Tuamini au tusiamini?

Tuamini au tusiamini?

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Sisi wananchi tunataka kuwa katika upande mmoja.Upande wa kuamini au wa kutoamini. Lakini,tunaitegemea Serikali ituaminishe au itufanye tusiamini. Serikali ya chama chetu cha Mapinduzi inazunguka.Inajikanyaga.Inajiuma.Inazunguka mbuyu tu.Haina kauli moja.Haina usawa wa hoja na majibu. Inapishana kutoka huyu hadi yule. Kizungumkuti. Mchafukoge.

Ni kuhusu UDA. Wapo wanaosema mauzo yamefanyika. Mnunuzi ni Saimon Group inayomilikiwa na Robert Kisena. Wapo wanaosema kuwa mauzo hayakufanyika na Kisena na Kampuni yake hawana hata hisa moja. Wapo wanaosema kuwa suala hili lipo TAKUKURU kwakuwa kuna harufu ya rushwa. Wapo wanaosema Serikali itakuja na jibu moja.Wapo waliokana uwepo wa UDA katika Wizara zao. Tuamini au tusiamini?

Tuamini au tusiamini kuwa Serikali haijui kinachoendelea na kilichotokea UDA? Suala hili la UDA linaiaibisha Serikali na chama cha Mapinduzi.Kinaanika udhaifu wa kiuongozi katika Taasisi na Idara za kiserikali zinazoshughulika na UDA katika maisha ya kila siku.

Wananchi wa Tanzania wanataka kujua.Kujua kuhusu UDA.Kujua kuhusu kilichotokea na kinachoendelea UDA. Kumjua mmiliki,mnunuzi,mwendeshaji na kadhalika. UDA haina ukubwa wowote wa kuogofya. Haina ukubwa wowote wa kuwafanya viongozi wetu wapishane katika kauli. Ishughulikiwe haraka.

Tunataka kuamini kuwa Serikali ni moja na inaweza.

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
Sisi wananchi tunataka kuwa katika upande mmoja.Upande wa kuamini au wa kutoamini. Lakini,tunaitegemea Serikali ituaminishe au itufanye tusiamini. Serikali ya chama chetu cha Mapinduzi inazunguka.Inajikanyaga.Inajiuma.Inazunguka mbuyu tu.Haina kauli moja.Haina usawa wa hoja na majibu. Inapishana kutoka huyu hadi yule. Kizungumkuti. Mchafukoge.

Ni kuhusu UDA. Wapo wanaosema mauzo yamefanyika. Mnunuzi ni Saimon Group inayomilikiwa na Robert Kisena. Wapo wanaosema kuwa mauzo hayakufanyika na Kisena na Kampuni yake hawana hata hisa moja. Wapo wanaosema kuwa suala hili lipo TAKUKURU kwakuwa kuna harufu ya rushwa. Wapo wanaosema Serikali itakuja na jibu moja.Wapo waliokana uwepo wa UDA katika Wizara zao. Tuamini au tusiamini?

Tuamini au tusiamini kuwa Serikali haijui kinachoendelea na kilichotokea UDA? Suala hili la UDA linaiaibisha Serikali na chama cha Mapinduzi.Kinaanika udahifu wa kiuongozi katika Taasisi na Idara za kiserikali zinazoshughulika na UDA katika maisha ya kila siku.

Wananchi wa Tanzania wanataka kujua.Kujua kuhusu UDA.Kujua kuhusu kilichotokea na kinachoendelea UDA. Kumjua mmiliki,mnunuzi,mwendeshaji na kadhalika. UDA haina ukubwa wowote wa kuogofya. Haina ukubwa wowote wa kuwafanya viongozi wetu wapishane katika kauli. Ishughulikiwe haraka.

Tunataka kuamini kuwa Serikali ni moja na inaweza.

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Uandishi gani wa kitoto huo? una umri gani wewe? mwalimu gani alikufundisha uandishi wa kuweka nukta kila baada ya neno? watu kama wewe ndio wanafanya walimu wasipandishiwe mishahara.
 
Sisi wananchi tunataka kuwa katika upande mmoja.Upande wa kuamini au wa kutoamini. Lakini,tunaitegemea Serikali ituaminishe au itufanye tusiamini. Serikali ya chama chetu cha Mapinduzi inazunguka.Inajikanyaga.Inajiuma.Inazunguka mbuyu tu.Haina kauli moja.Haina usawa wa hoja na majibu. Inapishana kutoka huyu hadi yule. Kizungumkuti. Mchafukoge.

Ni kuhusu UDA. Wapo wanaosema mauzo yamefanyika. Mnunuzi ni Saimon Group inayomilikiwa na Robert Kisena. Wapo wanaosema kuwa mauzo hayakufanyika na Kisena na Kampuni yake hawana hata hisa moja. Wapo wanaosema kuwa suala hili lipo TAKUKURU kwakuwa kuna harufu ya rushwa. Wapo wanaosema Serikali itakuja na jibu moja.Wapo waliokana uwepo wa UDA katika Wizara zao. Tuamini au tusiamini?

Tuamini au tusiamini kuwa Serikali haijui kinachoendelea na kilichotokea UDA? Suala hili la UDA linaiaibisha Serikali na chama cha Mapinduzi.Kinaanika udahifu wa kiuongozi katika Taasisi na Idara za kiserikali zinazoshughulika na UDA katika maisha ya kila siku.

