Tuelimishane: Sakata la Mafuta ya kula (TRA vs. TBS) - Hiki ndicho kinachobishaniwa

Tuelimishane: Sakata la Mafuta ya kula (TRA vs. TBS) - Hiki ndicho kinachobishaniwa

Pamoja na uchambuzi wako mzuri lakini kuna sehemu haupo sawa. TRA wanang'ang'ania kuwa Mafuta haya SIYO GHAFI ni SAFI

Hivyo wangefunguka tu kuwa ni Mafuta ghafi ila uzalishaji wake sehemu kubwa imefanyika Indonesia hivyo ni GHAFI ila watayachaji kama SAFI.
Ni sawa mkuu. Sema mpaka sasa TRA hawajajitokeza kutoa ufafanuzi mkubwa.
Tumesikia tu wanasema ni mafuta safi. Ila naamini kama wakijitokeza kufafanua lazima hii hoja niliyoiandika wataifafanua.

Rules of Origin ni somo gumu na lenye utata kidogo. Nimelisoma na bado nalisoma. Najua challenge iliyopo na uchanga wa mifumo ya kodi nchini kwetu Tz.
 
Ghafi sio ghafi?? hapa ndio imedhihirisha namna elimu ya Tanzania ilivyo na shida..
Hahaa umeona. Kuna namna elimu yetu haijibu maswali au haitoi wataalam walioiva.
 
Mawese yetu kule Kigoma hatuna uwezo kuongeza uzalishaji ili tujitosheleze kwa mafuta? Hao wanazalisha ziada kwa nchi zao wana ardhi kuliko sisi?
Mawese ya Kigoma ni mazuri ila hakuna aliyewekeza sana zaidi ya Hayati Nyerere. Leo tunaagiza mawese kutoka Indonesia na Malaysia ..
Kwa taarifa yako hao Malaysia walikuja kuchukua mbegu ya Mawese Tanzania enzi za Nyerere na walijifunza kwetu. Kwani mawese ya Tz yalikuwa ndio bora duniani.
 
Ambacho hujasema mkuu ni kuwa nyundo ya TRA inalima kodi iliyotulia kwenye 'concentrate' kama 'final product'. Huo ubishani ni wote ni kodi tu.
Ndio msimamo wa TRA kwamba watoze kodi kama 'final product'. Kuna kanuni wanaitumia kubana hilo..
 
Huyo mfanyabiashara alikuwa mpigaji....hizo taasisi zinazobishana leo zote zilikuwa mfukoni kwake! Sasa kila moja anaogopa kutumbuliwa kwa hiyo wameamua kumtosa tajiri wao!


Hapa sasa patamu, inabidi serikali ifanye kazi backwards kubaini kiasi gani tulipoteza na namna gani tufidiwe na hao wacheza mchezo mchafu ili haki kwa umma itendeke, haileti maana watanzania kupteza haki zao kwasababu ya watu wachache
 
Habari wakuu.

Sasa kama nchi tuna sakata la mafuta ya kula. Yamekwama bandarini.

Msingi wa kukwama ni ubishani kati ya mamlaka za serikali hasa TRA vs. TBS
Mamlaka ya Mapato (TRA) yenye wataalam wa kodi na Shirika la Viwango (TBS) yenye wataalam wa viwango na ubora.

Kinachobishaniwa ni je yale yaliyopo bandarini ni mafuta "ghafi" au "safi"?.

Kabla sijaeleza zaidi natoa hitimisho hili. Hakuna namna TRA na TBS watakuja kukubaliana ktk hili hata ashuke malaika gani.

Sababu ni kwamba mtazamo wa kimantiki kati ya hizi taasisi mbili ni tofauti kabisa.

Katika hili serikali inajaribu kuunganisha ncha ya kaskazini na ncha ya kusini. Haitawezekana. Nitaeleza.

