TUCTA kujadili kima cha chini cha mshahara 2019

TUCTA kujadili kima cha chini cha mshahara 2019

Haya mambo yashaongelewa sana, ila inaonekana utekelezaji wake ni mgumu...

Kama tulishindwa kufanya kipindi kile ambacho angalau mambo yalikua mambo, unadhani kipindi hiki itawezekana kweli...


Cc: mahondaw
 
1.) Sijasema washindwe kutwa nzima halafu wasilipwe, ninachosema ni wafanye kazi ili kujipatia riziki. (Wafanye kazi).

2.) Hata huyo wa nyumbani hafanyi kazi, ni anafanyishwa kazi na kupewa fadhila mwisho wa siku (ni fadhila tu, si haki yake)

3.).Sijasema kodi yangu isitumike kufadhili wafanyishwa kazi wasiotaka kufanya kazi.Ila tu, naguswa. WATUMISHI WA UMMA NI MIZIGO KWA TAIFA, NDIO MAANA MHESHIMIWA NI MGUMU KUONGEZA MIZIGO, ANAJUA HILI, ANA UELEWA MPANA SANA!
Hata kutangaza ajira ni fadhila tu.

Jitu linazunguka ulaya kuchafua nchi halafu linataka lilipwe mshahara for what?! Lingine linaenda kuuguza bila kuaga, halafu mshahara uingie tu, for what?! Mizigo tu..!!!!

Imagine mtu eti anakuletea orodha ya majukumu yako ya kazi kwenye kikaratasi, are you a robot? Au wewe ni zezeta? Mwisho wa siku nyie wapenda vitonga tutawa- replace wote kabisa na machines/ computers / robots, ndio akili itawakaa sawa. Tumeshaanza na ATM's na sekta nyingine mashine zinaendea kuwapunguza, mwishowe mtakuwa obsolete! Nani anataka mizigo? Tutatumia robots na machines ambazo hazidai mishahara! Hadi magari ya serikali yataendeshwa computer robots, hakuna msalie mtume, wote tutafanya kazi sasa!
Hao uliowatolea mfano kwa mfumo na taratibu za nchi hii siyo watumishi wa umma,unajichanganya sana ama kwasababu huelewi unachojadili,au wewe nawe ni sehemu ya maroboti hayo.Japan ambako kuna teknolojia ya hali ya juu kabisa ulimwenguni humu, na wanaroboti wa kutosha, lakini hadi sasa bado wanawahitaji watumishi wa umma na bado wanao hao watumikishwa wako,inakuwaje kwa Tanzania?.Au na wewe uko programmed kwa ubishi kama hao roboti wako?

Nimekuuliza ulishawahi kuishughulisha akili yako kufikiria nchi isiyokuwa na watumishi wa umma itakavyokuwa?.Wala hujajibu.Kwenye uzi wako wa kwanza uliwapa wito watumishi wa umma waache kutumikishwa ,na waje waungane na wewe kufanya kazi.Ndipo na mimi nakuuliza unajua huduma zinazo tolewa na hao unaowahita watumikishwa wa umma?.

Naomba ujielimishe juu ya utumishi wa umma, na uelewe nani ni watumishi wa umma,na ujielimishe vya kutosha halafu ndio urudi tena kuleta ubishi wako.Maana yake tukieendelea utasema hata askari polisi,magereza,uhamiaji,na JWTZ nao watumishi wa umma.

Mwisho Taifa halijawahi kuwachukulia watumishi wake wa umma kama mzigo,kwasababu serikali ndo huwaajiri kwa matakwa na utashi wake.Kwa mfano karibuni tu serikali imetangaza nafasi za ajira ya walimu wa sayansi,kwasababu kuna mahitaji ya walimu hao kwenye shule za umma,halafu hiyohiyo serikali ije iseme watumishi hao ni mizigo.Labda hiyo serikali ingelikuwa na watu wa size na type yako.Mishahara watakuja kuongezewa tu kama si mwaka huu hata mwakani Mheshimiwa Rais alishawaahidi kwani ni wajibu wa serikali kuwahudumia watumishi wake.
 
Hao uliowatolea mfano kwa mfumo na taratibu za nchi hii siyo watumishi wa umma,unajichanganya sana ama kwasababu huelewi unachojadili,au wewe nawe ni sehemu ya maroboti hayo.Japan ambako kuna teknolojia ya hali ya juu kabisa ulimwenguni humu, na wanaroboti wa kutosha, lakini hadi sasa bado wanawahitaji watumishi wa umma na bado wanao hao watumikishwa wako,inakuwaje kwa Tanzania?.Au na wewe uko programmed kwa ubishi kama hao roboti wako?

