Tuelimishane kuhusu Kilimo cha Pilipili Manga, kuanzia mbegu bora, magonjwa, utaalamu mpaka masoko

M-pesa

JF-Expert Member
Sep 4, 2011
602
151
Mwenye kujua hali ya hewa inayoruhusu hili zao kustawi na kuzaa kwa wingi tafadhali anijulishe.

Na ni sehemu gani Tanzania hili zao linastawishwa kwa wingi?

Asanteni


 
mwenye kujua hali ya hewa inayoruhusu hili zao kustawi na kuzaa kwa wingi tafadhali anijulishe. Na ni sehemu gani Tanzania hili zao linastawishwa kwa wingi?
Asanteni

Pili pili hiyo inamea na kuzaa sana milima ya Matombo huko Mvomero. tatizo barabara ya kwenda hapo mlimani, ni mbaya sana siku mvua ikinyesha.
 

Jumuiya ya Wakulima wa Kilimo Hai Usambara Mashariki (JUWAKIHUMA) ni chama kinachounganisha vijiji sita vilivyopo milimani Usambara Mashariki wilaya ya Handeni, mkoani Tanga.

Wakulima wa maeneo haya wanalima sana mazao ya viungo vya chakula hasa pilipili mtama, iliki na karafuu. Karafuu inayolimwa eneo hili ubora wake ni mkubwa kuliko karafuu inayolimwa Pemba na Unguja. Pia eneo hili yapo mashamba makubwa ya serikali ya miti ya mipira, iliyokuwa inatumika kama malighafi kwa kiwanda cha matairi cha General Tyre, Arusha.

Pilipili mtama ndilo zao la kwanza nchini lenye bei nzuri kwenye soko la ndani, bei yake kwa sasa ni kati ya shilingi 400,000/= hadi 600,000/= kwa gunia la kilo 100, sokoni Kariakoo.

Serikali ya Marekani kupitia shirika lake la misaada la USAID limewasaidia sana wakulima wa vijiji hivi sita, kuendeleza mazao yao, kiasi kwamba hali ya maisha ya wakulima imebadilika sana, na kila eneo utakalopita utakuta wakulima wanapanua mashamba na vitalu vya miche mbalimbali vikiwa mashambani, vikisubiri msimu wa kupanda.


https://lh3.googleusercontent.com/-f5DbakWscH8/Sq-VJDcPeII/AAAAAAAAO2E/_CMOVEuT4gI/s800/P1020187.JPG


https://lh6.googleusercontent.com/-RwmEeWtO59c/Sq-VMfTJ5oI/AAAAAAAAO2Q/CdZHm0UYOW0/s800/P1060002.JPG


https://lh6.googleusercontent.com/-I_huoY_M6Vk/Sq-VKarFQuI/AAAAAAAAO2I/cr4l1zb9pww/s800/P1020195.JPG
 
Mrdash1 umenichekesha sana..............umenikumbusha mara ya kwanza kulisikia jina hili likitamkwa na watu wazima nilipata wakati mgumu kidogo.

Tukirudi kwenye maada ni maeneo managapi nchini zao hili linaweza kustawishwa?
 
Mimi ni mfanyabiashara mkubwa wa pilipili manga ila kikwazo kinachokwamisha biashara hii hapa kwetu Tanzania hamna soko la uhakika.

Kama kuna mtu yupo tayari na aina hii ya viungo basi tuonane tufanye biashara!

0712720080 au +254721207560
 
Wadau jamvini habari zenu?

Kwa yeyeto mwenye kujua hivi vitu vinatoka mkoa gani kwa wingi? Maana nahitaji kwa wingi (tons) au kwa mtu mwenye kuweza kusupply kwa wingi tuwasiliane kwa maelezo zaidi.
 
Wadau jamvini habari zenu??
Kwa yeyeto mwenye kujua hivi vitu vinatoka mkoa gani kwa wingi? Maana nahitaji kwa wingi (tons) au kwa mtu mwenye kuweza kusupply kwa wingi tuwasiliane kwa maelezo zaidi.

Call:

0784 887 599
0784 422 571
0713 769 379
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…