Mantiki ya "u-ghafi" na "u-safi" kwa TBS:
- TBS wanatumia kigezo kikubwa kimoja kuamua kwamba ni ghafi au ni safi. Kigezo hiki ni je haya mafuta yanafaa kwa mlaji au bado yanatakiwa kusafishwa zaidi ndio yafae kwa mlaji?!. Kwa sababu kiuhalisia mafuta yanayoletwa na hivi viwanda ni "concentrate" na huja kusafishwa na kuchujwa na kupakiwa Ndio yanakuwa tayari kwa mlaji; basi TBS wataamua kuwa ni "ghafi".

- "Concentrate" ya mafuta haifai kuliwa, hivyo kwa viwango ni "ghafi". Simple like that.

- Kisichofaa au ambacho hakijawa tayari kwa kula/kutumika kwa TBS ni lazima kiwe ghafi.

Mantiki ya "u-ghafi" na "u-safi" kwa TRA:
- Hawa ni wataalam wa kodi. Swali la wengi limekuwa wanawezaje kusema haya ni mafuta "ghafi"?. Wana maabara?.
Jibu ni kwamba hawana maabara lakini wanaweza kusema ni "ghafi" au "safi"

- Kwanza hawatumii maabara kuamua hilo. Wao wana kanuni moja ya "sharia ya forodha ya Afrika Mashariki". Hii ni kanuni ya "asili ya bidhaa ni nchi ipi?" kwa kiingereza ni EAC RULES OF ORIGIN

- Kiufupi sheria ama kanuni hii inasema "bidhaa itahesabika imetengenezwa katika nchi flani ikiwa sehemu kubwa ya uzalishaji imefanyika ktk nchi hiyo". Hii ni kanuni inayotumika kutafuta nchi ilikotengenezwa bidhaa pale ambapo bidhaa hiyo hutengenezwa ktk nchi A na kwenda kumalizia utengenezaji ktk nchi B.

Sasa kwenye ishu ya mafuta:
Kwa kuwa yanaagizwa huko Indonesia n.k yakiwa ni "concentrate" (yani yamekuwa processed kiasi) na kuja kumalizia utengenezaji Tz basi ni nchi ipi bidhaa hii itakuwa ime procesiwa zaidi?

Kama uzalishaji mkubwa umefanyika INDONESIA na kwa uchache huku Tz basi hiyo itahesabika yamezalishwa fully huko huko Indonesia. Na kodi itapigwa kama mafuta kamili hata kama kuna hatua chache za kumalizia huku Tz.

Huo Ndio ufafanuzi mdogo. Nimetumia lugha nyepesi zaidi ili kueleweka.

Kwa mantiki hizo hakuna namna TRA na TBS wakakubaliana. Haipo. Haipo. Haipo!

Ombi langu kwa serikali:
Iweke mifumo mizuri ili haya mambo yawe yanashughulikiwa na vyombo sahihi.

Wanaweza kwenda South Africa ambao wako vizuri sana kwenye mifumo ya "RULES OF ORIGIN" na wakajifunza.
Hapa Tz ni TCCIA (Tz Chamber of Commerce and Industries Association) ndo wenye jukumu hilo ingawa hawana wataalam na hawaaminiki pia.

Naishia hapo.

Ahsanteni.
Hapo kuhusu rules of origin na haya mafuta umeingia chaka hata haihusianii.... Kasome vizuri rules of origin
 
tatizo TRA wamemaliza kumkamua ng'ombe kila njia sasa waanza mchuna ngozi na hapo ndo tatizo linapoanzia kodi haitakiwi kumuumiza mlaji na hapo wasidhani kwa kuweka kodi kubwa kwe mafuta ghafi basi wanaoumia ni kina mohamed dewji hapana..hii kodi huwa inashuka kama kawaida kwa mlaji wa mwisho ambaye ni mwananchi wa kipato cha chini
Uko sahihi, lakini pia hauko sahihi vile vile, hapa care must be taken.
Main Motive ya any businessman/Viwanda ni Profit Maximization.
Na ki kanuni Profit Maximization huja pale tu ambapo una-lower expenses including Taxes na maximize revenue through prices, quantities manufactured, etc.

