KalamuTena
JF-Expert Member
- Jul 7, 2018
- 13,181
- 17,174
"Kuchora mstari juu ya ushoga?". Njia pekee na ya uhakika iliyopo ni kuwaondoa wote kwa njia yoyote inayowezekana, hata ikibidi kuwaua. Je, upo tayari kufanya hivyo? Na hata ukiwaua waliopo, wengine wataendelea kuzaliwa. Hawa walikuwepo enzi na enzi. Kutowajua au kuwasikia haina maana kuwa hawakuwepo. Kilichobadilika sasa ni kuwa inazidi kuwa ngumu kuwanyamazisha.
Vinginevyo ni kuwakandamiza ili ionekane hawapo; lakini hii itakuwa ni 'aspirin' tu ya kuondoa maumivu kwa muda ugonjwa ukiendelea kukorea. Utakapofikia kiasi chake utafumburuka tu utake usitake.
Tusitake kujifanya kama hatujui historia ya mambo haya. Hata huko majuu, mahafizina bado wanajiapiza kuwa 'ushoga' haukubaliki, lakini unaendelea tu kufumburuka.
Ni kiasi cha muda tu, sote tutaanza kuwa tunatazama pembeni wakati jamaa wakisherehekea uhuru wao mitaani.
Vinginevyo ni kuwakandamiza ili ionekane hawapo; lakini hii itakuwa ni 'aspirin' tu ya kuondoa maumivu kwa muda ugonjwa ukiendelea kukorea. Utakapofikia kiasi chake utafumburuka tu utake usitake.
Tusitake kujifanya kama hatujui historia ya mambo haya. Hata huko majuu, mahafizina bado wanajiapiza kuwa 'ushoga' haukubaliki, lakini unaendelea tu kufumburuka.
Ni kiasi cha muda tu, sote tutaanza kuwa tunatazama pembeni wakati jamaa wakisherehekea uhuru wao mitaani.