Nimekuuliza ulishawahi kuishughulisha akili yako kufikiria nchi isiyokuwa na watumishi wa umma itakavyokuwa?.Wala hujajibu.Kwenye uzi wako wa kwanza uliwapa wito watumishi wa umma waache kutumikishwa ,na waje waungane na wewe kufanya kazi.Ndipo na mimi nakuuliza unajua huduma zinazo tolewa na hao unaowahita watumikishwa wa umma?.

Naomba ujielimishe juu ya utumishi wa umma, na uelewe nani ni watumishi wa umma,na ujielimishe vya kutosha halafu ndio urudi tena kuleta ubishi wako.Maana yake tukieendelea utasema hata askari polisi,magereza,uhamiaji,na JWTZ nao watumishi wa umma.

Mwisho Taifa halijawahi kuwachukulia watumishi wake wa umma kama mzigo,kwasababu serikali ndo huwaajiri kwa matakwa na utashi wake.Kwa mfano karibuni tu serikali imetangaza nafasi za ajira ya walimu wa sayansi,kwasababu kuna mahitaji ya walimu hao kwenye shule za umma,halafu hiyohiyo serikali ije iseme watumishi hao ni mizigo.Labda hiyo serikali ingelikuwa na watu wa size na type yako.Mishahara watakuja kuongezewa tu kama si mwaka huu hata mwakani Mheshimiwa Rais alishawaahidi kwani ni wajibu wa serikali kuwahudumia watumishi wake.
Kabla sijajibu hizo porojo, je , huwa unawalipa wewe kwa pesa zako binafsi au wanalipwa na pesa za umma?

Pia kazi haigombaniwi kama mpira wa kona, ila mtelezo ndio watu wanagombania, ona mwenyewe
https://www.jamiiforums.com/threads/walimu-91-000-wagombania-nafasi-4-500.1566014/
 
Kabla sijajibu hizo porojo, je , huwa unawalipa wewe kwa pesa zako binafsi au wanalipwa na pesa za umma?

Pia kazi haigombaniwi kama mpira wa kona, ila mtelezo ndio watu wanagombania, ona mwenyewe
https://www.jamiiforums.com/threads/walimu-91-000-wagombania-nafasi-4-500.1566014/
Kwanza umehama mada,pili wewe ulitaka wasomee ualimu halafu waje kulima na wewe?,wameomba kazi waliyo somea kosa hakuna.UELEWA wako ni wa kijiweni tafuta wa aina yako mjadiliane.
 
Mie wakati naoa Mke wa pili 1994 nilizungumza nae Pembeni nikamwambia uwezo wangu wa kulipa Mahari Ni kiasi gani

Alichofanya kilipoitishwa kikao Cha Familia Yao kupendekeza Mahari aliwasilisha kiwango ambacho Mie naweza kulipa Kama ndio proposal yake


Iliporudi kwangu nami nikakubali Bila ya kusita Familia Yao ikaona imepata Mkwe Kweli Kweli maana siku burgain Mahari waliyopendekeza bali nililipia yote kwa mkupuo mmoja


Vilaza watasema nimetoka Nje ya Mada kwa Kuwa mjadala Ni nyongeza ya Mshahara Mie nazungumzia Posa
Nimekuelewa
 
Tutaisoma namba kwa kweli, wasiache PAYE ile percent ifanyiwe marekebisho, hiawezekani mwajiriwa analipa kodi kubwa kuliko hata mfanyabiashara wa kati

Happiness is a lifestyle
Dunisni kote employees ndiyo hulips Kofi kubws....u must psy
 
Hivi lile tamko la rais kuhusu wastaafu na mafao yao
pamoja na wafanyakazi wa sekta maalum za migodi
kupewa fao la kujitoa lilishafanyiwa kazi?
kama bado ni afadhari wakajikita hapo badala ya
kuja kila siku na mapendekezo,kama marehemu mtikilia
 
"Ukisoma katiba vizuri kwa umakini,Magufuri una mamlaka makubwa sana ukiwa Rais waJamhuri ya Muungano wa Tanzania,Ili kutimiza malengo yako kwa nchi,narudia malengo yako kama Rais kwa nchi si kwa mwananchi mmojammoja,nakushauri mshahara kwa watumishi wa umma uongezwe tarehe 22.01.2020"
 
Back
Top Bottom