Sasa unaweza kumpiga kodi ndogo Mfanyabiashara/Manufacturer kwa vile tu mzigo ni Unfinished Goods, lakini je una uhakika gani kodi ndogo hiyo itaenda kuleta impact kwenye price ili nayo iwe ndogo? Je mfanyabiashara/Manufacturer hatoingia tamaa ya kupata Super Normal profit kwa kuendelea kutoza bei kubwa regardless kodi imeshuka?
 
Si mnasema wataalamu wetu wa TRA wako well qualified hivyo tutakuwa na wigo sawa ndani ya jumuia ya Amashariki! Hizo ndio indicators za awali kua tuendako jirani zetu watatukimbiza tu...kwa mambo yetu ya kuendekeza ukanjanja!
 
mtoa mada hebu nieleweshe, miaka ya nyuma walikua wanakubaliana vipi? au hayo mafuta yameanza kuagizwa hivi karibuni tu?
Mpango mzima wa kupiga kodi ya juu kwa imports za mafuta alipendekeza mkuu alipokua anazindua kiwanda cha mafuta ya alizeti lale Singida. Lengo ilikua kulinda viwanda vya ndani
 
Habari wakuu.

Sasa kama nchi tuna sakata la mafuta ya kula. Yamekwama bandarini.

Msingi wa kukwama ni ubishani kati ya mamlaka za serikali hasa TRA vs. TBS
Mamlaka ya Mapato (TRA) yenye wataalam wa kodi na Shirika la Viwango (TBS) yenye wataalam wa viwango na ubora.

Kinachobishaniwa ni je yale yaliyopo bandarini ni mafuta "ghafi" au "safi"?.

Kabla sijaeleza zaidi natoa hitimisho hili. Hakuna namna TRA na TBS watakuja kukubaliana ktk hili hata ashuke malaika gani.

Sababu ni kwamba mtazamo wa kimantiki kati ya hizi taasisi mbili ni tofauti kabisa.

Katika hili serikali inajaribu kuunganisha ncha ya kaskazini na ncha ya kusini. Haitawezekana. Nitaeleza.

Mantiki ya "u-ghafi" na "u-safi" kwa TBS:
- TBS wanatumia kigezo kikubwa kimoja kuamua kwamba ni ghafi au ni safi. Kigezo hiki ni je haya mafuta yanafaa kwa mlaji au bado yanatakiwa kusafishwa zaidi ndio yafae kwa mlaji?!. Kwa sababu kiuhalisia mafuta yanayoletwa na hivi viwanda ni "concentrate" na huja kusafishwa na kuchujwa na kupakiwa Ndio yanakuwa tayari kwa mlaji; basi TBS wataamua kuwa ni "ghafi".

- "Concentrate" ya mafuta haifai kuliwa, hivyo kwa viwango ni "ghafi". Simple like that.

- Kisichofaa au ambacho hakijawa tayari kwa kula/kutumika kwa TBS ni lazima kiwe ghafi.

Mantiki ya "u-ghafi" na "u-safi" kwa TRA:
- Hawa ni wataalam wa kodi. Swali la wengi limekuwa wanawezaje kusema haya ni mafuta "ghafi"?. Wana maabara?.
Jibu ni kwamba hawana maabara lakini wanaweza kusema ni "ghafi" au "safi"

- Kwanza hawatumii maabara kuamua hilo. Wao wana kanuni moja ya "sharia ya forodha ya Afrika Mashariki". Hii ni kanuni ya "asili ya bidhaa ni nchi ipi?" kwa kiingereza ni EAC RULES OF ORIGIN

- Kiufupi sheria ama kanuni hii inasema "bidhaa itahesabika imetengenezwa katika nchi flani ikiwa sehemu kubwa ya uzalishaji imefanyika ktk nchi hiyo". Hii ni kanuni inayotumika kutafuta nchi ilikotengenezwa bidhaa pale ambapo bidhaa hiyo hutengenezwa ktk nchi A na kwenda kumalizia utengenezaji ktk nchi B.

