Tuangalie namna nzuri ya kudai Tume Huru

Abdul Nondo

JF-Expert Member
Oct 28, 2016
515
2,874
Suala la tume huru ni suala nyeti sana ,sio suala la vyama vya siasa tuu ,sio suala la chama kimoja kimoja tuu, sio suala la wanaharakati tu, sio suala la Azaki tuu,ni suala jumuishi linalotakiwa kujumuisha watu wote na taasisi zote.

Ila ili huu ujumuishi (inclusiveness) uweze kufanikiwa kirahisi na kwa uimara zaidi ni vyema sasa wale main actors (MA) katika sphere hii kuanza mchakato wakulifanya suala hili kuwa jumuishi na sio binafsi. Main actors ni vyama vya siasa.

Tusikimbilie kusema " *suala hili sio la vyama tuu ,tusitegemee vyama.Bali hata wewe dai tume huru* " Ndio ninadai na tunadai Ila kwa mpangilio upi ? ,Lazima kuwe na mpangilio na uratibu wa pamoja ili sauti zetu zote zisikie kwa pamoja ,sauti zisizo na mpangilio ni fujo.Vyama vya siasa hili ni jukumu lao kubwa kuratibu kuweka watu na taasisi pamoja.

Kilichoniuma sana ni kuona pia waziri mkuu akijibu swali la Mh.@freemanmbowetz kivyepesi kabisa kama kauli au msimamo wa serikali alafu wala hakuna mjadala ulioibuka kumpinga na kumkosoa waziri mkuu juu ya kauli yake.

Watu walichukulia simple tuu ,alafu kesho yake naendelea kuona watu baadhi wanapost tume huru ,tume huru .Mzizi ungetakiwa kwa umoja kauli ya waziri mkuu kama kauli ya serikali kusema" tuna tume huru inayofanya kazi bila kuingiliwa "siku ile ile hii kauli ilipaswa kuoingwa kila Kona na watu wote.

Na kuonesha namna gani kauli yake ni ya upotoshaji ,nilijiaribu kuandika kuonesha hili Ila watu hawajali, watu wanadhani tume huru ni agenda ya kikundi fulani kwamba ukisema ,utaonekana umeiba agenda ya kikundi fulani na hicho kikundi fulani kitaona umeiba agenda yao,this is childish.

Tunaomba vyama pinzani (opposition parties) na Mabaraza ya vijana yote ya vyama pinzani (The party Youth leagues /wings) nchini miongoni mwao kwanza yangekutana haraka yakajadili namna ya ku mobilize vijana wao nchi nzima, namna ya kushirikiana na Azaki , taasisi za dini na wanaharakati na watu wengine.

Ili kuwe na Agenda moja ya kitaifa kuelekea uchaguzi mkuu.Lazima uratibu huu ufanyike sababu ni nje ya muda ingawa sote kwa pamoja hatujachelewa.tulitarajia this movement ya kudai Tume huru ingeanza muda miaka nyuma 2016/2017/2018/2019 kwa Sasa 2020 jambo hili linahitaji umakini na umoja wa hali ya juu sababu huu mwaka una mambo mengi sana.


Azaki pia hazipaswi kubakizwa nyuma ,zinapaswa kushiriki kikamilifu ingawa ni Azaki chache zipo active zingine nyingi zina hofu kwamba kudai Tume huru ni kujihusisha na siasa ,sababu Agenda hiyo ni ya wanasiasa nadhani kama kuna wanaodhani hayo ,wana uwelewa mdogo tuu wa mambo .Tume huru ya uchaguzi ni moja ya nyenzo kubwa ya uchaguzi huru na haki, uchaguzi huru na haki ni moja ya msingi mkubwa wa Demokrasia .Demokrasia kwa upana wake inajumuisha haki za binadamu katika upande wa haki za kisiasa na kiraia (Civil rights and political liberty).Kama Azaki zinahisi kudai tume huru ni jukumu la vyama vya siasa tuu zinajipotosha zenyewe.

