomo
Madaktari hawajafikia ukomo bali hamu ya CHADEMA ni kutumia teknolojia ya juu zaidi iliyopo duniani kwa sasa kuhusu watu walioshambuliwa na risasi. Hata kama mnafurahia kwa mateso ya Lissu lakini jueni kwamba mmemfanyia jambo baya sana binadamu mwenzenu!

bili inazidi kupaa,badala ya hata mkakope benki au mtumie ruzuku kumpeleka ughaibuni,mnafanya siasa
Hoja yako hii inaleta mkanganyiko, tatizo ni hela ama madaktari wa Kenya wamefikia ukomo wa utaalamu wao kwenye kumtibia Lissu!?
 
Hoja yako hii inaleta mkanganyiko, tatizo ni hela ama madaktari wa Kenya wamefikia ukomo wa utaalamu wao kwenye kumtibia Lissu!?
Mgonjwa anahitajika kupelekwa ughaibuni,uwezo wa madaktari wa kenya umefikia ukomo,pesa ndio shida,chadema wanaona aibu kurudi serikalini kwa sababu walitukana sana na kashfa kibao.
Dawa ni kumkabidhi mgonjwa kwa familia yake,Chadema wanamshikilia mgonjwa kwa kupata kiki ya kisiasa tu,ndio maana kila aendae kumuona mgonjwa lazima apige picha
Hivi watu wote wanaokwenda kuona wagonjwa wao muhimbili wakiamua kupiga selfie kila mtu na mgonjwa wake mitandaoni kutakuaje
 
Back
Top Bottom