Sasa kwenye ishu ya mafuta:
Kwa kuwa yanaagizwa huko Indonesia n.k yakiwa ni "concentrate" (yani yamekuwa processed kiasi) na kuja kumalizia utengenezaji Tz basi ni nchi ipi bidhaa hii itakuwa ime procesiwa zaidi?

Kama uzalishaji mkubwa umefanyika INDONESIA na kwa uchache huku Tz basi hiyo itahesabika yamezalishwa fully huko huko Indonesia. Na kodi itapigwa kama mafuta kamili hata kama kuna hatua chache za kumalizia huku Tz.

Huo Ndio ufafanuzi mdogo. Nimetumia lugha nyepesi zaidi ili kueleweka.

Kwa mantiki hizo hakuna namna TRA na TBS wakakubaliana. Haipo. Haipo. Haipo!

Ombi langu kwa serikali:
Iweke mifumo mizuri ili haya mambo yawe yanashughulikiwa na vyombo sahihi.

Wanaweza kwenda South Africa ambao wako vizuri sana kwenye mifumo ya "RULES OF ORIGIN" na wakajifunza.
Hapa Tz ni TCCIA (Tz Chamber of Commerce and Industries Association) ndo wenye jukumu hilo ingawa hawana wataalam na hawaaminiki pia.

Naishia hapo.

Ahsanteni.
Kwani biwanda vyetu vinatengeneza mafuta ili kuyapeleka nchi zingine za Afrika Mashariki? Hii Rules of Origin ingekuwa na maana ikiwa unazalisha nchi moja ya Afrika Mashariki na kupeleka nchi ingine. Hata hivyo kwa mujibu wa sheria hizo za Afrika Mashariki zinaheshimu (na zinataka kutumika) maamuzi ya taasisi za viwango (TBS, KBS n.k.). Na taasisi hizi zinafanya kazi kulinganisha viwango vyake. Ni upuuzi kwa TRA kuanza kudefine vitu nje ya taasisi za kitaalamu za nchi zinazohusika katika suala husika.
 
Mpango mzima wa kupiga kodi ya juu kwa imports za mafuta alipendekeza mkuu alipokua anazindua kiwanda cha mafuta ya alizeti lale Singida. Lengo ilikua kulinda viwanda vya ndani
Sasa hivyo Viwanda vya Nyumbani vimejitosheleza kiasi gani?
Ukute baada ya hii crisis hao jamaa wa ndani wamepandisha bei ya Alizeti zao
 
Sasa hivyo Viwanda vya Nyumbani vimejitosheleza kiasi gani?
Ukute baada ya hii crisis hao jamaa wa ndani wamepandisha bei ya Alizeti zao
Kama ulijua vile!
Baada ya TRA na TBS kuoneshana umwamba na kusababisha uhaba wa mafuta ya kula, wazalishaji wa ndani wameficha stock waliyokua nayo na kutengeneza "UHABA" bandia wa mafuta ili kuongeza bei. Anaeumia ni mwananchi mlaji. Wangeacha system ijiendeshe km zamani wala kusingekua na shida kubwa
 
Hakuna hoja ya Rules of origin hapa. Rules of origin kazi yake ni kutambua mzigo unatoka wapi ili ijulikane kama una stahili preferential tarriffs ama sio.

Kwa mfano, kutokana na umoja wa kiforodha Africa Mashariki, mizigo ya iliyotengenezwa Kenya au Uganda itakuwa na viwango vyake vya kodi tofauti na mizigo kutoka nje ya umoja huo. Mizigo ya SADC vilevile.