Wananchi wa Tanzania wanataka kujua.Kujua kuhusu UDA.Kujua kuhusu kilichotokea na kinachoendelea UDA. Kumjua mmiliki,mnunuzi,mwendeshaji na kadhalika. UDA haina ukubwa wowote wa kuogofya. Haina ukubwa wowote wa kuwafanya viongozi wetu wapishane katika kauli. Ishughulikiwe haraka.

Tunataka kuamini kuwa Serikali ni moja na inaweza.

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Kaka hebu tujuze kilichotokea dodoma kwenye kikao cha chama.
 
Uandishi gani wa kitoto huo? una umri gani wewe? mwalimu gani alikufundisha uandishi wa kuweka nukta kila baada ya neno? watu kama wewe ndio wanafanya walimu wasipandishiwe mishahara.

Lakini mwandishi ameeleweka. Jibu au changia mada kama unajeuri. Usilete hadithi zako ili kutuondoa kwenye mjadala.
 
Uandishi gani wa kitoto huo? una umri gani wewe? mwalimu gani alikufundisha uandishi wa kuweka nukta kila baada ya neno? watu kama wewe ndio wanafanya walimu wasipandishiwe mishahara.
MCHUNGUZI HURU halafu hujui hata uandishi!? Kijana,hufai kuwa CCM. Tunahitaji vijana tofauti na wewe.

Mzee Tupatupa

 
Last edited by a moderator:
Subiri ripoti ya TAKUKURU

Kazi za CAG zinajulikana zinaonekana matunda yake...haya tuambie hiyo TAKUKURU imewahi kufanikiwa kupeleleza kesi ipi na kufanikiwa kuchukua hatua kwa maslahi mapana ya Taifa?...Wajinga ndio waliwao...
 
"Wananchi wa Tanzania wanataka kujua.Kujua kuhusu UDA.Kujua kuhusu kilichotokea na kinachoendelea UDA. Kumjua mmiliki,mnunuzi,mwendeshaji na kadhalika. UDA haina ukubwa wowote wa kuogofya. Haina ukubwa wowote wa kuwafanya viongozi wetu wapishane katika kauli. Ishughulikiwe haraka.

Tunataka kuamini kuwa Serikali ni moja na inaweza."

Hiyo ni mali ya mwana wa mfalme. Huo ubabaishaji wa the so called serikali (mimi ninaamimi hatuna serikali bali genge la mahayawani, lakini tuiite serikali) hautokei kwa bahati mbaya. Ni namna ya kupoteza lengo. Nitakupa Tsh milioni 10 kama hili suala litakuwa kwenye magazeti ya Bongo au linaongolewa tena hapa JF ifikapo wiki kesho. Mfalme mwenyewe amekwenda kumwakilisha Mama Sofia katika mkutano wa mama na mwana huko canada!!
 
Kazi za CAG zinajulikana zinaonekana matunda yake...haya tuambie hiyo TAKUKURU imewahi kufanikiwa kupeleleza kesi ipi na kufanikiwa kuchukua hatua kwa maslahi mapana ya Taifa?...Wajinga ndio waliwao...

Buku saba huyo mkuu achana naye.
 
Uandishi gani wa kitoto huo? una umri gani wewe? mwalimu gani alikufundisha uandishi wa kuweka nukta kila baada ya neno? watu kama wewe ndio wanafanya walimu wasipandishiwe mishahara.
Kama kosa ni la kimantiki sawa tueleze ila kama ni tatizo la misspelling wewe ndiye una mawazo ya kitoto.
 
Umeruka makusudi Mkuu Tupa Tupa wa Lumumba kuhusu mtoto wa raisi kuhusishwa na ukwapuaji wa UDA,he ndio maana mawaziri na bunge la maCCM mnajikanganya??!!

Ikiwa pia Kasena huyu huyu na Kigwangala ambae alitetea UDA kupewa Kasena walifaidika na pesa za Stimulus Package ambapo hadi leo serikali imegoma kuyataja makampuni yaliyofaidika kwa vigezo gani inatoa picha gani??!! Dr huyo aliewahi kuhonga watu vitumbua kule Tabora na alikuwa mtumishi wa WAMA maCCM Mnataka tuamini nini??!!!
 
Uandishi gani wa kitoto huo? una umri gani wewe? mwalimu gani alikufundisha uandishi wa kuweka nukta kila baada ya neno? watu kama wewe ndio wanafanya walimu wasipandishiwe mishahara.

Mwandishi amefikisha ujumbe vizuri sana, si kwa maneno tu, bali zaidi katika namna ya uandishi alioutumia. Uandishi wake ni wa kutoa hisia kwa kuandika kila hoja katika sentesi fupi. Kwa kufanya hivyo anatilia mkazo kila hoja na kuonyesha uwingi wa hoja ulivyo.

Sijui ni kwa kiasi gani ambacho fasihi ya Kiswahili inafundishwa siku hizi. Hata hivyo wakati ule nikisoma High School miaka ya 1970, tulikuwa tunafundishwa namna ya kutafsiri hisia za mwandishi kwa namna ya uandishi wake. Kwa kifupi tu kuna aina mbalimbali za uandishi.
 
Back
Top Bottom