Sisi wananchi,lazima tutambue tume huru ndio nyenzo ya uchaguzi huru na haki, uchaguzi huru na haki ndio mlinzi mkubwa wa kura yako,ndio msingi wa mamlaka kwa kiongozi umpendaye ,ndio mlinzi wa uzito wa kura yako kwa kiongozi umtakae,mara nyingi sisi wananchi aidha CCM, ACT , Chadema ,NCCR au chama chochote,hata wasio na chama huwa tunaona mambo ya tume huru ni mambo ya vyama vya siasa hii sio kweli.Haya mambo yanatuhusu sote.

Kupitia uwepo wa tume huru ya uchaguzi ,tutakuwa na uchaguzi huru na haki ,kupitia uchaguzi huru na haki tutapata kuchagua viongozi tunaowataka ,watakaochaguliwa kwa uzito wa kura zetu . Viongozi hawa watakuwa wanyenyekevu kwetu wananchi na watakuwa wawajibikaji na ataongoza baada ya yeye kupata baraka na mamlaka kutoka kwetu, soma ibara ya 8(a) katiba yetu ya 1977, Kiongozi huyo sababu amechaguliwa kwa uchaguzi wa haki atawiwa kututumikia kwa ustawi wetu sisi wananchi (Soma ibara ya 8 b ya katiba ).

Wananchi bila kujali vyama vyetu,lazima tutambue kuwa serikali ya sasa haitaki kusikia neno tume huru sababu ya maslahi yao binafsi ,sababu wanahisi ndio njia ya wao kupoteza vyeo vyao,ndio maana kwa kujihami wanatangaza kufuta mfumo wa vyama vingi kwa njia mbali mbali .

a)kuzuis mikutano iliyopo kisheria kwa vyama vingine.
b)Kufungulia kesi viongozi vyama pinzani.
c).Kutumia polisi katika chaguzi.
d)Kununua wawakilishi wa wananchi kutoka vyama vingine.
e) Kufanya figisu katika chaguzi (Manipulations /riggings).
f)kutosikia neno tume huru .
g) kutishia watu wenye mlengo wa upinzani.

Lengo ni kuifanya Tanzania kuwa nchi ya chama kimoja "De facto single party state " ndio maana kauli kila siku ,tutafuta vyama pinzani na wananchi tunacheka ,kufuta vyama pinzani ni kufuta mfumo wa vyama vingi.

Na hayo Serikali hii ya CCM inaweza kuyatimiza bila uwoga kama sote tukiendelea kutoa meno nje na kuchekacheka.Pius Msekwa katika kitabu chake cha "The Reflections on the first Decade of Multiparty Politics in Tanzania" kurasa ya 327 "The future of Multipartism in Tanzania will depend on these three factors a)The Strength and seriousness of Political parties (b) the delivery of free and fair elections (c) A vibrant Parliament . Yaani uhai wa vyama vingi unategemea vitu vitatu uimara na nguvu kwa vyama pinzani (umoja),(b) uchaguzi huru na haki (c)Bunge machachari.

Yaani kama vya pinzani visipokuwa imara na mshikamano kipindi hiki kwa kuratibu vyema inclusiveness ya kudai Tume huru na namna nzuri ya kushiriki uchaguzi mkuu.Hakika Demokrasia yetu itazikwa rasmi.

Hatupaswi kuombea hayo ,tunatumai mambo yataenda sawa sawia kwa vyama vyetu kuwa imara ,kuwa na uratibu imara pia kuzidisha mahusiano mazuri miongoni mwao.

Shukrani.

Abdul Nondo.
0772151432.
abdulnondo10@gmail.com

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani kama vya pinzani visipokuwa imara na mshikamano kipindi hiki kwa kuratibu vyema inclusiveness ya kudai Tume huru na namna nzuri ya kushiriki uchaguzi mkuu.Hakika Demokrasia yetu itazikwa rasmi.
uimara mbele ya Risasi, kupotezwa, kubambikiwa kesi, uhujumu uchumi, money laundering... tunastukaje hapo? Idd Amin alikuwa anaua kila mpinzani, ndicho kinachofanyika hapa! Bila nguvu ya nje tutateseka sana! Idd Amin angelikuwa bado anatawala kama siyo Nyerere!
 