Swala la mafuta kama ni ghafi au sio ghafi limeelezwa kwenye Common External Tarrifs..hiki ni kitabu ambacho kina bidhaa zote amabzo zinatambulika kwa namba maalum HS CODEs.

Mfano: Mafuta ya alizeti(sun flower oil)
Bidhaa HS CODE customs duty

Crude oil........................1512.11.00.................................10%
Refined oil......................1512.19.00...............................25%

Process ya kurefine ndo inaamua kama mafuta ni ghafi ama sio ghafi.

Process ya refine mafuta inahusisha kufanya chemical treatment ili kuondoa impurities na toxic substances. Process ina husisha bleaching, deodorization and cooling. Process inabadili muundo wa mafuta kikemikali.

Hivyo kinachotofautisha crude na refined ni chemical composition ambayo TBS ndo wanapima maabara.

Je kama ni ishu ya kemikali, TRA kwanini wanapinga majibu ya TBS ilhali hawana maabara? TRA wanaamini huko TBS huenda mtu kashkishwa cha juu na kutoa ripoti ambayo sio. Wanaamini process ya refining ishafanyika kwa asilimia kubwa, hivyo hayafai kuitwa ghafi. Naamini uchunguzi unaendelea.

SINTOFAHAMU:
1. Watu wanadhani mafuta ghafi hayafai kwa matumizi binadamu...yanafaa sana, tena yanashauriwa kitaalamu kwa afya. Ukiweza kukamua mafuta yako mwenyewe ya nazi au mawese, fanya hivyo. Kitaalamu yanaitwa virgin...kama ushaskia virgin olive oil.

2. Kwa nini sasa haya ya viwandani yawe refined? Inatokana na mazingira yaliyovunwa na kukamuliwa. Kwa vile yanavunwa na kukamuliwa on a commercial scale, yanakuwa na uchafu mwingi sana. Vile vile bila kurefine hayawezi kukaa mda mrefu bila kuharibika.

Nawasilisha
 
Kwani biwanda vyetu vinatengeneza mafuta ili kuyapeleka nchi zingine za Afrika Mashariki? Hii Rules of Origin ingekuwa na maana ikiwa unazalisha nchi moja ya Afrika Mashariki na kupeleka nchi ingine. Hata hivyo kwa mujibu wa sheria hizo za Afrika Mashariki zinaheshimu (na zinataka kutumika) maamuzi ya taasisi za viwango (TBS, KBS n.k.). Na taasisi hizi zinafanya kazi kulinganisha viwango vyake. Ni upuuzi kwa TRA kuanza kudefine vitu nje ya taasisi za kitaalamu za nchi zinazohusika katika suala husika.
Ishu ni kwamba kinachoagizwa ni "raw material" au ni "mafuta". Mtazamo wa kikodi unatofautiana na mtazamo wa ubora wa kiwango.
 
Kwa serikali makini kabisa inayojali maisha ya watu wake hususani wanyonge kama wanavyojinasibu hii sintofahamu ni ya kipumbavu sana! kinachotakiwa hapa kupewa preference ni maisha na afya za watanganyika kwa hiyo TBS asikilizwe, hoja ya tra ni kukomalia mapato tu na kuwakatili wananchi kwa upungufu wa mafuta!
Watanganyika???
 
Hakuna hoja ya Rules of origin hapa. Rules of origin kazi yake ni kutambua mzigo unatoka wapi ili ijulikane kama una stahili preferential tarriffs ama sio.

Kwa mfano, kutokana na umoja wa kiforodha Africa Mashariki, mizigo ya iliyotengenezwa Kenya au Uganda itakuwa na viwango vyake vya kodi tofauti na mizigo kutoka nje ya umoja huo. Mizigo ya SADC vilevile.

