Tuelimishane namna ya kununua simu mpya but a midrange

Mi napenda kujua tu one plus nord mpya bei yake na duka naloweza kuipata
 
Hello: Nina 450k nataka kununua simu nzuri kulingana na bajeti hii. Je, kati ya:

1. Infinix Note 10 (RAM: 4GB, ROM: 128GB, Bettry capacity: 5000 mAh, Android 11, size 6.95 inches, IPS LCD Display, Helio G85 Chipset, Triple Rear and 16MP Selfie Camera) Au

2. Oppo A31. (RAM: 4GB, ROM: 128GB, Bettry: 4230 mAh, Display: IPS LCD, 6.5 inches, Camera: triple 12MP, 2MP, 2MP.
OS: Android 9.0).

Nichukue simu ipi?, je aina gani nyingine ya simu zenye specifications kama hizi 2 naweza kununua kwa bajeti isiyozidi 450k ?

Nawasilisha.
 
Huwa mimi kwenye ununuzi wa simu kitu cha kwanza ninachoangalia ni soc, ukipatia hapa then ndio unaanza kuangalia mambo mengine.

Kwenye Upper midrange simu za laki 7 mpaka 1m hivi kwa Snapdragon angalia sd 778G ni soc kali sana, Huhitaji battery kubwa hata 4000mah inatosha simu itakaa na chaji sana, alternative kwa Mediatek ni Dimensity 920/900.

Kwa simu za laki 4 na kitu hadi laki 6 hivi ambayo nahisi ni Budget yako Tafuta Snapdragon 695 ni soc nzuri sana nayo, ila ina weakness kubwa hairecord 4k video, hii soc ni efficient sana simu zake zinakaa na Charge pia ina nguvu sana compare na competition at Same price. Alternative yake ni Mediatek Dimensity 810.

Kwa laki 3 mpaka 4 hapa kama unapata Snapdragon 680 ni vyema, Otherwise Mediatek G80/G85/G88 si mbaya. Pia zipo Unisoc T606/610/700 etc nazo ni alternative nzuri.

Kwa chini ya laki 2 nusu unisoc T310 ina make sense zaidi sema simu chache sana wanatumia, Most of time ni eneo la kukimbia hakuna simu nzuri kivile, hope Samsung A03 itakuwa eneo hili (sio A03s)

Ukishapata soc of your choice sana una narrow down Choice zako. Mfano una 1m, Sd 778G ipo karibia Brand zote Samsung Ana A52s na M52, Xioami ana Mi 11 lite 5g ne, Kuna realme GT master etc. Kutokana na matumizi ndio unachagua inayokidhi, kama unakaa field wiki kadhaa huna umeme battery life itakua priority, upo dukani picha unapiga sana Camera itakuwa priority etc.
Ndugu hebu nisaidie hapa in deep maana nimeshindwa kufanya chaguo sahihi REALME 9 PRO PLUS vs REDMI NOTE 11 PRO PLUS, ingia deep kidogo
 
Ndugu hebu nisaidie hapa in deep maana nimeshindwa kufanya chaguo sahihi REALME 9 PRO PLUS vs REDMI NOTE 11 PRO PLUS, ingia deep kidogo
Unaweza ukasoma specs hapa


Hio realme ina camera nzuri sana japo
Ukiangalia specs kwa namba Redmi ina mp nyingi.

Perfomance itakuwa sawa sababu zote mbili zinatumia dimensity 920.

Redmi yenyewe ina memory card, faster charging na Display nzuri.

Kwa muono wangu mkuu zote mbili hazina Issue, zinauzwa Bei Ghali sana, most of Time zinakaribia milioni ama zinazidi milioni.

Hizo ni midrange za kawaida sio hata upper midrange then zinauzwa bei sawa na flagship ama premium midrange.
 
chief..!! ebu tuondoen tongotongo na sisi tusiejua hayo mambo maana mimi binafsi naskiaga tu soc , snapdragon, mediatex , amouldw nk

lakini maneno yote hayo sijui nini tafsiri yake

sasa kwafaida yangu na wengineo mngetupa msaada ili tuweze kufahamu
 
Back
Top Bottom