Sio rahisi fisimu kuachia mamlaka kwa kisingizio Cha tume huru. Wenzetu wanakuwaga na sauti moja linapokuja suala la kutetea chama Chao Cha kijani pale wanapoelekea uchaguzi mkuu.

Vyama vya upinzani viwekeze Kwanza kwa watu (wananchi) kabla ya kuwaza tume huru ya uchaguzi. Tafuta Kwanza namna ya kuondoa fikra na maarifa madogo yaliyoko kwenye vichwa vya watanzania wengi ndio uwaze umoja wa kutafuta tume huru.
 
Tawala za ki Africa, hua mpaka watu waumizane, ndiyo wanaona haja ya kukaa kujadili jambo. Na kwetu hapa watawala wetu hawaoni haja ya kutumia amani kuleta mabadiliko.

Tume huru ni mkuki kwa matendo ya wana CCM dhidi ya vyombo vya dola na vya maamuzi. Hawaoni leo umuhimu wake. Kwao tume hii ya remote control ni huru

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo unaandikaga kitabu mdogoetu... Tusome kama tunamitihani! Embu put it in a nutshell twendesawa
 
Kilichoniuma sana ni kuona pia waziri mkuu akijibu swali la Mh.@freemanmbowetz kivyepesi kabisa kama kauli au msimamo wa serikali alafu wala hakuna mjadala ulioibuka kumpinga na kumkosoa waziri mkuu juu ya kauli yake.
Hapo sasa!

Samahani sana mkuu Abdul Nondo, sio nia yangu kuuliza swali hili ambalo linatatiza na kimsingi huwa sipendi kuwaweka watu katika mafungu kama haya.

Swali ni hili: je, nawe asili yako ni Kigoma?
Namtambua Kabouru (sijui kama jina ni sawa?), Zitto, Kafulila, nani tena, yule diwani aliyenyang'anywa ubunge halafu akanunuliwa..., nani tena? Simbachawene?

Wote, katika kujieleza na kuwasilisha hoja, bila kujali mengine yote..., wamejipambanua kuwa vizuri sana!
Nawe naona upo kwenye mwelekeo huo. Huko Kigoma kuna shule/walimu maalum wanaofanya kazi hii ya kuwaandaa watu?

Hiyo mistari miwili uliyoweka kwenye mada yako, na nimeinukuu hapo juu, imenigusa na kunifanya niulize haya maswali.

Na siyo lazima unijibu, kwa sababu ukweli ni kwamba sitaki kujua unakotokea maadam najua unatokea Tanzania basi inatosha.

Samahani tena, kwa sababu sijachangia chochote kuhusu mistari yako hiyo miwili ambayo ndiyo inayobeba uzito wa mada yako, na watu hawawezi kuichangia ipasavyo hapa JF; je, na huko kwenye vyama , na sehemu zingine ulizotaja je, nao hawaoni uzito wake?
 
Hata sisi hatuwezi sikiliza mtu mpumbavu

Uwepo wa wapumbavu kama wewe ndio mawazo kama yako yanatokea

Ingawa Baba yako hana Msaada kwetu lakini kuzaa mpumbavu kama wewe ni hasara kwa taifa
Siwezi kukaa kudai tume huru wakati hanisaidii chochote katika maisha yangu! Kama tume hii sio huru wabunge wenu wangejiuzulu maana walishinda kwa tume hyohyo isiyo huru.
 
Siwezi kukaa kudai tume huru wakati hanisaidii chochote katika maisha yangu! Kama tume hii sio huru wabunge wenu wangejiuzulu maana walishinda kwa tume hyohyo isiyo huru.

Ahaa ahaaa acha nicheke kwa nguvu, ni sawa na kusema VAR ya nini kwenye soka wakati bingwa amekuwa akipatikana kila mashindano fulani yanapofanyika? Hapo unataka kusema wote waliochukua kombe kabla ya mfumo wa VAR kwenye soka warudishe huo ushindi maana walishinda bila kuwa na mfumo wa VAR. Ni hivi, tume huru ya uchaguzi ni lazima na hilo halina mjadala. Na iwapo haitapatikana kwa njia ya amani, basi tutaleta rabsha itakayowaleta wazungu wafanye watakalo.
 