Swala la mafuta kama ni ghafi au sio ghafi limeelezwa kwenye Common External Tarrifs..hiki ni kitabu ambacho kina bidhaa zote amabzo zinatambulika kwa namba maalum HS CODEs.

Mfano: Mafuta ya alizeti(sun flower oil)
Bidhaa HS CODE customs duty

Crude oil........................1512.11.00.................................10%
Refined oil......................1512.19.00...............................25%

Process ya kurefine ndo inaamua kama mafuta ni ghafi ama sio ghafi.

Process ya refine mafuta inahusisha kufanya chemical treatment ili kuondoa impurities na toxic substances. Process ina husisha bleaching, deodorization and cooling. Process inabadili muundo wa mafuta kikemikali.

Hivyo kinachotofautisha crude na refined ni chemical composition ambayo TBS ndo wanapima maabara.

Je kama ni ishu ya kemikali, TRA kwanini wanapinga majibu ya TBS ilhali hawana maabara? TRA wanaamini huko TBS huenda mtu kashkishwa cha juu na kutoa ripoti ambayo sio. Wanaamini process ya refining ishafanyika kwa asilimia kubwa, hivyo hayafai kuitwa ghafi. Naamini uchunguzi unaendelea.

SINTOFAHAMU:
1. Watu wanadhani mafuta ghafi hayafai kwa matumizi binadamu...yanafaa sana, tena yanashauriwa kitaalamu kwa afya. Ukiweza kukamua mafuta yako mwenyewe ya nazi au mawese, fanya hivyo. Kitaalamu yanaitwa virgin...kama ushaskia virgin olive oil.

2. Kwa nini sasa haya ya viwandani yawe refined? Inatokana na mazingira yaliyovunwa na kukamuliwa. Kwa vile yanavunwa na kukamuliwa on a commercial scale, yanakuwa na uchafu mwingi sana. Vile vile bila kurefine hayawezi kukaa mda mrefu bila kuharibika.

Nawasilisha
Nikuulize swali la kukufikirisha.
Tukitoza kodi kama "crude oil" hayo mafuta yanakuja kuandikwa 'made in Tz'.
Na kama yakitozwa Kodi na kuingizwa kama 'refined oil' unafikiri watakuwa na haki ya kuandika made in Tz?!!!
Fikiria halafu uone RULES OF ORIGIN inavyo apply.

Karudie kusoma rules of origin zote na zile zonazozungumzia "goods made by raw materials from outside EAC Countries".

Utanielewa..
 
Naanza kuelewa huenda baada ya hii sheria ya mwaka 2017 shida imeanzia hapo labda udhaifu wa sheria watu waagizaji wanataka kupigia hapo.
swali je wakati sheria hii inatugwa hivi vyombo hawakujua hiyo crude ao refine itaegemea kweye vipimo vipi?

Kunashida somewhere.
Kuna shida everywhere mkuu
 
Hapo kuhusu rules of origin na haya mafuta umeingia chaka hata haihusianii.... Kasome vizuri rules of origin
Mkuu nipo sahihi. Naamini wewe umesoma hizo rules of origin zote..
Nakuomba ukarudie kusoma ile inayohusu "goods made by the product/raw materials from outside EAC countries" utanielewa.
Haya mafuta yakiingizwa kama crude oil na kutozwa kodi kama crude oil.. Wakija kiwandani wakisha chuja wataandika ni refined oil na hapo zile "four digit HS Code" zikishabadilika basi wataandika ni mafuta "made in Tz".

Lakini yakitozwa kodi kama refined oil na kuingizwa kama refined oil basi wakija kiwandani baada ya kuchuja na kupaki yatabakia ina the same "four digit HS Code" na hawatakuwa na haki ya kuandika "made in Tz"..

Hebu jaribu kupitia ujue "Tax impact ninayokueleza".

Rules of origin ni somo pana. Tulia . Soma tena.

Soma kuelimika na sio tofauti.
 
Back
Top Bottom