TUCTA: Kima cha chini cha mshahara kiwe 970,000

Analogia Malenga

Platinum Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,292
Reaction score
10,842
Kaimu Katibu Mkuu wa TUCTA amesema wamefanya tafiti kubaini kiwango cha mshahara ambacho kinaweza kumtosha mtumishi kuendesha maisha yake.

Kutokana na Tafiti yao wamependekeza kiwango cha chini mshahara kiwe Tsh. 970,000 kutokana na gharama za maisha za sasa.

Hayo yamesemwa siku ya maadhimisho ya siku ya wafanyakazi ambayo kitaifa yamefanyika katika uwanja wa CCM Kirumba Mwanza.



Pia soma: LIVE - Mei Mosi Mwanza: Rais Samia ahutubia, aahidi kuongeza mishahara kuanzia mwakani
 

Mtumishi yupi?
 
Mhh hapo TUCTA mmezid na huo utafit hua mnafanyia wapi jaman mbona mtaani kwetu mara ya mwisho ni watu wa sensa tuh ndio wamepita
 
Hii ni nchi TAJIRI. Kwhy kima cha chini cha mshahara (KCCM) kiwe sawa na mshahara wa mbunge mwenye elimu ya darasa la Saba kfn Kibajaji au Msukuma, 2m/- kwa mwezi.
 
Waliwahi kupambania sh 350,000 ndo iwe kima cha chini kwa miaka takribani yote ya Mkwere, wakashindwa. Ebu fikiria walishindwa kumshawishi mkwere kuidhinisha hiyo 350,000, kwa jiwe walipendekeza kweli? Ngapi?

970,000 kwa mtu wa idara gani sasa? Wakisema Tanesco, sitashangaa ila wa wizarani nitasita kidogo.

Waache kuwaibia wafanyakazi, watengeneze tu chama cha siasa
 
Watumishi wa umma wanajiona kama wapo wenyewe tu sijui hawajui ni 0.6% ya raia wote? Huu upuuzi wa kudai laki 9.7 ni Seriikali gani hii itakayolipa hyo pesa? Hv wanajua impact ya mshahara kupanda huku mitaani ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…