Hata sisi hatuwezi sikiliza mtu mpumbavu

Uwepo wa wapumbavu kama wewe ndio mawazo kama yako yanatokea

Ingawa Baba yako hana Msaada kwetu lakini kuzaa mpumbavu kama wewe ni hasara kwa taifa

Angalia vizuri jibu la huyu jamaa, ni kama copy & paste ya viongozi wote wa ccm na wanachama wenye maslahi binafsi. Hawako tayari kuona tume huru ya uchaguzi maana wanategemea dhuluma pekee kukaa madarakani. Kwao tume huru ni kifo kwa chama chao, hivyo wanatumia huo utetezi ili kufanya watu wasiitake tume huru. Watakubali vipi tume huru huku wanaona idadi ndogo inajitokeza kwenda kujiandikisha kupiga Kura? Na iko wazi hao watu wachache ndio wapiga kura wa ccm.
 
Magufuli ana historia ya kutopenda ushindani katika chaguzi!
Mfano halisi ni uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka jana.
Kiongozi mbabe hushughulikiwa kibabe. Ni vurugu tu ndiyo zinaweza kumfanya huyu bwana asikie madai ya Watanzania ya kupatiwa tume huru itakayosimamia uchaguzi mkuu wa mwaka huu!
Jiwe hubomolewa kwa nyundo au baruti.
 
Hivi aliyevuruga mchakato wa kupata katiba mpya alikuwa nani kama si wale walioshangilia na kusherehekea kukwamisha ushindi wa kuikwamisha upatikanaji wake?
Mle kulipendekezwa kuwepo kwa Tume Huru ya Uchaguzi, hamkuona?
Na hakika dai hili likikubaliwa bado litatoka dai jingine, "Tuunde serikali ya mpito" kufanikisha tume huru, ilimradi kukwamisha mambo yasiende, Miafrika ndivyo tulivyo.
 
Tangia lini muuza chips akaanza kudai tume huru? Sema wanaotaka nafasi huko ndo wadai hyo tume.
 
Tawala za ki Africa, hua mpaka watu waumizane, ndiyo wanaona haja ya kukaa kujadili jambo. Na kwetu hapa watawala wetu hawaoni haja ya kutumia amani kuleta mabadiliko.

Tume huru ni mkuki kwa matendo ya wana CCM dhidi ya vyombo vya dola na vya maamuzi. Hawaoni leo umuhimu wake. Kwao tume hii ya remote control ni huru

Sent using Jamii Forums mobile app


Kwa nini kila kitu huwa mnakimbilia kuisingizia Afrika? Afrika inaingiaje hapo kwenye matatizo yenu?
 
Nondo achana na mambo ya kuunganisha nguvu sijui nini. Kila mtu mwenye nia njema na nchi hii apaze sauti kwa nafasi yake na pale alipo kudai tume huru ya uchaguzi. Haya mambo ya kuunganisha nguvu ndio yalizaa Ukawa kwenye katiba mpya. Matokeo yake ukawa hiyo ndio akina Mbowe wakatuletea viongozi matapeli aina ya kina Lowassa. Leo hao viongozi wa ukawa kila mtu anaongea lake. Ni vyema kelele yetu ikapazwa kila mtu kwa imani yake, na uzuri sisi wananchi tunajitambua na hatushiriki uchaguzi bila kuwa na tume huru.

Dini zote zinamuhubiri Mungu na kumpinga shetani, mbona hawaunganishi nguvu au kuungana ili kumpinga shetani, au kumfikia Mungu? Hiyo kuunganisha nguvu ndio tutajikuta akina Mbowe na kina Zito wanatuletea tapeli lingine la siasa toka ccm kama Membe. Bila tume huru ya uchaguzi hatuko tayari kushiriki uchaguzi, tutafuta njia nyingine ya kupata viongozi, kwa hilo tuko tayari kushirikiana na wazungu, kama ni mbaya acha iwe mbaya?
 
Back
Top Bottom